Koffi Olomide azidi kukinukisha mbaya

Miye nimesikiliza nyimbo nyingi kwenye hiyo album, lakini naona haijakaa poa kama ile ya 13 appotrè yenye nyimbo kama selfie, cobetox, symposium au album ya Abradacababra yenye nyimbo kama je taime na toukoutou. Maoni yangu
 
Habari zenu wanajukwaa! Bila shaka mu wazima wa afya.
Mwaka huu umekua hauna likizo kabisa kutokana na Kamanda Koffi Olomide Mopao Mokonzi Quadra Korea Man
Quadra= 4
Korea Man=Kora man
Kora=Tuzo za muziki za Afrika

"Quadra Koraman": Koffi hujiita jina hili ili kukumbushia kuwa yeye ndo mwanamziki pekee wa DRC kuwahi kuchukua tuzo 4 kwa mpigo za Kora kule South Africa kwa mwaka 2002/3 kupitia albamu ya 'Efrakatta' iliyotolewa mwaka 2002. Tuzo alizoshinda ni 'Best Male Artist', 'Best Male Central Africa', 'Best Video' na 'Jury Special Prize'.
 
Kuna sehem nimemsikia akitaja jina 'Jack Pemba' ktk hiyo ngoma Charisme ni huyu huyu jamaa aliesumbua miaka fulani hapa bongo na nasikia anaishi Uganda kwa sasa au sijasikia vzr tu hapo
ndio jack pemba mwenyewe huyo yuko uganda sasa hv
 
Je, wabongo watafikia kiwango hicho?

Wabongo wapi? Wakina alichoki na rogati hega wanaoimba flat? Bongo kama sio hawa wakongo wakina pacho na kina christian bella musiki ya rumba tungesikia kwa maredio tu.
 
Asante sana mkuu kwa taarifa....Hiyo Kora nimefanya typing error.
Kuhusu maana nilikua naelewa tofauti
Qudra =4
Kora=fanya,act,do (Nyarwanda)
Man=man
Kumbe nilikua nakosea. Asante kwa kunitoa tongotongo
 
Miye nimesikiliza nyimbo nyingi kwenye hiyo album, lakini naona haijakaa poa kama ile ya 13 appotrè yenye nyimbo kama selfie, cobetox, symposium au album ya Abradacababra yenye nyimbo kama je taime na toukoutou. Maoni yangu
Ni kweli ata mi siko mbali na mtizamo wako kwenye 13ème apôtre ukiongeza piscioles, changement de mentalite na 13ème apôtre yenyewe.
Hapo kwenye abracadabra ukiongeza jeune pato kazini siendi kabisa
 
Biso biso kinshasa makambo kende malamu te.. 😛 😛
 
Weka audio ya CHARISMA mkuu kweli unamjua Mopoa vilivyo kabisa na hongera kwa uchambuzi,ivi supersonic mirage yupo wapi siku izi?
 

Hii kitu " Alidor" nilikuwa sijaipata mzee mwambie muhudumu akuongeze zinginine na dj airudie tukeshe hapa
 
Daaaah haya makitu huwa yanafanya nisahau shida zote za kibongo bongo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…