Kitu gani cha thamani uliwahi kusahau au kudondosha na ukakipata au ukakikosa?

Kitu gani cha thamani uliwahi kusahau au kudondosha na ukakipata au ukakikosa?

Mwanafunzi mtoro

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2021
Posts
222
Reaction score
806
Habari waungwa sana wa JF

Leo nimeona nami nijaribu kushea tukio moja ambalo kila nikikumbuka nabaki kusema ni mungu tu.

Siku hiyo asubuhi naelekea stendi kupanda gari ya kuelekea Dar es salaam. Siku moja kabla ya safari nilitanguliza mizigo miwili ya kukaa kwenye buti. Sasa asubuhi nilibeba begi la mgongoni tu hadi stendi . Nilipofika booking office nililiacha begi ndani kisha nikatoka kwenda kukojoa.

Kwakuwa stendi haikuwa Mwanza mjini basi tulikuwa tunasubiri iingie stendi ndogo ili tupande. Wakati narudi tu toka kichakani ghafla basi likawa limeingia. Katika harakaharska tukaifata mizigo miwili tukaweka kwenye buti kisha nikapanda ndani ya gari.

Wakati gari inakaribia maeneo ya Hungumalwa ndio nakumbuka begisikupanda nalo kwenye basi na wala halipo kwenye buti. Nilihisi kuzimia .Nilihisi labda begi nililisahau wakati wa kupakia mzigo kwenye buti nilizidi kuchanganyikiwa nilihisi mwili unaganda.

Begi sio kitu kilichonichanganya bali kwenye begi kulikuwa na laki 8+ . Pesa hizi nilisahau kuingiza kwenye akaunti baada ya kuagiza bidhaa flani kisha kusubiri kama zitapatikana zingine nitume tena . Nikaona haina haja kuweka mfukoni kwakuwa begi nipo nalo acha niweke huko .

Nikajipa utulivu kisha kumfata dereva anishushe. Wakati anatafuta mahali pa kunishusha nikawa nawasiliana na ajenti ambaye tunafahamiana sana. Akanambia nimelisahau kwenye ofisi..hapo nikapumua. Kisha baada ya hapo nikamweleza hilo begi lina pesa.

Nashukuru alipata basi la kunifukuzia hadi niliposhuka. Na hilo basi ndio nilipanda mimi kuendelea na safari.
Hasara ndogo niliyopata ni kuwa basi la kwanza nililipia mizigo ga kwenye buti elfu 10. Kisha karudishiwa elfu 15. Basi la pili nililipa elfu 30 kwakuwa nilikuwa nashuka Morohoro


Tupe mkasa wako na wewe ni kitu gani ulisahau na ukakipata?
 
Nilidondosha noti za dola mia tano kumi pale ubungo nimestukia nipo ostabay nikarud nikazikuta nilisali kujushukuru kwa kuwa na moyo wa kurud
 
Niliwahi msahau ex wangu kwenye gari la Mwenge Posta.

Tumetoka Coco nikawa nimenunua juisi za Sunvita mbili akasema nimshikie.

Pale Mbuyuni tumepanda gari ili twende kwetu, kufika Victoria mi nikashuka nachanja mbuga kwenda nyumbani.

Akili ikaclick kwamba mbona nina Sunvita mbili? Memory ilivyorudi nikajiongeza tu kwamba leo hakatwi mtu. Hapo nimefika kwa Kimbau, naamini kwa muda huo kashafika Millennium tower.

Nikafungua na Sunvita yake nikanywa.
 
Nliokota simu kwenye basi.

Ile nashuka kituoni usiku wa saa5 mi nlikuwa siti ya nyuma kabisa muda tunashuka mlangoni watu nyomi balaa bodaboda, bajaji na tax wanagombea abiria nikasema ngoja hizi fujo zipungue nami nishuke.

Baadae nashuka wakati huo taa za ndani ya basi zimewashwa naona bonge la smartphone chini ya siti nikaiokota kuicheki imezima nikashuka nayo ilikuwa na Samsung A9 pro(19).

Nikasepa nayo home nikaichaji nikaiwasha nikasubiri huenda mwenye nayo ataitafuta.

Hadi asubuhi bilabila nikasachi majina nikaona namba ambayo alikuwa anachati nayo mara kwa mara nikampigia kumjuza kama anamfahamu mwenye simu, akaniunganisha naye kesho yake nikampatia simu yake.

Kidogo tamaa iniingie maana mi nlikua natumia Samsung s5.

Yule mama alinipa 50K

View attachment 2158254
 
Nliokota simu kwenye basi.

Ile nashuka kituoni usiku wa saa5 mi nlikuwa siti ya nyuma kabisa muda tunashuka mlangoni watu nyomi balaa bodaboda, bajaji na tax wanagombea abiria nikasema ngoja hizi fujo zipungue nami nishuke.

Baadae nashuka wakati huo taa za ndani ya basi zimewashwa naona bonge la smartphone chini ya siti nikaiokota kuicheki imezima nikashuka nayo ilikuwa na Samsung A9 pro(18).

Nikasepa nayo home nikaichaji nikaiwasha nikasubiri huenda mwenye nayo ataitafuta.

Hadi asubuhi bilabila nikasachi majina nikaona namba ambayo alikuwa anachati nayo mara kwa mara nikampigia kumjuza kama anamfahamu mwenye simu, akaniunganisha naye kesho yake nikampatia simu yake.

Kidogo tamaa iniingie maana mi nlikua natumia Samsung s5.

Yule mama alinipa 50K
Hongera mkuu kwa kuishinda nafc
 
Nliokota simu kwenye basi.

Ile nashuka kituoni usiku wa saa5 mi nlikuwa siti ya nyuma kabisa muda tunashuka mlangoni watu nyomi balaa bodaboda, bajaji na tax wanagombea abiria nikasema ngoja hizi fujo zipungue nami nishuke.

Baadae nashuka wakati huo taa za ndani ya basi zimewashwa naona bonge la smartphone chini ya siti nikaiokota kuicheki imezima nikashuka nayo ilikuwa na Samsung A9 pro(18).

Nikasepa nayo home nikaichaji nikaiwasha nikasubiri huenda mwenye nayo ataitafuta.

Hadi asubuhi bilabila nikasachi majina nikaona namba ambayo alikuwa anachati nayo mara kwa mara nikampigia kumjuza kama anamfahamu mwenye simu, akaniunganisha naye kesho yake nikampatia simu yake.

Kidogo tamaa iniingie maana mi nlikua natumia Samsung s5.

Yule mama alinipa 50K
Una roho nzuri sana



Mi sirudishi nauza
 
Nliokota simu kwenye basi.

Ile nashuka kituoni usiku wa saa5 mi nlikuwa siti ya nyuma kabisa muda tunashuka mlangoni watu nyomi balaa bodaboda, bajaji na tax wanagombea abiria nikasema ngoja hizi fujo zipungue nami nishuke.

Baadae nashuka wakati huo taa za ndani ya basi zimewashwa naona bonge la smartphone chini ya siti nikaiokota kuicheki imezima nikashuka nayo ilikuwa na Samsung A9 pro(18).

Nikasepa nayo home nikaichaji nikaiwasha nikasubiri huenda mwenye nayo ataitafuta.

Hadi asubuhi bilabila nikasachi majina nikaona namba ambayo alikuwa anachati nayo mara kwa mara nikampigia kumjuza kama anamfahamu mwenye simu, akaniunganisha naye kesho yake nikampatia simu yake.

Kidogo tamaa iniingie maana mi nlikua natumia Samsung s5.

Yule mama alinipa 50K
Safi sana Moyo huo ndio tulizaliwa nayo maeneo tunayoishi ndio yameubadilisha
 
Ilikuwa mwaka 2004 natoka zangu Mzuzu Malawi narudi Mbeya nimefika kitaa najikuta sina passport ikabidi niende Police kutoa maelezo ili nipate barua ya kwenda uhamiaji. Kufika pale uhamiaji baada ya kuwaeleza na kuonyesha ile paper wakapanic na kunirudisha central wakanisweka ndani ati madai yao nimefanya uzembe, walipoondoka hata sikukaa sana ndani askari wakanitoa wenyewe wakaniambie we nenda zako basi niliacha kufatilia hizo mambo hadi ninavyoandika hapa sina mkoba tena enzi zile passport za kitabu.
 
Ilikuwa mwaka 2004 natoka zangu Mzuzu Malawi narudi Mbeya nimefika kitaa najikuta sina passport ikabidi niende Police kutoa maelezo ili nipate barua ya kwenda uhamiaji. Kufika pale uhamiaji baada ya kuwaeleza na kuonyesha ile paper wakapanic na kunirudisha central wakanisweka ndani ati madai yao nimefanya uzembe, walipoondoka hata sikukaa sana ndani askari wakanitoa wenyewe wakaniambie we nenda zako basi niliacha kufatilia hizo mambo hadi ninavyoandika hapa sina mkoba tena enzi zile passport za kitabu.
Unatatizo unawekwa ndani tena. Pole sana
 
Nliokota simu kwenye basi.

Ile nashuka kituoni usiku wa saa5 mi nlikuwa siti ya nyuma kabisa muda tunashuka mlangoni watu nyomi balaa bodaboda, bajaji na tax wanagombea abiria nikasema ngoja hizi fujo zipungue nami nishuke.

Baadae nashuka wakati huo taa za ndani ya basi zimewashwa naona bonge la smartphone chini ya siti nikaiokota kuicheki imezima nikashuka nayo ilikuwa na Samsung A9 pro(18).

Nikasepa nayo home nikaichaji nikaiwasha nikasubiri huenda mwenye nayo ataitafuta.

Hadi asubuhi bilabila nikasachi majina nikaona namba ambayo alikuwa anachati nayo mara kwa mara nikampigia kumjuza kama anamfahamu mwenye simu, akaniunganisha naye kesho yake nikampatia simu yake.

Kidogo tamaa iniingie maana mi nlikua natumia Samsung s5.

Yule mama alinipa 50K
Hongera kijana
 
Kuna mama alituma 300k kimakosa kwenye simu yangu 2013 nliiacha siku 2 haitolewi akanipigia baadae nikairudisha
 
Nilipoteza funguo ya gari aina ya Lexus na nilikua nayo hiyo hiyo. Halafu ilikua ni gari ya shemeji yangu ambayo nilikua napigia misele plus kipindi hiko bado Jobless na nikaambiwa yeye anachohitaji ni gari na funguo tu.. [emoji3][emoji3]..Sitokuja rudia uzembe kama huo...
 
Back
Top Bottom