Kitu kisicho cha kawaida chapatikana katika pwani ya bahari ya Japan

Kitu kisicho cha kawaida chapatikana katika pwani ya bahari ya Japan

HERY HERNHO

Senior Member
Joined
Mar 4, 2022
Posts
110
Reaction score
458
Kugunduliwa kwa chuma kikubwa cha mviringo kinachofanana na mpira wa miguu katika mji wa pwani ya Japan wa Hamamatsu, takriban kilomita 200 kusini magharibi mwa Tokyo, kumezua wimbi kubwa la uvumi.

Mamlaka za mitaa, polisi na kikosi cha mabomu walitumwa kwenye ufukwe wa Enshuhama kuchunguza kitu hicho kisichojulikana.

Wamegundua tu kwamba chuma hicho cha mvirongo hakina lolote ndani yake na hakina tishio lolote, huku wengine wakishuku kuwa inaweza kuwa aina ya boya.

Wenyeji waliovutiwa tayari wamekuja na majina machache ya kuupatia mpira huo kama vile "yai la Godzilla" , "mooring buoy" na kitu cha "anga ya nje".

Ugunduzi kama huo mara chache huibua mashaka katika nyakati za kawaida, lakini umekuja wakati ambapo kuna wasiwasi juu ya vitu visivyojulikana kufuatia kudunguliwa kwa puto linaloshukiwa kuwa la kijasusi la China na Marekani mapema mwezi huu.

Jumatano iliyopita, Japan iliiarifu China kuhusu kutoridhika kwake kutokana na tuhuma za kugundua puto za uchunguzi kwenye anga yake angalau mara tatu tangu 2019.

b8c75760-b32f-11ed-89f4-f3657d2bfa3b.jpg
 
Hicho kitu hakina umaajabu ni waandishi wanakuza habari. Hiyo ni buoy, probably kutoka vita ya pili ya dunia. Kwa ukubwa wake itakuwa ni zile zilitumika na US Navy kufunga submarine nets kwenye Pacific theatre.
Hilo simply ni boya la kijeshi. Sio naval mine, kama ingekuwa mine sappers wangeshakuja kazini
 
Inawezekana kuwa ni bomu.maana kipindi cha vita vya pili mabomu mengi yalipotea sehemu nyingi kuanzia kwenye mito,ardhi,maziwa na bahari.
Meli nyingi zilizama na silaha.
Ila serikali inapoona jambo kama ili iwezi kutoa majibu haraka kama sisi wana JF tunavojua kuhukumu haraka.
View attachment 2527270
Screenshot_20230223-114911_Gallery.jpg
 
Back
Top Bottom