Kocha mpya wa Simba SC Patrick Aussems atambulishwa rasmi leo

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Klabu ya Simba 'Wekundu wa Msimbazi' ya jijini Dar es salaam, leo imemtambulisha rasmi kocha mpya Mbelgiji Patrick Aussems, ambaye anatarajia kuifundisha klabu hiyo kuelekea kwenye maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu Tanzania bara sambamba na michuano ya Kimataifa.

Kocha Aussems amesaini mkataba wa mwaka mmoja mbele ya Kaimu Rais wa Simba, Salim Abdallah (Try Again) pamoja na Kaimu Makamu Rais Idd Kajuna, kukinoa klabu hiyo akichukua nafasi ya Pierre Lechantre raia wa Ufaransa aliyemaliza muda wake mwezi uliopita.
 
Huu ugonjwa wa wazungu sijui utaisha lini tanzania. Kocha wa maana hawezi akafunga safari kutoka ulaya akaja tanzania.
 
Masikini wachezaji wa simbaa! Huu 'mzuzu' salama kweli? Yasije yakarudia ya Karume Songoro!
 
Huyu unaweza kuta ni mlima chumvi tu huko kwao ubelgiji
 
Huu ugonjwa wa wazungu sijui utaisha lini tanzania. Kocha wa maana hawezi akafunga safari kutoka ulaya akaja tanzania.
Mwafrika akienda kufanya kazi ulaya anakuwa wa maana. Ila mzungu akifunga safari kuja Afrika kufanya kazi si maana..Ugonjwa huu utaisha lini?
 
Kocha hajui kiswahili hafu wachezaji karibia wote wanajua kiswahili na hawajui Kiinglish wala kifrenchi. Watapata tabu sana
 
Mwafrika akienda kufanya kazi ulaya anakuwa wa maana. Ila mzungu akifunga safari kuja Afrika kufanya kazi si maana..Ugonjwa huu utaisha lini?

Mishahara ya maana iko kwao. Kocha mwenye sifa za maana hawezi kutoka huko akaja huku. Umewahi kusikia mchezaji ametoka ulaya akaja africa kucheza mpira?
 
Mimi sijaona umuhimu wa kumleta kocha mwingine wakati masud djumaa anafanya vzr tu.
 
Alikuwa muuza Matikiti
Kuna mmoja kazi yake kucheza Ndombolo, lakini cha kushangaza Mbute fc [emoji196][emoji196] wamemchukua..[emoji3][emoji3][emoji3]
 
Kwa mtazamo wako huo. Lakini hujui lengo la klabu ya Simba SC
Ni saidie wewe ni lipi.


Najua presha yetu kubwa ni kwenye mechi za kimataifa msimu ujao?

Pia nahisi wameona kama kocha kashindwa kagame atawezaje caf.
 
Ni saidie wewe ni lipi.


Najua presha yetu kubwa ni kwenye mechi za kimataifa msimu ujao?

Yah..lengo nikufanya vizuri kutetea ubingwa wa VPL na kufuzu makundi michuano ya kimataifa. Kwa hivyo Djuma siyo mbaya lakini kwa klabu ya Simba anatakiwa kocha zaidi ya Djuma, ndio maana kwenye mkutano wa leo wanasema Kocha huyu Aussems mpaka kupewa kazi imetokana kukidhi vigezo kuelekea kwenye lengo la Klabu na falsafa ya klabu ambayo safari hii benchi la ufundi lilishirikisha wataalamu wa tano wa mpira ambao walimpa interview na kuridhika na kocha huyu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…