Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,306
Kiwanda cha Bodaboda
Ikiwa kichwa cha habari kimekufanya uwaze mitambo ya kutengeneza pikipiki, karibu kwenye mada.
Mada hii si kuhusu mitambo ya kutengeza pikipiki (factory). Mada hii inahusu watoa huduma za usafiri wa bodaboda. Mafundi wa pikipiki za bodaboda. Watumia huduma za bodaboda. Na kiasi cha pesa kinachozunguka kila siku kutokana na bodaboda. Yaani, Kiwanda cha Bodaboda (Bodaboda Industry).
Fikiria iwapo leo hii serikali itapiga marufuku bodaboda. Kiwanda cha Bodaboda kitakwisha mara moja. Je, ni watu wangapi wataathirika kwa kukosa ajira na kukosa huduma? Je, tutaweza kumudu gharama za kukifunga kiwanda hicho? Bila shaka jibu ni hapana.
Mafanikio makubwa ya Tanzania ya Viwanda yameripotiwa kuhusiana na Viwanda ambavyo ni Factories. Hii imepelekea baadhi ya watu kudhani Viwanda ni vile tu vya mitambo. Pengine ni wakati muafaka wa kupembejea viwanda (industries) vya huduma kama sehemu ya mkakati wa Tanzania ya viwanda. Bodaboda ni mfano tu. Vibanda vya huduma ya pesa kwenye simu (M-Pesa/Tigopesa/Airtel-Money/Halopesa/T-Pesa...) nayo ni mfano wa kiwanda. Watu wangapi wameajiriwa na kiwanda hicho? Wangapi ni wanufaika? Ujazo wa mzunguko wa pesa ni kiasi gani? Serikali ikiamua kukifunga kiwanda hicho, wangapi wataathirika? Je, tutaweza kumudu gharama za kukifunga kiwanda hicho? Bila shaka jibu ni hapana.
Viwanda-huduma (service industries) zilizoko ziimarishwe, na nyingine mpya zihamasishwe kuanzishwa ili kuboresha utekelezaji wa sera ya viwanda, kama nyongeza ya mwelekeo wa kwenye viwanda-mitambo (factories).
Ikiwa kichwa cha habari kimekufanya uwaze mitambo ya kutengeneza pikipiki, karibu kwenye mada.
Mada hii si kuhusu mitambo ya kutengeza pikipiki (factory). Mada hii inahusu watoa huduma za usafiri wa bodaboda. Mafundi wa pikipiki za bodaboda. Watumia huduma za bodaboda. Na kiasi cha pesa kinachozunguka kila siku kutokana na bodaboda. Yaani, Kiwanda cha Bodaboda (Bodaboda Industry).
Fikiria iwapo leo hii serikali itapiga marufuku bodaboda. Kiwanda cha Bodaboda kitakwisha mara moja. Je, ni watu wangapi wataathirika kwa kukosa ajira na kukosa huduma? Je, tutaweza kumudu gharama za kukifunga kiwanda hicho? Bila shaka jibu ni hapana.
Mafanikio makubwa ya Tanzania ya Viwanda yameripotiwa kuhusiana na Viwanda ambavyo ni Factories. Hii imepelekea baadhi ya watu kudhani Viwanda ni vile tu vya mitambo. Pengine ni wakati muafaka wa kupembejea viwanda (industries) vya huduma kama sehemu ya mkakati wa Tanzania ya viwanda. Bodaboda ni mfano tu. Vibanda vya huduma ya pesa kwenye simu (M-Pesa/Tigopesa/Airtel-Money/Halopesa/T-Pesa...) nayo ni mfano wa kiwanda. Watu wangapi wameajiriwa na kiwanda hicho? Wangapi ni wanufaika? Ujazo wa mzunguko wa pesa ni kiasi gani? Serikali ikiamua kukifunga kiwanda hicho, wangapi wataathirika? Je, tutaweza kumudu gharama za kukifunga kiwanda hicho? Bila shaka jibu ni hapana.
Viwanda-huduma (service industries) zilizoko ziimarishwe, na nyingine mpya zihamasishwe kuanzishwa ili kuboresha utekelezaji wa sera ya viwanda, kama nyongeza ya mwelekeo wa kwenye viwanda-mitambo (factories).