Klabu Bingwa Afrika: Dar Young African Vs Zesco

Nimefurahi kusikia hivyo maana hapa nilishatayarisha dawa ya maumivu kama yangeendelea na leo ingebidi uje unywe tu mamii
Iweke tu Ses huenda mechi ya marudiano nikaitumia japo sitarajii kwani najua inawezekana tukawapindulia meza vile vile. 😎😎😎
 
Hatujakataa mbona. Na sisi tutawachezea mwingi huko Zambia. 😎😎
Na huko kwao mna ubavu wa kufunga goli la move? Maana haiwezakani mpewe penati ya bure kwenye nchi ya watu

Kwanza goli la move ni tamu sana ujue Shadeeya. Kuna mwana bongofleva mmoja wa zamani sijui Chege Chigunda yule alikua na wimbo wake akiimba 'Raha ya mechi bao tena bao tamu lile la patashika" ndio kama lile la Zesco sasa.

Sio nyie mnatafuta huruma ya refa hadi akawaponza maana aliweka amadakika kibao ya nyongeza akidhani mtaongeza goli la pili, pole love
 
Iweke tu Ses huenda mechi ya marudiano nikaitumia japo sitarajii kwani najua inawezekana tukawapindulia meza vile vile. 😎😎😎
Hahahaaa uzuri wa Yanga ni hapo tu, mna roho saba nyie, yaani mnaona mnaenda kufa hivihivii lakini bado mnajipa moyo tu
 
Na huko kwao mna ubavu wa kufunga goli la move? Maana haiwezakani mpewe penati ya bure kwenye nchi ya watu
Kwani kule kwa Townshipp Rollers tulipewa Penalti?
Kwanza goli la move ni tamu sana ujue Shadeeya. Kuna mwana bongofleva mmoja wa zamani sijui Chege Chigunda yule alikua na wimbo wake akiimba 'Raha ya mechi bao tena bao tamu lile la patashika" ndio kama lile la Zesco sasa.
Kwa hili nionavyo tunywe Mtori nyama tutazikuta chini kwani bahati ya kuzilenga nyavu tu ndio hatuna lakini hizo move tunazitengeneza sana tu.
Sio nyie mnatafuta huruma ya refa hadi akawaponza maana aliweka madakika kibao ya nyongeza akidhani mtaongeza goli la pili, pole love
Haya ni mawazo yenu tu love na wala hatuchezi mpira tukiyatarajia hayo. Na pia niseme ile ni sehemu ya mpira hivyo yote tumeyapokea na kujipanga kwa 90 mins za kule Zambia ambazo nina hakika tutazitumia vyema. 😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…