Kiuno hana kisa chipsi kuku ya mapenzi

Kiuno hana kisa chipsi kuku ya mapenzi

Laswell

Senior Member
Joined
Feb 23, 2024
Posts
144
Reaction score
191
Salaam alaikum,
Kijana wa chuo,kijana wa kiume ambaye familia yake ilitegemea apate elimu Kisha kupitia elimu hiyo ukombozi wa kiuchumi upatikane kwa wanaomtegemea,ameamua ajirushe gorofani kisa chipsi alizomnunulia mpenzi wake.

Iko hivi, jamaa ana mpenzi wake chuoni na kwa alivyokuwa anaona yeye nikwamba alikuwa anapendwa,ama tuseme walikuwa wanapendana. Siku ya tukio mdada yupo chumbani(wote wanaishi hostel),akampigia jamaa kwamba anaumwa na chakula anachojisikia kula ni chipsi kuku na Azam embe ya baridi.

Kijana katika Hali ya kujali akavinunua hivyo vitu akapeleka chumbani kwa mdada na kumkabidhi huku akimsisitiza mpenzi wake ale ili arejee kwenye Hali yake ya kawaida. Mdada akadai hajisikii kula kwa muda ule hivyo jamaa amuache tu atakula badae kidogo. Baada ya stori mbili tatu kijana akaondoka kwa kuwa tayari ilikuwa ni usiku.

Aiyaaa! kufika katikati ya safari akagundua kasahau ufunguo wake pale alipokuwa hivyo ikabidi arudi. Wakati yupo nje ya chumba akasikia mdada anacheka na anaaongea kwa bashasha kama vile sio yeye aliyekuwa mgonjwa. Kijana akiwa anaamini kuwa chipsi zimeleta uponyaji wa gafla kwa mpenzi wake akaamua kuingia bila hata kugonga mlango ili aungane na mwenzake kwenye hiyo furaha then achukue funguo zake aondoke.

Kuingia anakutana na njemba imekalia zile chipsi huku wakilishana na yule mdada kwa raha zao. Kilichofuata jamaa aliyeleta chipsi alitoka akaaenda gorofa ya 3 ya jengo lile akajitupa chini. Uzuri hakufa ila kiuno na mgongo havileti matumaini kwamba Kuna siku atatembea tena. Yupo hospitali na kwa kiasi kikubwa wazazi wake ndo wanabeba garama za matibabu kwani Ile bima imeshindwa kugharamia kila kitu.

Tuwaambieje hawa vijana kuhusu mapenzi?
 
Biblia inasema ni mzigo kwa mamaye.. sijui suleimani alimaanisha nini? Kuwa mama hawezi tupa mtoto wake?
 
Da! Mambo haya ni magumu sana duniani hapa Pesa, maradhi, mapenzi hivi vitu hatari sana
 
Daah dogo angebeba chips zake au hata angevunja tu uhusiano. Usijidhuru kisa mapenzi. Kumamamamake ugali mtamu sana aisee. Killing myself for bitch nop
 
stori ya mwaka juzi iyo kama sio mwaka jana mjini UDOM, uko outdated sana
 
Ndiyo kataa ndoa wa kesho huyo kama siyo wa leo.
 
MAPENZI yametumika tu kama kisingizio, hapo ni laana za ukoo na roho chafu zinamuandama.

hamuwezi kunielewa, ipo hv kila mzaliwa katika familia anayeonekana kuwa ni lango la baraka katika familia yao lazima akumbane na vizingiti kama hv, inawezekana hata familia aliyotoka imezingirwa na roho chafu ya umauti lakn watu hawajui.

shetani ameamua kuzima ndoto na baraka za familia kwa njia ya majini ya mapenzi.

VIJANA WETU WA KITANZANIA WANAPITA KATIKA MSONGO MKUBWA WA MAWAZO, TUWAOMBEE KILA MTU KWA IMANI YAKE.

TANZANIA NA WATU WAKE NI TAIFA TEULE LAKINI LIMEFUNIKWA NA GIZA TOTORO LA SHETANI, KUANZIA WAKUBWA HADI CHINI HAKUNA ANAYE ONA MBELE. TULIOMBEE TAIFA KILA MTU KWA IMANI YAKE.
 
Ningekua mimi... ningebeba hio azam embe ningeondoka nayo aisee askuambie mtu ile juisi tamu balaa.
 
Umeweka kifungu cha maneno utupe kazi ya kuchambua eti? Nawewe ni msomi wa elimu ya juu ulioandika fungu hili
 
Sema mkuu nimependa ulivyosimulia hasa pale uliposema "akaamua kuingia bila hata kugonga mlango ili aungane na mwenzake kwenye hiyo furaha then achukue funguo zake aondoke"🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom