Lizzy,
Ni yapi hayo?? Nimesema akili imegota Kigoma mwisho wa reli mwenzenu!!
Hahahaha....MJ mami hata kumdanganya mwajiri kwamba umeshindwa kwenda kazini leo kwasababu umekwama kwenye foleni ya mafuta ni dhambi kwasababu UMEDANGANYA japo uongo wenyewe hauna madhara kiviiiile!!!
Babu DC nikwambie kitu...mi hua nasema hivi dhambi ni dhambi iwapo kilichofanyika kitakua na madhara either kwa mtendwa au mtenda!Na ukubwa wa dhambi (kwangu mimi) unaonyeshwa kwa ukuvwa wa dhara litakalotokana na hicho kitendo!!
Kwa maelezo hayo naomba nikwambie dhambi kwa nnavyoina mimi na sio collectively!!
Kumdanganya mwajiri iwapo uwongo wako unamcost yeye...if not ahhh well kila mtu anastahili break now and then.
Kumwibia mtu ambae kureplace kile ulichomwibia itakua kazi sana kwake.Mfano ni kumwibia mama mfanya biashara wa nyanya za reja reja mtaa kwa mtaa simu ya sh. 40,000 maana kuipata alijipinda sana so thats to me is unfair.Ila ukimwibia mwingine ya million kama 20 bank ahhj naona poa tu hata kama ni mimi nimeibiwa!Na nilishawahi kuibiwa na mwizi wangu nikamjua ila nilimsehe kwa sababu hii hii!
Kumcheat mtu ambae ni mwaminifu kwako..,ila kama wote ndo wale wale wakomoane tu!!
Kumsingizia/kumtuhumu mtu kitu ambacho ni uongo!!Inamuumiza sana mhusika!!!
Kutamani kitu usicho na uwezo nao hata kufikia kufanya mambo ya ajabu ili kukipata!!Mf. Kumwendea mwabaume kwa mganga...kuiba...kudhulumu...n.k
Kumdhulumu yatima...mtu ambae hana kwingine kwa kukimbilia so unfair!!
Kumsingizia/mpakazia mtu kitu hata kufikia kumharibia sifa yake na kumchafua kwenye jamii/familia haifai kabisa!!
Chuki mbaya mpaka kufikia kumuumiza mtu iwe physically au pschologically.Ila kama unamchukia tu mtu basi heey go ahead and ridhisha moyo wako!
Kulaani/kuita watoto majina ya ajabu ajabu mpaka wakafikia kukua na hizo character mbaya ulizowatupia!!
Kuua kwa kukusudia!
Kumprovoce mtu hata akafanya kitu ambacho mwanzoni hakuwahi kukifikiria/hakuwahi kudhani kiko ndani ya uwezo wake kama kuua.
Kumdharau mtu yeyote yule ambae bila yeye usingekua hapo ulipo.Mzazi/ndugu/rafiki/jirani/mwalimu n.k
Dah ntaendelea baadae.....