Mzalendo_Mkweli
JF-Expert Member
- Jan 30, 2012
- 2,025
- 1,270
Yawekana Kocha wa Kibrazili Pitso Mosimane alikosekana katika mtanange uliofanyika katika uwanja wa Lucas Moripe ambapo Mamelodi Sundowns’ waliwafanyia kitu kibaya Al Ahly ya Misri kwa kuwafunga 5-0, lakini kuna mengi ya kusisimua na kujivunia jinsi huyu Mbazili alivyoshinda hiyo mechi.
Kinyume na ilivyotarajiwa, Kocha Mosimane haukuonyesha au kusema lolote la kujikuza baada walichokifanya uwanjani. Badala ya kuanza kujipia kifua na kuwaambia watu kwamba yeye na timu yake ya Sundowns ndio vidume wa Afrika kwa sasa, alibakia kuwa mnyeyekevu licha ya kwamba walikuwa wamepatia Al Ahly kipigo kikubwa kuliko vyote walikwisha vipata katika Ligi ya Mabingwa ya Caf.Ushindi huu wa kwanza wa huyu Mbrazili Mosimane ulifikiwa kwa njia ya mikakati madhubuti. Mosimane ambaye alikuwa Kocha bora wa CAF mwaka 2016 pamoja na timu yake ya ushindi (sio uchawi) waziangalia mechi Nane muhimu za Al Ahly ambapo katika hizo mechi sita zilikuwa za hatua ya makundi dhidi ya AS Vita, JS Saoura na Simba pamoja na mechi zao mbili za ligi za ligi ya misri dhidi ya Zamalek na Piramidi
"Kwanza nikiri, ni maandalizi (yaliyotusaidia kushinda mchezo huu) kwa sababu tuliangalia michezo nane ya Al Ahly," alisema Mosimane. "Tulijaribu kufinya michezo hiyo katika mawasilisho mawili ya dakika 15. Wasilisho letu la kwanza tulilifanya siku ya ijumaa (Siku moja kabla ya mechi yetu na Al Ahly) kabla ya mazoezi yetu na mwisho tulifanya wasilisho letu la pili baada ya mazoezi.Ni maandalizi yaliyotuwezesha kushinda mechi hii na sio bahati kabisa. Kilichotokea hakikutokea kwa bahati tu, aliongeza kocha Mosimane. Al Ahly labda hakujua kwamba Sundowns wanaweza kuwachimba kwa kina na kufahamu udhaifu wao kwa kiasi hiki na pia kujianda kuwakabili kwa namna ile ukizingatia kwamba sisi ni timu ndogo.
"Sidhani kwamba walitarajia hii. Lakini juu ya hayo, ni 'wachezaji wetu ambao walicheza kulingana na njia tunayocheza. Kule Misri tunaenda na tutaweka na kuongeza kasi zaidi kwa kuwatumia labda Phaka (Mahlambi), Thapelo (Morena) na Lebo (Maboe). Tutaweka kasi zaidi dhidi yao Al Ahly kwa kwa sababu watatakiwa kufunga sisi tutakapoenda kwao. Najua watajaribu kila njia kutunga goli tano.Nakuambia tunaenda kuifanya kazi yao kuwa ngumu kabisa
Sundowns tayari wameshaweka mguu mmoja katika nusu fainali za Ligi ya Mabingwa. Wao wanaenda kule pembezoni mwa mfereji wa Suez katika mchezo wao wa marudiano siku ya Jumamosi wakiwa na ujasiri kwamba mwisho mwa wiki watakuwa mojawapo ya timu nne zitakazokuwa zimesalia katika haya mashindano.Lakini kama kuna timu inayoweza kugeuza matokeo ya 5-0 basi hiyo timu ni Al Ahly ambao ni wafalme wasio na kifani katika soka la Afrika.
"Ushindi huu una maana kubwa kwa timu na watu," alisema Mosimane. "Ina maana kubwa kwangu pia.Nitasisitiza kwamba unyenyekevu ni muhimu katika kipindi hiki.
Updates
https://www.thesouthafrican.com/sundowns-cry-foul-over-al-ahly-shenanigans-after-fixture-is-moved/
https://www.sport24.co.za/Soccer/So...rules-to-destabilise-sundowns-report-20190409
Source : https://www.thenational.ae/sport/fo...-big-questions-for-egyptian-football-1.846170
https://www.iol.co.za/pretoria-news...in-the-caf-champions-leagues-history-20788088
Kinyume na ilivyotarajiwa, Kocha Mosimane haukuonyesha au kusema lolote la kujikuza baada walichokifanya uwanjani. Badala ya kuanza kujipia kifua na kuwaambia watu kwamba yeye na timu yake ya Sundowns ndio vidume wa Afrika kwa sasa, alibakia kuwa mnyeyekevu licha ya kwamba walikuwa wamepatia Al Ahly kipigo kikubwa kuliko vyote walikwisha vipata katika Ligi ya Mabingwa ya Caf.Ushindi huu wa kwanza wa huyu Mbrazili Mosimane ulifikiwa kwa njia ya mikakati madhubuti. Mosimane ambaye alikuwa Kocha bora wa CAF mwaka 2016 pamoja na timu yake ya ushindi (sio uchawi) waziangalia mechi Nane muhimu za Al Ahly ambapo katika hizo mechi sita zilikuwa za hatua ya makundi dhidi ya AS Vita, JS Saoura na Simba pamoja na mechi zao mbili za ligi za ligi ya misri dhidi ya Zamalek na Piramidi
"Kwanza nikiri, ni maandalizi (yaliyotusaidia kushinda mchezo huu) kwa sababu tuliangalia michezo nane ya Al Ahly," alisema Mosimane. "Tulijaribu kufinya michezo hiyo katika mawasilisho mawili ya dakika 15. Wasilisho letu la kwanza tulilifanya siku ya ijumaa (Siku moja kabla ya mechi yetu na Al Ahly) kabla ya mazoezi yetu na mwisho tulifanya wasilisho letu la pili baada ya mazoezi.Ni maandalizi yaliyotuwezesha kushinda mechi hii na sio bahati kabisa. Kilichotokea hakikutokea kwa bahati tu, aliongeza kocha Mosimane. Al Ahly labda hakujua kwamba Sundowns wanaweza kuwachimba kwa kina na kufahamu udhaifu wao kwa kiasi hiki na pia kujianda kuwakabili kwa namna ile ukizingatia kwamba sisi ni timu ndogo.
"Sidhani kwamba walitarajia hii. Lakini juu ya hayo, ni 'wachezaji wetu ambao walicheza kulingana na njia tunayocheza. Kule Misri tunaenda na tutaweka na kuongeza kasi zaidi kwa kuwatumia labda Phaka (Mahlambi), Thapelo (Morena) na Lebo (Maboe). Tutaweka kasi zaidi dhidi yao Al Ahly kwa kwa sababu watatakiwa kufunga sisi tutakapoenda kwao. Najua watajaribu kila njia kutunga goli tano.Nakuambia tunaenda kuifanya kazi yao kuwa ngumu kabisa
Sundowns tayari wameshaweka mguu mmoja katika nusu fainali za Ligi ya Mabingwa. Wao wanaenda kule pembezoni mwa mfereji wa Suez katika mchezo wao wa marudiano siku ya Jumamosi wakiwa na ujasiri kwamba mwisho mwa wiki watakuwa mojawapo ya timu nne zitakazokuwa zimesalia katika haya mashindano.Lakini kama kuna timu inayoweza kugeuza matokeo ya 5-0 basi hiyo timu ni Al Ahly ambao ni wafalme wasio na kifani katika soka la Afrika.
"Ushindi huu una maana kubwa kwa timu na watu," alisema Mosimane. "Ina maana kubwa kwangu pia.Nitasisitiza kwamba unyenyekevu ni muhimu katika kipindi hiki.
Updates
https://www.thesouthafrican.com/sundowns-cry-foul-over-al-ahly-shenanigans-after-fixture-is-moved/
https://www.sport24.co.za/Soccer/So...rules-to-destabilise-sundowns-report-20190409
Source : https://www.thenational.ae/sport/fo...-big-questions-for-egyptian-football-1.846170
https://www.iol.co.za/pretoria-news...in-the-caf-champions-leagues-history-20788088