Labani og
JF-Expert Member
- Sep 15, 2020
- 19,637
- 29,473
KOCHA MEADEAMA ATESWA NA MAXI NA PACOME.
Yanga inavaana na Medeama kesho Desemba 8 kuanzia saa 1:00 usiku, ikitoka kulazimishwa sare nyumbani na Al Ahly ya Misri kwenye mchezo wa pili wa kundi hilo baada ya awali kufungwa 3-0 ugenini na CR Belouizdad, huku ikiwatesa wenyeji kutokana na aina ya wachezaji walionao kwa sasa kikosini.
Kocha Mkuu wa Medeama, Evance Adotey amesema wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na tahadhari kubwa kutokana na ubora wa timu wanayokwenda kukutana nao.
Kocha huyo alisema kwa Yanga ilivyo, kama vijana wake wanataka ushindi wa pili nyumbani wanatakiwa kujipanga kukabiliana na ubora wa viungo wa timu hiyo, waliounda kombinesheni iliyopewa jina la MAP, yaani Maxi Nzengeli, Stephane Aziz Ki na Pacome Zouzoua.
“Yanga hata kama imetoa sare na kupoteza bado unaona inacheza kama timu bora, wana viungo hatari sana ambao wakati wowote wanaweza kuleta shida eneo lako kama hutajipanga sawasawa. Kuna yule anayevaa jezi namba 10 (Aziz KI), mwingine ni yule jezi namba 7 (Maxi) na hata yule jezi namba 26 (Pacome) ni wachezaji wenye akili kubwa uwanjani, lazima ujue jinsi ya kukabiliana nao kwa nidhamu kubwa,” alisema Adotey
#FutbalPlanetUpdates
Yanga inavaana na Medeama kesho Desemba 8 kuanzia saa 1:00 usiku, ikitoka kulazimishwa sare nyumbani na Al Ahly ya Misri kwenye mchezo wa pili wa kundi hilo baada ya awali kufungwa 3-0 ugenini na CR Belouizdad, huku ikiwatesa wenyeji kutokana na aina ya wachezaji walionao kwa sasa kikosini.
Kocha Mkuu wa Medeama, Evance Adotey amesema wataingia kwenye mchezo huo wakiwa na tahadhari kubwa kutokana na ubora wa timu wanayokwenda kukutana nao.
Kocha huyo alisema kwa Yanga ilivyo, kama vijana wake wanataka ushindi wa pili nyumbani wanatakiwa kujipanga kukabiliana na ubora wa viungo wa timu hiyo, waliounda kombinesheni iliyopewa jina la MAP, yaani Maxi Nzengeli, Stephane Aziz Ki na Pacome Zouzoua.
“Yanga hata kama imetoa sare na kupoteza bado unaona inacheza kama timu bora, wana viungo hatari sana ambao wakati wowote wanaweza kuleta shida eneo lako kama hutajipanga sawasawa. Kuna yule anayevaa jezi namba 10 (Aziz KI), mwingine ni yule jezi namba 7 (Maxi) na hata yule jezi namba 26 (Pacome) ni wachezaji wenye akili kubwa uwanjani, lazima ujue jinsi ya kukabiliana nao kwa nidhamu kubwa,” alisema Adotey
#FutbalPlanetUpdates