hekimatele
JF-Expert Member
- May 31, 2011
- 9,890
- 2,795
Wadau katika pita pita zangu nimekuwa nikisikia juu ya ongezeko la kodi kwenye maeneo mbalimbali ya uchumi.
Aidha watu wengi wamekuwa wakilalamika juu ya ongezeko la kodi kwenye vinywaji vya kileo.
Leo nimekutana na mfanyabiashara mmoja analalamika kuhusu ongezeko la kodi. Anaendesha biashara ya Pub ambapo anauza vinywaji.
Awali anadai alikuwa analipa hadi mpaka 360,000/- kwa mwezi ikiwa ni kodi ya mapato. Kwa mujibu wa bajeti hii mpya ambayo itaanza kutumika rasmi kuanzia Julai watatakiwa kulipa asilimia 100 juu yake. Kwa ufupi atatakiwa kulipa 720,000/- kwa mwezi.
Ukija kwenye uhalisia, wakati analipa kodi ya mwanzo alikuwa anasuasua kwa sababu biashara yake ina msimu. Kuna msimu ambao kwa siku anauza mpaka bia chupa 5 tu, na kuna msimu anauza mpaka kreti 3 kwa siku.
Sasa hivi anafikiria kufunga biashara yenyewe kwa sababu haitamlipa.
Swali langu kwa TRA, wamefikiria nini mpaka kuongeza hiyo kodi katika kiwango hicho?
Hawaoni kuwa watapoteza pato kubwa badala ya kuongeza? Na pia kuongeza mianya mingi sana ya wafanyabiashara wengi kukwepa kodi?
Kuongeza kodi kwa bidhaa za ndani ndio njia pekee ya kuongeza pato la ndani? Na je hawaangalii athari zinazotokana na ongezeko Hilo?
Karibuni tuchangie kwa pamoja great thinkers manake athari zimeshaanza kujitokeza kwenye uchumi ambapo mwishowe itasababisha more unemployment and leading to crimes in the country.
Aidha watu wengi wamekuwa wakilalamika juu ya ongezeko la kodi kwenye vinywaji vya kileo.
Leo nimekutana na mfanyabiashara mmoja analalamika kuhusu ongezeko la kodi. Anaendesha biashara ya Pub ambapo anauza vinywaji.
Awali anadai alikuwa analipa hadi mpaka 360,000/- kwa mwezi ikiwa ni kodi ya mapato. Kwa mujibu wa bajeti hii mpya ambayo itaanza kutumika rasmi kuanzia Julai watatakiwa kulipa asilimia 100 juu yake. Kwa ufupi atatakiwa kulipa 720,000/- kwa mwezi.
Ukija kwenye uhalisia, wakati analipa kodi ya mwanzo alikuwa anasuasua kwa sababu biashara yake ina msimu. Kuna msimu ambao kwa siku anauza mpaka bia chupa 5 tu, na kuna msimu anauza mpaka kreti 3 kwa siku.
Sasa hivi anafikiria kufunga biashara yenyewe kwa sababu haitamlipa.
Swali langu kwa TRA, wamefikiria nini mpaka kuongeza hiyo kodi katika kiwango hicho?
Hawaoni kuwa watapoteza pato kubwa badala ya kuongeza? Na pia kuongeza mianya mingi sana ya wafanyabiashara wengi kukwepa kodi?
Kuongeza kodi kwa bidhaa za ndani ndio njia pekee ya kuongeza pato la ndani? Na je hawaangalii athari zinazotokana na ongezeko Hilo?
Karibuni tuchangie kwa pamoja great thinkers manake athari zimeshaanza kujitokeza kwenye uchumi ambapo mwishowe itasababisha more unemployment and leading to crimes in the country.