Kitu gani kinachomfanya Dkt. Bashiru aweweseke hadi kutamani Membe arejee CCM?

Kitu gani kinachomfanya Dkt. Bashiru aweweseke hadi kutamani Membe arejee CCM?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Kutokana na kauli alizotoa mfululizo katika siku chache zilizopita, mtu yeyote hana budi kujiuliza swali, kulikoni tena Dkt Bashiru amepoa na kutaka kujirudi hadi "kutamani" Membe aweze rejea CCM?

Ametamka mwenyewe Dkt Bashiru, akiwasihi wanaccm wenzake, wasisheherekee kufukuzwa kwa kada maarufu wa Chama hicho cha CCM, Bernard Membe, kwa kuwa kumpoteza mwanachama maarufu kiasi hicho kwenye chama ni msiba mzito!

Ameendelea kusema kuwa yeye mwenyewe amesaini barua 14 za wanachama waliotimuliwa CCM na wakaomba msamaha na kurejea tena CCM, kwa hiyo anaisubiri kwa hamu sana barua ya Membe ya kuomba msamaha na hiyo itakuwa barua ya 15 kuisaini na kumrejesha "mwana mpotevu" kundini!

Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hii U turn ya Dkt Bashiru, imetokana na nini?

Si ndiyo hao hao CCM walikuwa wakitamba kwenye majukwaa ya kisiasa, wakimtukana Membe, kuwa chama cha CCM, kuwa ni "baba lao" kwa hiyo hakuna mwanachama, anayeweza kujiona yuko juu ya Chama?

Hivi kumbe chama hicho cha CCM kinatumia vitisho kuwatimua wanachama wake, kikijua kuwa hawajafanya makosa yoyote na baadaye kutegemea wanachama hao watapiga magoti na kuomba msamaha ili warejee kwenye chama chao?

Ina maana baada ya kupima upepo wa kisiasa unavyovuma, huku ukizingatia kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu, ndipo Dkt Bashiru ameshituka na kuona hatari kutokana na vitendo vyao vya visasi, vilivyosababisha Membe avuliwe uanachama wake?

Kumbe CCM wameanza utamaduni mpya wa kidemokrasia kwenye Chama Chao, ambapo kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kwenye chama hicho, inahesabika kuwa ni kosa kubwa la jinai, ambapo unaweza hata kustahili kufukuzwa kwenye chama hiko?

Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa Membe hakuwa na kosa lolote la kufanya Chama hiko kimfukuze uanachama wake na ndiyo sababu zinazofanya Dkt Bashiru ajutie nafsi yake ya "kutumika" kumtoa Membe, kwa kosa tu la kuonyesha nia ya kugombea Urais, ndani ya chama cha CCM, kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa 2020

Hivi tangu lini mtu kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kwenye Chama cha CCM, ikawa kosa kubwa, hadi kusababisha mtu kuweza kufukuzwa kwenye chama hicho?

Tujiulize swali jingine dogo, hivi ni kwanini hao kina Membe, waliolalamika kuwa huyu Musiba ni nani ndani ya nchi hii, hadi "aruhusiwe" kuwatukana viongozi wakubwa wa CCM, waliostaafu kadri atakavyo na vyombo vya usalama wa nchi, vipigwe "ganzi" na kuogopa kumchukulia hatua zozote za kishetia?

Maswali yako mengi yanayokosa majibu, lakini itoshe kwa hayo maswali machache, niliyoyaorodhesha, ambayo nimeuliza ni kwanini Dkt Bashiru, akose raha kabisa, kwa kumfukuza Membe, kwa sababu tu ya kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kupitia CCM, kuwa ndiyo kosa lake kuu, lililomfanya mwanachama huyo Membe, apoteze uanachama wake?
 
Mkuu Mikakati ya CCM ni kwamba Apatikane Mgombea wa Kushindana na Magu..

Ili kuiaminisha Dunia kwamba demokrasia ipo Tanzania..

Walitegemea hasira za Membe asingemaliza saa 24 bila kujiunga na Upinzani na kutangaza nia.

Bashiru anajaribu kuwaaminisha Upinzani Kwamba Membe ni Tunu kwamba hata wao bado wanamuhitaji .UONGO..

plan B ndiyo hiyo ya kuita Upinzani kutafuta Maridhiano ..Maana Membe bado hajasomeka.
 
Nadhani hujamwelewa vizuri Bashiru alichokisema rudia tena kumsikiliza au umemwelewa na unataka kujipotosha Tu na nafsi yako
 
Kwanini wang'ang'anie kubaki CCM, kwani chama kina walipa au ndio kungoja subira za mwenyekiti awateuwe? kwanini watu wasiwe na free minds za kutafuata mkate kwa nguvu na jasho? Hivi vya kupewa, mara kuteuliwa unakuwa kama MWANAMKE MWENYE EXPECTETIONS ZA KUHONGWA.
 
Mkuu Mystery,

Ngoja nikupe jibu fupi, halafu ulitafakari kwa makini, pengine unaweza kuona njia zinazotumika hazijabadilika tokea siku ya kwanza ya Mh Rais Magufuli anazozitumia kusawazisha njia.

Alianza kwa vitimbi vya kuwaweka akina Lema Mhabusu na jela, ili akili ziwaingie kichwani, wafuate anayoyataka yeye.

Hayo mengine ya hapo katikati, nayaruka, lakini yote yanajulikana kuwa ndizo mbinu zake za kuwalainisha wanaompinga.

Tumepiga hatua sasa, hadi za kuwanunua wanaoonyesha bei inawatosha

Sasa hivi singo inayoonekana kuuzwa ni ya akina Lipumba na Maalim Seif, hatujui itaishia wapi, nao bei itatosha? Lipumba kwa mara ya pili?

Kama'vitisho na kutia woga' havifanyi kazi, je vyeo na pesa nazo huvitaki? Wewe utakuwa ni 'special' kama akina Mbowe na wenzake kadhaa.

Unakumbuka biashara zilivyovurugwa. Akina Lowassa na Sumaye wakamwaga manyanga, mchezo ni ule ule haujabadilika hadi hii leo.

Akina Kinana je, huoni 'trend' ni ile ile? Watafutie jambo, halafu uwanyamazishe!

Sasa kama huwezi kusoma haya ya Membe na kuyaweka sambamba na hayo yaliyopita, nadhani utakuwa unatafuta nadharia mpya ambayo haipo.

Huyu dogo Bashiru atahangaika sana.
 
prs,
Nasikitika na pia nashangaa kuona hadi hivi sasa huna Likes nyingi kwa hiki ulichokiandika wakati katika Wachangiaji wote niliowaona hapa walioandika Kitu sahihi na cha uhakika tena wa 99.9% ni Wewe.

Hongera sana Mdau kwani umewasilisha Kitu chenye kuhitaji Upeo mkubwa Kukielewa. Upo vizuri mno Kichwani.
 
Kalamu1,
Kwa hiyo kwa maana nyingine ni kuwa huyu Jiwe hayupo tayari kabisa kusikia demokrasia ya vyama vingi, wa kufanya uchaguzi huru na wa haki kwa kupitia sanduku la kura, ambapo wananchi ndiyo wanawachagua wawikilishi wao, bali anachoamini yeye ni kuwa analoamini yeye na kulitekeleza ndiyo sahihi kwa asilimia 100
 
Kutokana na kauli alizotoa mfululizo katika siku chache zilizopita, mtu yeyote hana budi kujiuliza swali, kulikoni tena Dkt Bashiru amepoa na kutaka kujirudi hadi "kutamani" Membe aweze rejea CCM?

Ametamka mwenyewe Dkt Bashiru, akiwasihi wanaccm wenzake, wasisheherekee kufukuzwa kwa kada maarufu wa Chama hicho cha CCM, Bernard Membe, kwa kuwa kumpoteza mwanachama maarufu kiasi hicho kwenye chama ni msiba mzito!

Ameendelea kusema kuwa yeye mwenyewe amesaini barua 14 za wanachama waliotimuliwa CCM na wakaomba msamaha na kurejea tena CCM, kwa hiyo anaisubiri kwa hamu sana barua ya Membe ya kuomba msamaha na hiyo itakuwa barua ya 15 kuisaini na kumrejesha "mwana mpotevu" kundini!

Ndipo hapo ninapojiuliza hivi hii U turn ya Dkt Bashiru, imetokana na nini?

Si ndiyo hao hao CCM walikuwa wakitamba kwenye majukwaa ya kisiasa, wakimtukana Membe, kuwa chama cha CCM, kuwa ni "baba lao" kwa hiyo hakuna mwanachama, anayeweza kujiona yuko juu ya Chama?

Hivi kumbe chama hicho cha CCM kinatumia vitisho kuwatimua wanachama wake, kikijua kuwa hawajafanya makosa yoyote na baadaye kutegemea wanachama hao watapiga magoti na kuomba msamaha ili warejee kwenye chama chao?

Ina maana baada ya kupima upepo wa kisiasa unavyovuma, huku ukizingatia kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu, ndipo Dkt Bashiru ameshituka na kuona hatari kutokana na vitendo vyao vya visasi, vilivyosababisha Membe avuliwe uanachama wake?

Kumbe CCM wameanza utamaduni mpya wa kidemokrasia kwenye Chama Chao, ambapo kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kwenye chama hicho, inahesabika kuwa ni kosa kubwa la jinai, ambapo unaweza hata kustahili kufukuzwa kwenye chama hiko?

Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa Membe hakuwa na kosa lolote la kufanya Chama hiko kimfukuze uanachama wake na ndiyo sababu zinazofanya Dkt Bashiru ajutie nafsi yake ya "kutumika" kumtoa Membe, kwa kiss tu cha kuonyesha nia ya kugombea Urais, ndani ya chama cha CCM, kwenye uchaguzi wa mwaka huu wa 2020

Hivi tangu lini mtu kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kwenye Chama cha CCM, ikawa kosa kubwa, hadi kusababisha mtu kutimuliwa kwenye chama chake?

Tujiulize swali jingine dogo, hivi ni kwanini watu waliolalamika kuwa huyu Musiba ni nani ndani ya nchi hii, hadi "aruhusiwe" kuwatukana wanachama wengine, kadri atakavyo na vyombo vya usalama wa nchi, vipigwe "ganzi" na kuogopa kumchukulia hatua zozote za kishetia?

Maswali yako mengi yanayokosa majibu, lakini itoshe kwa hayo maswali machache, niliyoyaorodhesha, ambayo nimeuliza ni kwanini Dkt Bashiru, akose raha kabisa, kwa kumfukuza Membe, kwa sababu tu ya kuonyesha nia ya kutaka kugombea Urais kupitia CCM, kuwa ndiyo kosa lake kuu, lililomfanya mwanachama huyo Membe, apoteze uanachama wake?
Bashiru ameongea ki-diplomasia, JPM ameongea na akina Maalim Seif na wenzake; hamuoni kwamba kuna dalili njema; mnataka nini?
Waacheni, wapeni muda watafakari what next!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom