Kodi ya tsh 12000 kwa mwezi stanbic current account imekaaje?

Kodi ya tsh 12000 kwa mwezi stanbic current account imekaaje?

tanira1

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2011
Posts
942
Reaction score
159
wakuu naomba kujulishwa hii tozo ya sh 12000 kwa mwezi kwa ajili ya current account imekaaje mbona mimi siilewi kabisa licha ya liba kubwa wanazochukua licha ya kufanyia biashara fedha zetu bado wanatoza 12000 yaani imepanda kwa asilimia 1200 nafikiri hii si sawq selikari iingilie kati
 
Baada ya kukata hiyo 12,000 wanakukata pia account administration 2,500. Ni wizi mtupu! Kuhusu riba ni mabenki yote, watakuambia 18% ukija ku calculate unakuta 40 - 55% Ni nchii hii tu ambapo hakuna usimamizi wa riba za mabenki? Sijui financial act na memorundums kama zinasema chochote juu ya riba!
 
Inapotokea unapokopa kwenye mabenki yetu kama mfanyabiashara au mfanyakazi, hesabu zinaonyesha utarudisha kati ya asilimia 40 - 60 zaidi ya kile ulichokopa. Percentage hii inategemea muda wa kulipa. Nataka wenye utaalamu watueleze sheia ya fedha inasemaje juu ya asilimia ya jumla atakayorejesha mkopaji baada ya kuchukua kiasi fulani cha fedha? Je sheria iko kimya hivyo kuyapa mabenki kufanya maamuzi kwa kadri wanavyojisikia? Naomba tuliweke hili wazi ili liweze kuamsha majadiliano na pengine mabadiliko. Na hii inaweza pia kuleta changamoto wakati huu ambao tunafikiria kuwa na morgage act. Kwa nchi za wenzetu (zilizoendelea) riba wakati mwingine haifiki hata 5%.

Cha ajabu ni kuwa, wakati mabenki yakiendelea kutangaza kupata faida, bado yamekuwa yakiongeza riba, gharama za ATM withdraw, transfer, deposit, nk.
 
Muda sio mrefu watatia Akili,Maana mwenendo wa makampuni ya sim ndio kiboko yao.
Kuna watu wenye vimitaji vidogo wameamua kuweka pesa zao kwenye sim tu
 
Hawa Stanbic wahuni tu. Ukiwauliza wanakwambia watatoa mikopo. kila siku ni hadithi ya kama mama kuku anawadanganya wanae lini watanyonya. Mikopo awatoi na watu kila kukicha wanaikimbia benki yao
 
...nimekuwa mteja wa stanbic Bank kwa muda wa miaka miwili na zaidi; kwa ujumla hawana utaratibu mzuri, linichukua mkopo bila kuwajua kiundani, mara nyingi terms and conditions zao haziko wazi. Pia kulikuwa na wafanyakazi walikuwa wanachezea A/C za wateja, pia utaratibu wa riba walionao siyo mzuri.
Kuna ubabaisha wa hali ya juu.
 
Hawa Stanbic wahuni tu. Ukiwauliza wanakwambia watatoa mikopo. kila siku ni hadithi ya kama mama kuku anawadanganya wanae lini watanyonya. Mikopo awatoi na watu kila kukicha wanaikimbia benki yao
...si kushauri kwenda kukopo pale!
Sisi walikuja kazini kwetu wakatutangazia kuwa wameshusha RIBA ya mikopo hadi 15%, baada yakupita miezi3 ya kuchukua mikopo tulipandishiwa RIBA hadi 21%
Tuliwafuata ofisini kwao haikusaidi, mpaka mameneja walikuwa wanatukimbia, na wakati mwingine unapigwa danadana.
"mwisho wasiku tulidanganywa na kuambiwa kuwa ni agizo kutoka Benki Kuu"
 
Hivi humu JF tukianzisha kitaasisi chetu itakuwaje,maana kesi hizi zipo nyingi za mabenki.na pia humu tumo wengi
 
washenzi hawo.wamepiga hela za mikopo kule kkoo sasa hasara ndo inawatafuna na vijana wamesha kimbia walio fanya hayo madeal.Mie nimewahama siku hizi niliona naibiwa hovyo hovyo.na kibaya zaidi nilipata pesa Fake kwenye ATM machine yao wajinga kabisa.
 
wakuu naomba kujulishwa hii tozo ya sh 12000 kwa mwezi kwa ajili ya current account imekaaje mbona mimi siilewi kabisa licha ya liba kubwa wanazochukua licha ya kufanyia biashara fedha zetu bado wanatoza 12000 yaani imepanda kwa asilimia 1200 nafikiri hii si sawq selikari iingilie kati

Average monthly charges kwa current account ni 12,000 b'se of feature unazopata forexample

Cheque counterfoils and monthly statements provide a reliable means of keeping a record of transactions.  Electronic banking facilities allow customers to operate their accounts after banking hours in the comfort of their home or office.  Several signatories can be appointed on one account and businesses may choose the details they want printed on their cheques.  Overdraft facilities can be arranged.  Standing / stop orders can be loaded.  Interest can be earned on minimum monthly balance and a small monthly service fee is applied.  Customers have access to expert business and financial advice from an experienced and dedicated business bankers and Relationship Managers of the bank

So kama imekushinda waweza fungua account nyingine kama T plus account
 
Kwanini usifungue savings tu a/c? Bongo tumeathiriwa sana na ubepari uchwara sasaivi, watu wanatafuta pesa kwa nguvu bila kufanya kazi/
 
washenzi hawo.wamepiga hela za mikopo kule kkoo sasa hasara ndo inawatafuna na vijana wamesha kimbia walio fanya hayo madeal.Mie nimewahama siku hizi niliona naibiwa hovyo hovyo.na kibaya zaidi nilipata pesa Fake kwenye ATM machine yao wajinga kabisa.
Kweli kabisa imegeuka kuwa benki ya kijahili 2.Nchi hii haina Regulator wa ukweli maana dalili zote mbaya zinaonekana ila Benk Kuu imelala.Ngoja tusubir majanga 2
 
Tatizo ni Benki kuu ambao kama sikosei ndio wasimamizi wa hizi banki. Mnapokuwa na rais aliyeingia madarakani kwa wizi wizi na kuwa na viongozi goi goi AMBAO HUCHELEWA KUTOA MWONGOZO TATIZO LAKE NDILO HILO KILA SEKTA NI UVUNDO TU.
 
Hapana tatizo wala si BOT Tatizo ni lao hao Stanbic bank kwa kutojali wafanya kazi wao.wala kujali wateja wao.kwanza ni Bank ya makaburu hiyo wamekuja kuvuna hapa.tusubilie mwakani ndo tutajua baada ya taarifa za mabank BOT watatoa orodha ya bank zisizofanya vizuri na zitakazo fungiwa kutoa service.hapo sasa kama sinto ona orodha ya stanbic bank kufungiwa ndo ntajua BOT wazembe>mbona waliweza kwa Barclays mwaka jana na matawi yake yakafungwa?
 
Back
Top Bottom