KERO Kivuko cha Busisi - Kigongo chenji ikibaki sh. 100 hurudishiwi kwa kisingizio hakuna chenji

KERO Kivuko cha Busisi - Kigongo chenji ikibaki sh. 100 hurudishiwi kwa kisingizio hakuna chenji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Busisi.jpeg

Ukifika kivuko Cha Busisi mkoani Mwanza unakuta tangazo kuwa kuna changamoto ya chenji ya Sh mia, ukichungulia mezani kuna silver za mia Tano na mia mbili, nauli ya kuvuka ni TSH 400 kwa mtu mzima lakini ukitoka sh 500 unapewa risiti yenye thamani ya 400 inayobaki hupewi.

Je, huwa wanazipeleka wapi hela zinazozidi?, ukiangalia wanaovuka kwa siku ni wengi sana na sio wote wanakuja na sh. 400 kamili, kama kuna changamoto ya chenji kwanini wasitengeneze tu risiti za TSH 500 kuliko hizo sh 100 zinazobaki na hazina maelezo zimepatikana vipi maana pesa yenye maelezo ni ile iliyokatiwa risiti

Naishauri serikali kufatilia hili jambo ili wananchi wasizid kupoteza chenji zao.
 
Kukaa unalalamika kuhusu shilingi 100 ambayo hainunui hata chumvi ni dalili nyingine za kukaribisha umaskini kichwani. Umeshasoma tangazo njoo na 400 kamili. Au njoo na 500 upigwe 100. Inaonekana unamaindi 100 kubaki na kwenda kwa mtu mwingine. Unatamani ijulikane ni 500 ili iende ikapigwe na serikali. Si bora ibaki kwa huyo unayemuona naye afaidi matunda ya serikali!?,au ndo roho ya kwanini!?..,
 
Kukaa unalalamika kuhusu shilingi 100 ambayo hainunui hata chumvi ni dalili nyingine za kukaribisha umaskini kichwani. Umeshasoma tangazo njoo na 400 kamili. Au njoo na 500 upigwe 100. Inaonekana unamaindi 100 kubaki na kwenda kwa mtu mwingine. Unatamani ijulikane ni 500 ili iende ikapigwe na serikali. Si bora ibaki kwa huyo unayemuona naye afaidi matunda ya serikali!?,au ndo roho ya kwanini!?..,
Ni kweli kaka acha jamaa ale Kwa urefu wa kamba yake.

Kihesabu jamaa akikeep chenchi ya watu 5000 wanaovuka hapo Kwa kila siku ataweza kutengeneza 500,000/= Kwa siku ambayo Kwa mwezi ni 15,000,0000/= Kwa hiyo hiyo mia.

Ni Bora ale yeye bhana kuliko ifike huko juu itumbuliwe
 
Upigaji sasa uko kwenye kila kona ya hii nchi
Urefu wa kamba kwa majibu wa mkulu
 
Back
Top Bottom