Pre GE2025 Kitila Mkumbo: Nimejipanga vilivyo kugombea Ubunge 2025, msije kudharau nyoka mdogo sumu ni ile ile!

Pre GE2025 Kitila Mkumbo: Nimejipanga vilivyo kugombea Ubunge 2025, msije kudharau nyoka mdogo sumu ni ile ile!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Kash kash zimeanza rasmi sasa!

=====

Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, Januari 1, 2025, amewahutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wa Jimbo la Ubungo katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika Ubungo Plaza.

Pia soma: Orodha ya CV za Wabunge kwa mwaka 2020 - 2025 kutoka kila mkoa Tanzania

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkumbo ameeleza dhamira yake ya kugombea tena nafasi ya ubunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu wa 2025, huku akitoa onyo kali kwa watu wanaonyemelea jimbo la Ubungo.

"Sasa mimi niseme mambo mawili, kwasababu katika hizi harakati kuna watu wanapitapita, mimi ni mzoefu wa mapambano ya kisiasa, kama umeamua kugombea, gombea sawasawa bila ujanjaujanja", ameeleza Prof. Kitila.

Ameongeza kuwa uchaguzi ni sawa na vita, na kwamba yeye binafsi amejiandaa kikamilifu kwa ushindani wa mwaka 2025.

 
Jimbo la Ubungo lina shida kubwa kwenye upatikanaji endelevu wa huduma ya maji pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara (mfano ile ya Kimara - Bonyokwa - Kinyerezi & Kimara - Matosa). Anahitajika Mbunge mwenye ushawishi mkubwa na mbinu za kufanikisha haya mambo

Sina uhakika kama Kitila Mkumbo anaweza kuyafanikisha haya mambo ila nina uhakika mgombea wa Ubunge kutoka Chama cha Upinzani hatoweza kuyapigania mpaka yakatokea - let alone kuconvince wapiga kura, especially if vyama vitaleta wapiga kelele kama Boni Yai
 
Badala ya kutumia muda huu ambao Kodi zetu zinamlipa kufanya mambo anaongelea kugombea..., Ingekuwa ni kunufaisha wananchi angefanya hivyo sasa sababu anawigo wa kufanya hivyo..., ila ndio hivyo kama kawaida ya hivi so called vyama vya siasa ila ukweli ni platforms za kutafuta Kura ili kwenda Kula
 
Wakuu,

Kash kash zimeanza rasmi sasa!

=====

Mbunge wa Jimbo la Ubungo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, Januari 1, 2025, amewahutubia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wa Jimbo la Ubungo katika hafla ya kuukaribisha mwaka mpya iliyofanyika Ubungo Plaza.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkumbo ameeleza dhamira yake ya kugombea tena nafasi ya ubunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu wa 2025, huku akitoa onyo kali kwa watu wanaonyemelea jimbo la Ubungo.

"Sasa mimi niseme mambo mawili, kwasababu katika hizi harakati kuna watu wanapitapita, mimi ni mzoefu wa mapambano ya kisiasa, kama umeamua kugombea, gombea sawasawa bila ujanjaujanja", ameeleza Prof. Kitila.

Ameongeza kuwa uchaguzi ni sawa na vita, na kwamba yeye binafsi amejiandaa kikamilifu kwa ushindani wa mwaka 2025.
P lipi neno lako,sumu yako iko chini ya viwango vinavyohitajika,nini?
 
Jimbo la Ubungo lina shida kubwa kwenye upatikanaji endelevu wa huduma ya maji pamoja na ubovu wa miundombinu ya barabara (mfano ile ya Kimara - Bonyokwa - Kinyerezi & Kimara - Matosa). Anahitajika Mbunge mwenye ushawishi mkubwa na mbinu za kufanikisha haya mambo

Sina uhakika kama Kitila Mkumbo anaweza kuyafanikisha haya mambo ila nina uhakika mgombea wa Ubunge kutoka Chama cha Upinzani hatoweza kuyapigania mpaka yakatokea - let alone kuconvince wapiga kura, especially if vyama vitaleta wapiga kelele kama Boni Yani
Boni yai kajimaliza kwa kumkampenia Mbowe.
 
Watu tunazungumzia Uraisi we unaleta habali za ubunge.
 
Back
Top Bottom