Kocha Fadlu Davids amevunja rekodi za makocha wote waliowahi kufundisha Simba tangu mwaka 2007

Kocha Fadlu Davids amevunja rekodi za makocha wote waliowahi kufundisha Simba tangu mwaka 2007

19792magufuli

New Member
Joined
Feb 21, 2023
Posts
1
Reaction score
5
Kocha huyu ingawa kwangu ananipa mashaka sana kutokana na sub zake lakini haiondoi ukweli kuwa amevunja rekodi ambazo hazijawahi kuwekwa na kocha yeyote aliyewahi kufundisha Simba.

Fahdu ameweka rekodi kubwa tatu ambazo mtu yeyote wa mpira anipinge kwa takwimu na sio porojo.

1. Fact ya kwanza kwa kocha huyu ni kupata goli katika mechi zote za ugenini, kumbuka Simba ilikuwa inashinda sana home na ikienda ugenini kupata goli ni mtihani, huyu mtu kusema kweli amejitahidi maana mechi zote za ugenini Simba imepata bao.Kule kwa Constantine Tshabalala alifunga, kule Tunisia Jeans Charles Ahoua akaweka kambani na jana kule Angola Leonel Ateba Mbida.

2.Rekodi ya pili kwa kocha huyu ambayo haijawahi kufikiwa na kocha yoyote aliyewahi kufundisha Simba ni kufuzu hatua ya robo fainali ugenini tena tukiwa na mchezo mmoja mbele.Kwa kweli makocha wengi waliowahi kufundisha Simba hili liliwashinda, tulikuwa tunaenda kucheza lakini mwishoni fainali ni uwanja wa Mkapa, tukaanzisha Kwa Mkapa hatoki mtu, Do or Die.

3. Rekodi ya tatu kwa kocha huyu ni kwa Simba kucheza soka inayoeleweka.Kiukweli japokuwa tuna shida sehemu ndogo ndogo sana lakini ukweli kuwa kiwango cha timu yetu ni kizuri sana, mpira unaanzia kwa Pin Pin Camara, anamrushia Kapombe anarudisha kwa Camara, anapeleka kwa Kagoma anaivusha kwa Mpanzu, anamlamba chenga mzembe mmoja wa Bravos anaivusha kwa Kibu, inaletwa kwa Mavambo inapelekwa kwa Kapombe anaitupia kwa Ateba anauweka wavuni.

Rekodi hizo ni unprecedented kwa kweli.
 
Huko luser cup ( kombe la wamama) hata kama Kalpana angekuwa kocha ....angetoboa robo fainali

Kimbembe ni huku club bingwa...Kwa wanaume
 
kucheza soka inayoeleweka.Kiukweli japokuwa tuna shida sehemu ndogo ndogo sana
Sasa unaharibu haiwezekani timu ikawa inacheza mpira mzuri alafu nado kuwe na shida ndogondogo..maana yk kiwango bado.
 
Ila chemaloan aka ukuta wa Yeriko unachoma sana mahindi. Utafikiri katumwa kuharibu clean sheet ya 📍 📌 Camara.
 
Sijaumia kaka utopolo..nimekujibu niliona kama wamekususa nikasema ngoja nikujibu jamani..
Sema dada una moyo mgumu wewe.

Wewe hata kulala na chatu chumba Kimoja unaweza.

Mdada mrembo unaanzaje kuishabikia nyau fc.
 
Fadlu unashindwa kulaumu maana takwimu zinambeba,nadhani ni kocha wa mbinu zaidi au anakesha kusoma video za wapinzani na kubaini mapungufu. Maana Simba inapocheza sasa hivi siyo mbaya na huwezi kusema inatisha sana ikiwa uwanjani kuna mazingira unaona goli litafungwa tu hata kama itachelewa.
 
Sema dada una moyo mgumu wewe.

Wewe hata kulala na chatu chumba Kimoja unaweza.

Mdada mrembo unaanzaje kuishabikia nyau fc.
Hayakuhusu kaka....hujui labda nimeolewa na mdau mkubwa wa Simba...
Wee kuwezaa?
 
Hayakuhusu kaka....hujui labda nimeolewa na mdau mkubwa wa Simba...
Wee kuwezaa?
Achana nae mashabiki wa yanga wengi wachawi tu. Kama siyo mchawi basi ana roho ya kichawi sema amekosa vitendea kazi.
 
Back
Top Bottom