Koffi Olomide deported following JKIA assault

huyu ndio mwanaume wa ukweli....mwanamke akizingua hapo hapo onyesha tofauti yenu sio mambo ya kuongelea pembeni wana midomo domo sana hawa wakina dada
Acha huo ujinga ....
 
Safi sana,anadharau sana huyu,sijui kwa vile ana hela,ndo maana hawezi kanyaga ulaya,maana anahitajika Paris ili kujibu mashitaka ya kumbaka dancer wake,aendelee kumuonea huyo huyo mjinga mjinga Cindy le coeur

Victoire,

Huyu demu Cindy le Coueur namuonea huruma jinsi Koffi anavyomnyanyasa. Na yeye mwenye amekuwa kusema mtu aiye jihurumia, maana amekuwa kama msukule. Unakuta Koffi anaondoka na mwanamke mwingine baada ya show lakini yule demu hathubutu hata kuleta vurugu. Amefanywa kama mke - Kijakazi (refer to biblical days stories jinsi wafalme / Matajri walivyokuwa wanalala na kuzaa na vijakazi wao).
Niliona mwaka juzi Koffi akifanya sherehe ya kumkabidhi babake Cindy gari aina Jaguar (kuu kuu sijui la mwaka gani🙂 kama sehemu ya mahari. Na sasa kusikia tayari ameshazaa na Kofii nikasema mtoto kwisha habari.

Inasemekana Koffi alimwahidi mambo makubwa lakni kubwa ikiwa ni kujenga jina na Kipaji chake. Lakini mwisho wa siku si jingine kubwa ni affair. Hivyo kipaji cha Cindy ndani ya bendi ya Koffi Olomide ni cha 'kutumiwa' zaidi kuliko kuendelezwa.

Binafsi kwa mtazamo wangu naona ni afadhali Cindy angalibakia kuwa Gospel Singer kule kwenye bendi ya Pastor Charles "Carlyto' Lassa, (The ex le TP OK Jazz Band legendary Vocalist singer back in the good old days 70's to late 80's) kabla ya kurubuniwa na Koffi na kuishia.

Hebu mtazame (kwenye video attached below) hapa Bi Cindy alipoanzia akiwa Gospel singer kwa Pastor Carlyto Lassa.Katika safu ya wasichana kwenye hii video ni wa kwanza kutoka kulia.


Wikiendi njema.
 

Mkuu, kuna watu wanasema kuwa wakongo ni wachawi sana...you never know!!
 
Hakufanya kitu kizuri kabisa

Maana nilimfikiria mama angu zaidi nilipoona hilo teke
 
Kashishi Cindy hajazaa na koffi,akibeba mimba koffi anamwambia atoe,Koffi anasema hahitaji mtoto nje ya ndoa,Koffi ana mke wa ndoa na watoto wanaishi Paris,Huyu Cindy ni kama msukule tu,pozeo,yaani mpaka namuhurumia.Cindy ana kipaji na angeweza hata kuimba Solo na kumiliki bend yake,ila ndo hivyo kishakuwa pozeo la koffi wakati Mke wa Koffi akiwa analea watoto Paris.Na koffi anasemaga wazi wazi kabisa kuwa mali zake zote ni za wanae na mkewe na mahawara hawana chao.
 
I don't see this happening in Tanzania. Well done Kenyans. Huku kwetu mchina kampiga hadi kumuua mfanyakazi aliyedai nyongeza ya mshahara na vyombo vya ulinzi vimehamia Dodoma kwenye mkutano wa chama.

Mwekezaji haguswi.
 
Inawezekana hili la Wakenya kuja juu kuonyesha msimamo wao dhidi ya unyanyasaji wa wanawake likaifungua macho Serikali na hivyo kuanzia sasa kuweka nguvu katika kupambana na udhalilishaji wa wanawake kwa namna yoyote ile, iwe hadharani au majumbani mwa wahusika. Serikali inaweza kuona kwamba kwa kupinga udhalilishaji dhidi ya wanawake inaweza kujiongezea umaarufu na kujiongezea kura kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2017.

Wakenya wanafiki.

Mbona Gavana Kidero alimpiga kofi mbunge Rachel Shebesh na hakufanywa kitu?

Na mpaka leo hii bado ni gavana!

Upuuzi mtupu.
 
Hongera kwako pia Mkuu kwa kuwa wa kwanza kupinga kitendo kile pamoja na kushambuliwa na baadhi humu. I salute you Sir.


Mkuu BAK bado tunasafari ndefu sana.
 
Ahsante sana kwa kuandika ukweli kuhusu nini kingetoka kama hili lingetokea Tanzania. Ngoja tusubiri tuone hili la Mchina muuaji. Kuna Wachina maelfu ambao wanaishi nchini kiharamu lakini hata siku moja hutasikia wamekuwa deported bali utasikia waliokamatwa na Waethiopia na wengine wa mataifa ya Afrika. Kulianzishwa zoezi la kusaka wahamiaji haramu na hii awamu ya tano, kumbe ilikuwa nguvu ya soda, limeisha kimya kimya.

I don't see this happening in Tanzania. Well done Kenyans. Huku kwetu mchina kampiga hadi kumuua mfanyakazi aliyedai nyongeza ya mshahara na vyombo vya ulinzi vimehamia Dodoma kwenye mkutano wa chama.
 
Waipate fresh kwa mpango gani? Congolese are not stupid to support huyu mpuuzi na hakuna chochote atafanya zaidi ya kuomba msamaha zaidi akifika kwao, kwanza inabidi awe arrested akifika Congo kwa kumshambulia mwanamke wa Congo
 
Sana Mkuu yaani nasoma baadhi ya wachangiaji walivyoandika humu mpaka nashangaa. Sijui kama wanaweza kuandika wanavyoandika kama yule aliyedhalilishwa angekuwa binti yao au kama wana mabinti watakubali mabinti wao wadhalilishwe kiasi kile.

Mkuu BAK bado tunasafari ndefu sana.
 

My friend, nakuelewa sana.

Ila hapa serikali ya Kenya imeonyesha unafiki ulio wazi kabisa.

Evans Kidero, Gavana wa county ya Nairobi, county kubwa na ya muhimu sana Kenya, alimzaba kibao Rachel Shebesh mbele ya watu na akanaswa na kamera.

Hiyo ilikuwa miaka kama miwili au mitatu ilopita, kama nakumbuka vizuri.

Sasa rafiki, hebu tusemezane. Kitendo alichofanya Kidero ni sawa kweli? Kinateteeka kweli? Na kimsingi, kina tofauti gani na kitendo alichofanya Koffi jana?

Gavana wa county ya Nairobi ni mtu mkubwa sana. Huyu jamaa kwa kitendo chake hicho alipaswa kujiuzulu au kulazimishwa kujiuzulu kwa namna moja au nyingine na binafsi ningependelea kuona anachukuliwa hatua kali za kisheria.

Pengine ni Afrika tu ambapo kiongozi mkubwa namna hiyo anaweza kumpiga mwanamke [au mtu yeyote yule iwe mwanamke au mwanamme] hadharani na bado akaendelea na kazi yake.

Imagine Gov. Andrew Cuomo anamzaba kibao mmoja wa female state representatives tena ofisini kwake mbele ya watu na kamera. That would cook his goose. It would be political suicide and he will never be governor again.

Lakini kwa Kenya...aah jamaa bado anadunda tu. Sasa jana Koffi kumpiga teke mcheza shoo wake eti Kenya nzima kuna outrage na wamemfukuza huyo falla.

Where was this outrage when Kidero slapped Shebesh? Hypocrisy much? Double standards much?

Halafu, huyu Kidero hana uwezo kudhibiti hasira zake. Ona hapa juzijuzi tu alitaka kupigana na seneta wa Nairobi, Mike Sonko.


Huyu Kidero, a woman beater, eti ndo gavana wa Nairobi. Shame on Kenyans.

Na simtetei Koffi. Kwanza naona alichopata ni kidogo sana. Alipaswa kunyea debe walau wiki nzima halafu ndo afukuzwe.

Lakini pia unafiki unapokuwa dhahiri namna hii lazima nao tuuseme tu.
 

Mkuu, kuna watu wanasema kuwa wakongo ni wachawi sana...you never know!!

Ni kweli kabisa. Koffi husifika sana kwa sifa ya ushirikina ('Ulozi' kama wenyewe waitavyo kule DRC) akihusishwa zaidi na Mama yake mzazi inadaiwa na kusemekana kuwa ati ndiye "Gwiji" na mhimili wake mkuu katika mafanikio yake ya kimuziki.

Nakumbuka safari moja nilikuwa jijini Kinshansa, DRC na ilikuwa wana long weekend holiday pale. Ikatokea kwamba weekend hiyo Koffi naye alikuwa anapiga show ya kufa mtu pale Hilton Hotel. Hii ilikuwa show ya oldies but goodies (yaani Bakulutu... aka "Rumbha Solosolo" ikiwa lengo ni pamoja na kuwaenzi nyimbo za wanamuziki wa kale...achana na hii abrakata anayopigia show za vijana siku hizi.

Nakumbuka kiingilio ilikuwa $100.00 kila kichwa.Tulipofika dirisha ya kuhakiki na kununua tiketi mwenyeji wangu alinitonya kuwa huyo Bi mkubwa anayechukua pesa (Cashier) ndio Mama mzazi wa Koffi. Binafsi nilishangaa sana nikauliza mwenyeji wangu kwani huyu jamaa hana management team. Nikaambiwa Koffi anapopiga show Kinshansa mshika pesa ni mama yake. Na hata hiyo inayoitwa 'management team' inamgwaya huyo mama jinsi alivyokuwa authoritative.

La mwisho ni kuwa kuna jambo moja ambalo nimeli note ambalo kwa Koffi liko tofauti na wanamuziki wengine. Koffi Olomide nimemuona hapendi ku entertain (au ku encourage) habari ya 'kumtunza' awapo jukwaani akiwajibika. Unamuona kabisa kuwa hapendi au hakaribishi au siyo rafiki wa hiyo tabia. Na akiipokea ile pesa huwa haitii mfukoni mwake kama wanamuziki wengine tuliowazoea wawapo majukwaani. Yaani akipokea tu huziweka (kusanya) zile pesa kwenye sakafu. Na yeye siye ataondoa hizo pesa kwa floor. Nimekuwa nikijiuliza na hii nayo ni nini au ndio masharti ya wale jamaa ma consultants🙂 (akina Babalao au Sangoma) Hahaha

Haya bwana wikiendi njema.
 

Hahaha..Hawa jamaa wa DRC ni noma sana. Mkuu story yako inanikumbusha miaka ya nyuma wakati nahudumia kambi za wakimbizi wa kongo nchini Tanzania. (intake ya 1997). kawaida, kabla mkimbizi hajapewa hifadhi, tulikuwa tunamfanyia "Refugee status determination" ili kujilidhisha kama kweli wanastahili kuitwa wakimbizi. kwa wale niliowasahiri, kama 05 hivi walikuwa hawakidhi vigezo, sasa siku ya kusoma majina yao,...Ilikuwa kimbembe. unatafuta jina kwenye karatasi halionekani.....tafuta weeeee! Ikabidi niahirishe zoezi. Lakini wakati narudi ofisini nikaanza kuona majina yaleyale niliyokuwa nayatafuta kwa tochi kwenye karatasi hiyojiyo.....
Kuna jamaa aliwahi kunisimulia kuwa DRC wana-conduct witchcraft festival kama Bongo tunavyosherehekea sabasaba/nanenane......

Good evening Boss
 
huyu ndio mwanaume wa ukweli....mwanamke akizingua hapo hapo onyesha tofauti yenu sio mambo ya kuongelea pembeni wana midomo domo sana hawa wakina dada

Unatakiwa kupimwa Ubongo. Kama bado unaamini alichokifanya ni kipimo cha Uanaume.
 
Safi sana wakenya, kwa hili mmenifurahisha sana. Huu unafaa uwe mfano wa kuigwa. Mimi nikikuona unampiga mwanamke mbele yangu basi ujue nahusika moja kwa moja, lazima nikupe vitasa vya maana uweke kumbukumbu maishani mwako.
Unaweza dundwa wewe badala yake, usijiaminishe hivyo. Nakumbuka shule aliwahi dundwa mbabe mmoja aliyekuwa anatusumbua sana na jamaa wa kawaida.
 
silipendi likofi alamude...sawa kabisa wame likick out! pole sana dada...
 
Safi sana... uonevu mkubwa kaonyesha Koffi.. na mbaya zaidi alimpiga teke la nguvu dancer wake wa kike Jomo Kenyatta airport, very shame...!!
PAMELA-OLOMIDE DID NOT ASSAULT ME!

The victim, identified as Pamela, has, however, denied that she was assaulted by the Selfie hit-maker despite the action being caught live on camera.

“Dear fans of Koffi Olomide, I would like to tell you that Koffi did not attack me, it was a girl at the airport that was threatening me and Koffi came to defend me…Koffi can never beat us in public, and we all know that Koffi loves his dancers and he can never do something like that,” said Pamela in a video shared on Koffi Olomide’s Facebook page Friday.
She added: “For your information, Koffi does not beat us. For all those who love Koffi, I want to tell you that Koffi is not someone who is aggressive… he loves us very much and it’s just a girl who came and started attacking us. As far as we are concerned, we don’t have any problem. We came for a concert. We are in good terms with Koffi. He is our president and he never harms us.”
Koffi Olomide on his side expressed disappointment at how social media users and a section of his fans in Kenya reacted to his alleged assault.
“I watched the video with a lot of distress where it seems that I was assaulting one of my dancers. On the contrary I was defending my dancers from a lady who was threatening them at the airport. I respect women and everyone knows that I do. I would like to apologize to all women because of my actions but I was defending my dancers.”
 
PAMELA-OLOMIDE DID NOT ASSAULT ME!

The victim, identified as Pamela, has, however, denied that she was assaulted by the Selfie hit-maker despite the action being caught live on camera.

“Dear fans of Koffi Olomide, I would like to tell you that Koffi did not attack me, it was a girl at the airport that was threatening me and Koffi came to defend me…Koffi can never beat us in public, and we all know that Koffi loves his dancers and he can never do something like that,” said Pamela in a video shared on Koffi Olomide’s Facebook page Friday.


She added: “For your information, Koffi does not beat us. For all those who love Koffi, I want to tell you that Koffi is not someone who is aggressive… he loves us very much and it’s just a girl who came and started attacking us. As far as we are concerned, we don’t have any problem. We came for a concert. We are in good terms with Koffi. He is our president and he never harms us.”

Koffi Olomide on his side expressed disappointment at how social media users and a section of his fans in Kenya reacted to his alleged assault.

“I watched the video with a lot of distress where it seems that I was assaulting one of my dancers. On the contrary I was defending my dancers from a lady who was threatening them at the airport. I respect women and everyone knows that I do.

I would like to apologize to all women because of my actions but I was defending my dancers.”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…