Kiwanda cha mbu: Njia ya kisasa kupambana na mbu wanaoleta maradhi kwa binadamu

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363



Katika mji wa Guangzhou nchini China, kuna kiwanda kikubwa zaidi cha mbu duniani, ambacho kinazalisha mbu wa kiume zaidi ya laki 5 hadi milioni 1 kila wiki.

Mbu wote wanaozalishwa katika kiwanda hicho wanabeba kimeleo cha Wolbachia. Mbu wa kiume wa aina hiyo wakijamiiana na mbu wa kike, mbu wa kike hawataweza kuzaa tena.

Mwaka 2001, Xi Zhiyong alianza kutafiti kimeleo cha Wolbachia, na ni mtu wa kwanza kuweka kimeleo hicho katika mbu wenye virusi vya dengue na malaria.

Xi Zhiyong na timu yake hawataki kuangamiza mbu wote, na wanatakia kubadilisha mbu wanaoweza kuambukiza virusi kuwa mbu wa kawaida.
Kiwanda cha Mbu pia kinaungwa mkono na tajiri mkubwa dunia Bill Gates, ambaye alichangia dola milioni 15 za kimarekani.

Chanzo: CRI Kiswahili
 
Tanzania pale mkoani Pwani nafikiri kuna kiwanda pia kinachozalisha mbu kwa dhamira kama hii... Mwenye updates anaweza kitupatia pia.
 
waache.ujinga wasije kutuletea mgonjwa ya ajabu ajabu
 
Hata Tanga kuna kiwanda wanazalisha ndorobo for the same purpose
 
NASKIA KILIKUWEPO DSM SIJUI MUHIMBILI.KUNA SIKU WALIFUNGULIWA WAKAJAA HADI DIT
 
Hapo lazma wana plan B ya kupiga hela, hawawezi zuia malaria kirahisi hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…