beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
ULAYA: Klabu ya soka ya Liverpool ya Uingereza imeinyuka klabu ya Manchester City ya Uingereza goli 3-0 katika Michuano ya Klabu Bingwa Ulaya
Katika mchezo huo uliofanyia katika uwanja wa nyumbani wa Liverpool(Anfield), magoli ya Liverpool yamefungwa na M. Salah(12'), A. Chamberlain(21') na S. Mane(31')
Wakati huo huo Klabu ya Barcelona ya Uhispania imeibuka na ushindi mnono wa goli 4-1 dhidi ya klabu ya AS Roma ya Italia
Barcelona ikiwa nyumbani(Camp Nou) ilipata magoli yake kupitia kwa D. De Rossi(OG 38'), K. Manolas(OG 55'), G. Pique(59') na L. Suarez(87'). Goli la Roma la kufutia machozi lilifungwa na E. Dzeko(80')
Mechi hizi zote ni mzunguko wa kwanza(first leg) na watarudiana tena Aprili 10, 2018