OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Natoa wito kwa TFF na hata club ya Yanga,kumdhibiti kocha Luc mapema iwezekanavyo. Nimemsikiliza mahojiano yake baada ya kupigwa na Azam ameonyesha dhahiri kwamba ni kiburi na mzushi kuliko kiasi.
Kinachonisikitisha zaidi ni kuingiza ubaguzi wa rangi katika michezo. Tanzania na ubaguzi wa rangi wapi na wapi. Amenyimwa mkono kama ambavyo angenyimwa Matola au Masta Mkwasa.
Nimemsikia pia akisema ingekuwa Congo mashabiki wangeingia uwanjani. Hii ni kauli ya kichochezi.