Kocha mpya wa Taifa Stars, Mkwasa atangaza kikosi kipya

hivi hawa makocha wanalipwa kiasi gani??
maana hao wazungu wakija huku wanachotewa tu hela zetu bila kujali tunafungwa au lah ila wabongo mshahara wao haueleweki kabisa.

ni bora hizo hela wale wabongo wenzetu kuliko hao vitifire wanaoletwa bila faida yoyote
 
ngja mbwana na yy ale goli nyingi nyingi naye atimimukiwe....
 
Hebu tuone,lakini safari ya matumaini kwa stars haipo kabisaaa.Ni aibu kila idara.Boko naye mwili mkubwa lakini hakuna kitu.
 
Bocco kimeo sana huyu............


Huo ni mtazamo wa kishabiki tu na chuki dhidi yake kutokana na kuboronga kwake ktk baadhi ya michezo siku za nyuma. Kuboronga kunasababishwa na vitu vingi ikiwa ni pamoja na mifumo, chemistry, ukosefu wa utimamu wa mwili, majeruhi na kutojiamini.

Lkn nakwambia kwa mtu yeyote anayejua mpira atakuambia Bocco ktk ubora wake ni kati ya washambuliaji ambao huwezi kumweka nje ya timu kulinganisha na washambualiaji tulionao Tanzania ukiacha Samatta na Ulimwengu.
 
Nilitamani sana timu ya taifa apewe kocha wa mtibwa sugar, ila kwakuwa bado ipo mikononi mwa mtanzania sio mbaya wacha tuiombee mungu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…