NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Kocha Mkuu wa USM Alger Benchikha Abdelhak amesema bado ni 50 kwa 50 kwa kikosi chake kutwaa ubingwa wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika, licha ya kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Young Africans jana Jumapili (Mei 28).
Young Africans ilikuwa nyumbani Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam ikishuhudiwa na Mashabiki na Wanachama wake, lakini ilishindwa kufurukuta, na sasa inajipanga kwenya kujiuliza kwenye mchezo wa Mkondo wa Pili utakaopigwa Jumamosi (Juni 03) nchini Algeria.
Kocha Benchikha amesema inafurahisha kushinda ugenini, lakini bado wana kazi kubwa katika mchezo wa Mkondo wa Pili ambao anaamini utakua mgumu zaidi, kwa sababu utakwenda kuamua nani atakuwa Bingwa wa Kombe la Shirikisho msimu huu.
Young Africans ilikuwa nyumbani Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam ikishuhudiwa na Mashabiki na Wanachama wake, lakini ilishindwa kufurukuta, na sasa inajipanga kwenya kujiuliza kwenye mchezo wa Mkondo wa Pili utakaopigwa Jumamosi (Juni 03) nchini Algeria.
Kocha Benchikha amesema inafurahisha kushinda ugenini, lakini bado wana kazi kubwa katika mchezo wa Mkondo wa Pili ambao anaamini utakua mgumu zaidi, kwa sababu utakwenda kuamua nani atakuwa Bingwa wa Kombe la Shirikisho msimu huu.