KKKT : Maaskofu hatujagawanyika kuhusu Katiba

Greenwhich

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
1,337
Reaction score
968
Askofu Benson Bagonza wa KKKT Dayosisi ya Karagwe amepinga vikali kauli ya serikali kwamba maaskofu wamegawanyika kuhusu Kura ya Hapana kwenye Katiba Mpya.

Askofu Bagonza ambaye ni mjumbe wa CCT ameonya kauli ya Samwel Sitta kwamba Serikali haitarudi nyuma kuhusu katiba mpya.

Askofu Bagonza ambaye ana msimamo thabiti amesema wapo maaskofu wa mfukoni wanaoandaliwa na Serikali ambao wanatumika kujibu hoja mbalimbali za kanisa.

Akizungumzia Kauli ya Kadinali Pengo kupingana na maaskofu wenzake, Askofu Bagonza amesema huo ni msimamo binafsi wa Kadinali Pengo na siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesema msimamo wa Kanisa Katoliki nchini unatolewa na TEC ambalo ni Baraza la Maaskofu Katoliki nchini.

Askofu Bagonza amesisitiza kwamba pamoja na msimamo binafsi wa Kadinali Pengo lakini ameruhusu Tamko la Maaskofu kusomwa katika Makanisa yote ya Jimbo lake la DSM.

Askofu Bagonza ameishangaa serikali kusema Kanisa halina haki ya kuwataka waumini kupiga kura ya Hapana.

Askofu Bagonza amesema.." Kama CCM na serikali yake wanawashawishi watu wapige kura ya Ndiyo, Ukawa wamewaeleza watu wao wasusie,iweje iwe tatizo kwa Jukwaa la Wakristo kuwaeleza wafuasi wao wapige kura ya Hapana?"...alihoji.
======================


Chanzo:
Mwananchi
 
Asante sana Askofu Wangu.....

Naomba askofu Wangu wa Dayosisi Ya Kaskazini na Wewe uuunge mkono Kura ya HAPANA.....hii katiba sio chaguo la wananchi.....

Huyu Askofu ni Nabii wa ukweli kama alivyo Severine Niwemugizi
 
Kardinali Pengo alisema hivi;

Hawana nguvu za kumjibu Kardinali Pengo na wanachofanya ni kuzunguka mbuyu na kutafuta easy target!
 
Kardinali Pengo alisema hivi;
Wanazunguka mbuyu!

Umeambiwa mambo mawili
(a) Cardinal Pengo siyo msemaji wa TEC
(b) Kwa kuwa amepata amri toka juu kwenye baraza naye kwenye jimbo lake ameamuru Waraka ule wa KICHUNGAJI usomwe jinsi ulivyo.

YATOSHA MAOVU YAKE KWA SIKU - PIGA HAPANA katiba iliyoandikwa na Nyoka wa makengeza
 
aaah!!!aaaah!! ama kweli wanadhani hii ni karne ya NYEUPE ni NYEUSI..msimamo mmoja rasimu ya makengeza ina matatizo!!!
 
kardinali pengo alisema hivi;

hawana nguvu za kumjibu kardinali pengo na wanachofanya ni kuzunguka mbuyu na kutafuta easy target!

kwa taarifa yako cardinal pengo yuko chini ya rais wa tec angezuia usisomwe jimbo kuu la dsm,mbona ulisomwa huyo ni bosi wa mkombozi bank analipa fadhira,lakini sisi wakatoliki msimamo baraza la maaskofu ndio msimamo wa kanisa katoliki tanzania.
 

Hakika yatosha Maovu yake kwa Siku.....Piga Kura ya HAPANA
 
Kardinali Pengo alisema hivi;

Hawana nguvu za kumjibu Kardinali Pengo na wanachofanya ni kuzunguka mbuyu na kutafuta easy target!

MwanaDiwani,

Baraza la Maaskofu ni taasisi yenye nguvu.Waraka uneshasambazwa na Pengo hana uwezo wa kuzuia
 
Last edited by a moderator:
hongera baba askofu kwa kuwakilisha sauti ya kkt
 
Kazi kweli kweli kwani haraka ya nni na haraka hiyo kwafaida ya nani?
Mbona watz mna papara hivyo? Hiyo kura yenyewe haiwezekani kupigwa hiyo tarehe 30/04/2015. Kama imechua takriban mwezi mmoja kuandisha watu ktka daftari la wapiga kura katika mkoa mmoja,

je mikoa iliobaki itachukua muda gani kwa utaratibu huu? Jiulize.! kwa hiyo kimsingi kama utaratibu wa kuandikisha wananchi kwenye daftari la wapiga kura utaendelea kufanyika kwa staili ya sasa , basi tusahau kupiga kura 30/04/2015 labda wapange tarehe nyingine!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…