Koffi Olomide ashitakiwa kwa kupigana

Koffi Olomide ashitakiwa kwa kupigana

Pasco_jr_ngumi

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2010
Posts
1,802
Reaction score
283
Koffi Olomide, ambaye ni mwanamuziki mashuhuri
barani Afrika ameshitakiwa kwa kumpiga
Mtayarishaji wake wa muziki. Mwanamuziki huyo alikamatwa na kufungiwa katika
kituo cha polisi na kufikishwa mahakamani
jumatano. Koffi alikamatwa kufuatia vurugu katika hoteli moja
mjini Kinshasa. Waandishi wa habari wanasema mahakama hiyo ya
Kinishasa ilifurika kutokana na watu wengi kuja
kumuona kiongozi huyo wa bendi ya Quartier Latin
akiwa kizimbani. Kesi hiyo iliharishwa hadi Alhamisi asubuhi wakati
atakaposhitakiwa rasmi. Wakati wa kesi hiyo hapo jana Koffi Olomide
aliwakilishwa na mawakili 10. Ugomvi kati ya mwanamuziki huyo na mtayarishi
wake Bwana , Diego Lubaki, ni kuhusu pesa dola
$3,680. Hakimu alimfahamisha mwanamuziki huyo ikiwa
atapatikana na hatia huenda akafungwa jela miezi
sita. Olomide ni gwiji wa muziki aina ya "soukous",
mtindo ulitokana na jina la kifaransa "secouer", lenye
maana ya kujitikisa au kujinengua ,na wachezaji
wake vile vile wanatambulika kwa kunengua
maungo.

Source. bbc swahili
 
Tayari katiwa hatia na kapatiwa kifungo cha miezi mitatu iwapo atafanyakosa jingine tena wakati huu.
 
Hii si habari njema hata kidogo.Kiio cha jamii kinapochafuka...watazamaji wataonaje sura zao katika kioo hicho??Ninasikitika.
 
achana kabisa na koffi ni noumer, hao wote wanafuata nyuma, mengine hayo ni upepo tu unapita
 
ngoja akapakatwe kidogo na masela wa kinshasha jela ili akitoka ajirekebishe na aheshimu utu wa wengine
 
achana kabisa na koffi ni noumer, hao wote wanafuata nyuma, mengine hayo ni upepo tu unapita

binafsi nam-feel ile kinoma huyu jamaa. kwanza bonge la TOOZI, show yake pale Mwanza Yatch Club 2006 nili-enjoy vya kutosha. POLE SANA PAPA MOPAO MOKONZI. MAKILA MABE, BOLINGO NANGAI, ha ha haaa!!!!
 
Nampenda sana huyu msomi msanii. yatapita tu papaa pole sana.
 
Waswahili bana,badala ya kujadili kesi wameanzisha malumbano ya nani zaidi,mnapotosha mada kama wabunge wa CCM
 
Loo, simpendi huyu....,
Mambo yote ni Werasson

bila simba hakuna yanga. Uwepo wa timu hizo huongeza ushindan ambao huwafanya waongeze bidii. Uwepo wa olomide na werra huwafanya kila mmoja ajitahid kufanya vizur il ampite mwenzie, matokeo yake wewe shabiki wake unata kitu supa.
 
Mopao Mokonzi ni MKOROFI SANA, hili sio tukio la kwanza kupiga wadau wa muziki wa kundi lake. walishwai kuzichapa na Felix Wazekwa akimtuhumu kumuiga staili ya uimbaji
 
mambo yote jb mpiana,dance kinkole!

feux de l'amour, hii ngoma ilikua MEGA HIT, haijawai kupata kutokea rhumba kali congo DRC kama hii iliyoporomoshwa na JB Mpiana. inshort Mopao hatii mguu kwa Jean Bedel Mpiana haswa kwa muziki wa rhumba.
 
Back
Top Bottom