Klabu ya Simba SC yamteua Method Mwanjale kuwa Nahodha mpya akichukua nafasi ya Jonas Mkude

Yaani kupigwa wiki ndiyo sababu ya kumtoa Mkude!

Sent using Jamii Forums mobile app
Wachoma jezi FC bhana.. Yaani kwa uongo mmekubuhu, kwahivyo Runinga iliyowekwa pale bwawani Full Time ndo ilionyesha matokeo hayo?

Tano zinakuhusu kwa mara nyingine tena, maana safari hii Rais wenu wa pale Tifuatifua hayupo..!
 
Hawezi kujisikia vibaya Mkude?
Kama akili yake ilikuwa kwenye unahodha tu na akajisahau kuwa kazi ni kucheza soka ili kuiletea mafanikio klabu na yeye kutaraji kwenda hata nje ya nchi kucheza soka, yamkini atakuwa hivyo. Lakini kama mwerevu basi eandelee kukuza kiwango chake, kwanza klabu imempa heshima na kumshukuru kwa kipindi chake cha uongozi kwa wachezaji wenzake uwanjani na nje ya uwanja.
 
Mkude kimemponza baada ya kuvujisha habari kuwa simba imepigwa bao saba
 
Hawezi kujisikia vibaya Mkude?

Kwani Yeye anapolewa Mipombe yake na kufanya Umalaya wake huku akiwa Kambini na Timu mara kwa mara ( japo alishaonywa mara kibao tu ) bila kusahau akiuendekeza Uyanga wake na akitumika na hao hao Yanga ' kuihujumu ' Simba SC Sisi wana Simba SC huwa hatujisikii vibaya?
 
Kwahivyo Mkude ndo mwenye televisheni ilionyesha habari hiyo mpaka mkaangalia nyinyi tu Gongowazi, ambapo watu wengine hawakuona eeh..!
TV gani ilionyesha hiyo mechi ?
Mbona mlimtuma msemaji wenu Manara akanushe kuwa hamjafungwa wiki
 
Mkude kimemponza baada ya kuvujisha habari kuwa simba imepigwa bao saba

Hapa ndipo huwa ninawadharau baadhi ya Watanzania hasa kwakuwa uwezo wao wa ' Ufahamu ' ni mdogo sana. Hivi katika dunia ya leo ambayo teknolojia imefanya tuwe kama Kijiji kimoja Klabu kubwa kama ya Simba inaweza kuwa na mchezo wa Kirafiki tena nchini Afrika ya Kusini halafu hiyo mechi ama isiwe televised au covered na Media zingine mbalimbali za huko huko Afrika ya Kusini? Hivi ni kwanini tunakuwa ' Wapumbavu ' hivi kila uchao?

Wanasema kuwa Simba SC ilicheza mechi hiyo na Timu ya Daraja la Kwanza iitwayo Royal Eagles FC ambapo hata ukiingia tu katika Website yao utakuta hakuna taarifa yoyote kwamba walicheza na Simba SC isipokuwa kuna Fixtures tu zingine za mechi zake za Kirafiki na Usajili.

Kinachoniudhi ni kwamba Watu tuna access ya Mitandao lakini tunashindwa hata tu ' Kujiongeza ' Sisi wenyewe kuweza kutafuta ukweli wa hii kitu na tunabaki tu kuleta ' Upumbavu ' wetu humu wa Ushabiki wetu wa ' hovyo hovyo ' wa Simba na Yanga ambao ndiyo umechangia hadi leo hii tunapiga tu ' mark time ' katika Maendeleo ya Soka huku Wenzetu walio serious wanatuacha.

Tusikimbilie tu kutaka mabadiliko TFF bali hata Sisi ' Mashabiki ' pia tubadilike hasa Kifikra, Kiueledi na Kimtizamo la sivyo kila uchao tutabaki tu kumsifia Mbwana Samatta wakati majirani zetu tu hapa wana akina Samatta wao wengi tu huko Ulaya hali ambayo hupelekea Sisi tunapocheza nao wao kuleta Wachezaji wao Vijana kabisa ila Sisi kama kawaida ya ' Umbumbumbu ' wetu tunaweka ' full mkoko ' na bado tunafungwa vile vile.

Kwa kukusaidia tu na ' Wapuuzi ' wenzio ni kwamba japo Uongozi umeamua kulifunika kwa maslahi mapana ya Klabu na kuimarisha Umoja ndani ya Timu sababu Kuu zilizofanya Mkude ' kupokwa ' Kitambaa cha Unahodha ni hizi zifuatazo:

  1. Ulevi
  2. Umalaya ( R.I.P sana yule Dada aliyefariki kwa Ajali ya Gari wakitokea Dodoma kuangalia Fainali ya ASFC )
  3. Kupenda starehe hasa Muziki kupitiliza hapa najua ' Masela ' wa Kipande cha Kinondoni Biafra hadi Mango Garden najua mtakuwa mnanielewa ambako pia ndiko Mkude amekulia na kucheza sana Soka
  4. Uyanga wake uliopitiliza
  5. Usaliti kwani hakuna ambaye hajui kwamba Mkude ' katuumiza ' mno katika VPL iliyoisha kwa gharama za Yanga
  6. Kugawa Wachezaji wenzie ( Kuendekeza Ufaza ) na kuwatenga wengine kwa kuwaona ni ' Washamba '
  7. Dharau kwa baadhi ya Watu wa Benchi la Ufundi hasa kwa Kocha Msaidizi Jackson Mayanja a.k.a Mia Mia
Kazi Kwako!
 
Pole sana mpaka povu limekutoka, hujui unasubiri kuona game kwenye tv, pole, hata clouds leo wameiongelea hiyo issue, watangazaji wote wa sports extra ni washabiki na wanachama wa Simba hasa shaffih dauda, na wana access ya kujua kinachoendelea huko maana wanapigiana simu na wachezaji, wameongea leo kuwa huenda ndiyo sababu ya kuponywa ukapteni wa timu baada ya kuvujisha habari za kula bao saba.
 
TV gani ilionyesha hiyo mechi ?
Mbona mlimtuma msemaji wenu Manara akanushe kuwa hamjafungwa wiki
GENTAMYCINE post #30 Amemaliza kila kitu hapo, rejea kuisoma ili uondoe Uzwazwa hapo bwawani
 
GENTAMYCINE post #30 Amemaliza kila kitu hapo, rejea kuisoma ili uondoe Uzwazwa hapo bwawani
Huyo ambaye alisema FIFA wameleta barua Simba mpewe ubingwa bado unamwamini ?

Ndio maana Rage aliwaita mbumbumbu
 

Hopeless mkubwa! Nani aliyekuambia kuwa Shaffih Dauda ni ' Mshabiki ' wa Simba SC? Ngoja niendelee ' kukudharau ' tu. Wakati Wewe ukisema kuwa hao Watangazaji wako uliowataja hapo wana ' access ' na Wachezaji Mimi pia moja kwa moja nina ' access ' na Wachezaji Watatu tena ' Waandamizi ' kabisa wa Simba SC ila kwa kutowasababishia ' matatizo ' na Uongozi wa Klabu sitowataja hapa.

Na nimalizie tu kwa kukuhakikishia na kukuthibitishia tena kwa ' Kujigamba ' kabisa kuwa Simba SC haijacheza mechi yoyote na haijafungwa goli Saba ( 7 ) huko ' Bondeni ' ila wanajiandaa sasa kwa mechi zao mbili za Kirafiki na Orlando Pirates na Bidvest hivyo kama mnangoje muone ' tukifungwa ' hizo goli zenu ' wiki ' basi suburini tufungwe na hizi Timu mbili. Hivi hiyo mechi aliyekuwa anajua tumecheza ni Mkude tu peke yake? Hivi hao Wachezaji wengine wa Simba SC hawana ' access ' na Watu wao huku Tanzania? Hivi Simba SC icheze mechi halafu hiyo mechi ama isifuatiliwe na Watazamaji au na Waandishi wa Habari mbalimbali wa huko Afrika ya Kusini?

Namshukuru sana Mwenyezi Mungu hakunibariki na ' Upumbavu ' ulionao Wewe na wenzako wote mnaong'ang'ania kuwa Simba SC ilifungwa goli Saba ( 7 ) halafu hamna hata ' ushahidi ' wowote ule wa kuyathibitisha hayo muyasemayo. Nilichokigundua tu ni kwamba yawezekana wana Yanga FC ' wanaziota ' mapema goli Saba ( 7 ) ambazo huenda ' wakafungwa ' na Simba SC ( Mnyama ) hapo tarehe 23, August 2017 ndani ya Uwanja wa Taifa hivyo siwalaumu sana.
 
Huyo ambaye alisema FIFA wameleta barua Simba mpewe ubingwa bado unamwamini ?

Ndio maana Rage aliwaita mbumbumbu
Hakuna chochote hapo kwenye kuthibitisha hilo labda Runinga Gongowazi ndo ilionyesha mechi hiyo. Post #30 rejea inakuhusu vilivyo kabisa

Hivi unajua Katibu Mkuu wa Cecafa Nicolas Musonye alisema nini kuhusu Yanga? Yamkini hakukosea kusema vile!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…