Tetesi: Kitila Mkumbo kumvaa Mwigulu Nchemba Iramba Magharibi

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,358
WanaJF

Habari ambazo zinaenea ni kwamba Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Dr Kitila Mkumbo anajiandaa kugombea ubunge Iramba Magharibi 2020 kupitia CCM.

Taarifa za uhakika kutoka kwa watu kadhaa wa karibu na Dr Kitila ni kwamba kiongozi huyo aliyejitenga na ACT hivi karibuni anatarajia kujiunga CCM siku si nyingi kutoka sasa.

Baadhi ya viongozi wa CCM Iramba Magharibi wamegawanyika makundi mawili huku kundi moja likimuunga mkono Mwigulu Nchemba mbunge wa sasa na kundi lingine likimuunga mkono Dr Kitila.

Dr Kitila amekuwa akilitamani kwa udi na uvumba jimbo hilo tangu akiwa Chadema ila kizingiti kikubwa kilikuwa Mwigulu Nchemba.

Kwa sasa Dr Kitila ana uhakika wa kumuondoa Mwigulu kwa kile kinachosemekana anaungwa mkono na ngazi za juu
 
Kwa katiba ya CCM, mpaka atimize miaka mitano ya uanachama,
 
Nchi huru hii, mwenyewe hapa najiandaa kuchukua kadi Chadema na kumng'oa Mbowe nafasi ya uenyekiti maana naona walioko huko wote wanaogopa.
 
Wakumbuke tu wamekuwa wa mwisho katika matokeo ya daraja la saba.
Hilo hawa mabwana walijue waone wanasaidiaje kukuza taaluma maana wamepitwa mpaka na mikoa iliyozoelea nafasi hizo
Nchemba mpaka leo hajaleta mkakati wowote wa namna ya kuinua taaluma jimboni kwake sijui huyu mwalimu ataweza?
Sina imani sana na madokta wala maprofessa huwa wanatuangusha Mara kwa mara
 
Acha kupiga kampeni muda bado mtu wako asije akakatwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…