Kitimoto rost, ndizi mbili na mirinda nyeusi baridi

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Somewhere in Kigogo Sambusa....

Katika utulivu wa hali ya juu najiuliza haya maisha yangekuwaje bila kitimoto rost, ndizi mbili na kachumbari pembeni? Kungekua na mbadala wake?.... nikiwa ndani ya tafakuri nzito, namwona Dada nadhifu na mrembo akisogelea mezani kwangu kashikilia sinia lenye kitimoto safi imeiva kiwango cha juu.. ni ufundi wa Shirima. Anafika na kuninawisha mikono kisha kutenga vitu na kuanza kuondoka na sinia. Wakati akiondoka namsihi aniletee Pepsi ya baridi.

Basi kazi ikaanza taratibu, yaani one-touch, finyango baada ya finyango. Ile ndo mwendo unaanza kushika kasi, mara ghafla simu ikaanza kuita..... nikajiuliza kwa hasira ni nani huyu anayeweza kunipigia nikiwa kwenye starehe kama hii??..😬😑😑..

Sasa wakati naitoa simu mfukoni kwa bahati mbaya ikaniponyoka.... kwenye harakati za kuiwahi isianguke nikajikuta nimesukuma ile meza ya plastic.... KITIMOTO yote na ile soda ikamwagika.. Aaarghh!!😬😬.. kuja kukaa sawa tayari yule mdada kashafuta meza na kusafisha pale chini huku akidai chake......
 
Mungu alikupenda kukuepushia kuendelea kula mafunza na wadudu, unachotakiwa ushukuru, Afya muhim sana
 
Punguza kupenda tumbo mkuu
 
Mungu alikupenda kukuepushia kuendelea kula mafunza na wadudu, unachotakiwa ushukuru, Afya muhim sana
hao wadudu na mafunza hata mwilini mwako wapo kwahiyo hawana madhara kama wangekua na madhara tungeona kwa babu zetu wanalioanza kula miaka 60 iliyopita na mpaka leo wapo na wananguvu maradufu
 
hao wadudu na mafunza hata mwilini mwako wapo kwahiyo hawana madhara kama wangekua na madhara tungeona kwa babu zetu wanalioanza kula miaka 60 iliyopita na mpaka leo wapo na wananguvu maradufu
Acheni ukaidi
 
Picha hata ya Huyo dada anaekudai imeshindkana?
 
Wengine postini issue za udi na ubani huku tuacheni wenye akili. Haya weka picha Wewe. Na utoe direction vizuri. Wavaa msuli hoiiiii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…