Kocha aliyepewa "THANK YOU" Azam FC, Youssouph Dabo aibukia AS Vita Club ya DRC

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Youssouph Dabo ametangazwa rasmi kuwa kocha mpya wa AS Vita Club, klabu maarufu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC). Dabo anachukua nafasi hii baada ya kuachishwa kazi na Azam FC, ambapo aliifundisha timu hiyo.

Uteuzi wa Dabo unakuja wakati ambapo AS Vita Club inahitaji kuimarisha mipango yake ya ushindani, hasa katika mashindano ya ndani.


Pia, Soma:

RASMI: Kocha wa Azam FC, Youssouph Dabo avunjiwa mkataba
Azam FC na Dabo habari imeisha. He will be fired upon arriving in Tanzania
 
Kama alishindwa pale Azam na facilities zote zile uko sioni akifanya chochote.
 
Namtakia kila la kheri... Dabo ni kocha mzuri sana Kwanza alifanya Azam kucheza soka zuri la kuvutia na kuisadia timu kushika nafasi pili mbele ya simba..

Naamini kutokana na fan base ya Vita Club atafanya poa sana
 
Namtakia kila la kheri... Dabo ni kocha mzuri sana Kwanza alifanya Azam kucheza soka zuri la kuvutia na kuisadia timu kushika nafasi pili mbele ya simba..

Naamini kutokana na fan base ya Vita Club atafanya poa sana
Azam inaonekana pana shida nyingi sana. Team ina kila inachohitaji lakini ipoipo tu kama timu ya shule za kishua.
 
 
Fei toto asirudie tena kumwangalia hivyo mwanamume yoyote yule.
 
VITA CLUB
Ishakuwa timu ndo DRC
Kwa Sasa timu kubwa CONGO ni FC LuPopo, FC maniema na TP mazembe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…