DOKEZO Kituo cha Afya Mji Tunduma "Serikalini" kinatoza fedha kumuona Daktari, vipimo na dawa kwa Watoto chini ya Miaka mitano

DOKEZO Kituo cha Afya Mji Tunduma "Serikalini" kinatoza fedha kumuona Daktari, vipimo na dawa kwa Watoto chini ya Miaka mitano

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Screen Shot 2025-02-05 at 12.09.34.png

Screen Shot 2025-02-05 at 12.10.19.png
Nimehudumiwa mara mbili katika Kituo cha Afya Halmashauri ya Mji Tunduma maarufu kwa jina "Serikalini" Kata ya Majengo ambapo walilazimisha nitoe gharama za kumuona daktari licha ya kuwa mgonjwa alikuwa ni mtoto mdogo wa miezi 9 tu.

Nililazimika pia kugharamikia vipimo pamoja na dawa ambazo walidai hazipo pale lakini kwa wenye pesa walipewa dawa hizo hizo ambazo mimi niliambiwa hazipo.

Naomba Serikali iingilie kati suala hili kwani ni tofauti na ahadi tunazopewa na Serikali kuwa mama Mjamzito na Watoto watapewa huduma bure katika vituo vyote vya afya.
 
Back
Top Bottom