Zakayophillyx
JF-Expert Member
- Jun 2, 2012
- 306
- 103
Kwani sebene limeanzia wapi? Kama ni gitaa basi OK Jazz na TP OK Jazz ya Luambo ni habari nyingine kabisa. Shiko Mawatu (Soukus Stars, amepiga sana na Madillu post OK Jazz) anakuambia akiulizwa wapiga solo wakali 3 kushinda wote huko DRC atakuambia ni (1) FRANCO, (2) LUAMBO, (3) MAKIADI hayo yote ni majina ya mtu mmoja. Syran Mbeza (Lovy du Zaire, Kekele, 4 Stars) ametoa album inaitwa Immortal Franco: Africa’s Unrivalled Guitar Legend. Hapo ingiza solo la Papa Noel, Gerry Dialungana,na Bass la Mpudi kionjo cha rythm ya Papa Lutumba, Makoso, unapata kitu Papa Tshimanga Asossa (Negro Success, Lipua Lipua, Kamale, Fuga Fuga, Sikinde, Marquis, Bana Marquis) anakuambia ngoma ya watoto hailali, lazima wakubwa watambe. OK Jazz (1956-1993) haitegemewi kutokea tena. Bingwa wa muziki wa taratibu enzi hizo alikuwa OK Jazz katika mtindo wa BOLERO-ingia Youtube tafuta "suite letter no 1" uonje utamu.sebene lipo?gitaa maana raha ya congo man hata nyimbo ikiwa ya taratibu unacheza kiboss boss hapo ndo koffi alipotuwin
Franco Luambo atakuwa ni mkulima
Kwangu Mimi Pepe kalle ni zaidi, ngoma zake zote ni kali, ataimba kiswahili sawa, kingereza au kifaransa sawa tuu, ukija kilingala ndo kabisa,Leo acha niseme ukweli wakuu,watu wanapenda kutompa mtu sifa zake mpaka afe.
Toka kizazi cha kina Lwambo mpaka sasa kina ferre na fally hakuna msanii wa kumlinganisha na koffi kimuziki apo Congo.Sema watu wanapenda kutukuza vitu vya kale kama kwenye mpira wanavyompaisha Pele na Maradonna wakati messi na Ronaldo wamefanya mengi makubwa tu.
Sasa basi hata kwenye mziki,utasikia sijui Madilu,Papa wemba sijui nani.Ndio wametoa nyimbo kali sana lakini hakuna aliefanya consistency ya nyimbo nyingi kuwa juu kama koffi.
Hata huyo Werrason bado anapaishwa tu kwa nyimbo chache ukifananisha na Koffi.
Tukubali tu wakuu hakuna kama Koffi kwenye muziki wa boringo.
Inaitwa Maggie, ilikuwa ni moja ya hit song iliyofanywa na Koffi Papaa Mopao akishirikiana na kundi lake la Quartier Latin na ndo ilibeba jina la album iliyotoka 1994.Kuna ile ngoma inaimbwa...nanga nanga nanga kolelangaaaaa mwana mama aaaah mwana maaaama aaaaah....sijui inaitwaje hiii
Sent using Jamii Forums mobile app
Anajua sana kuichezea sauti yake, pia anajua kuwapangalia vijana wake, check ngoma kama Respect, Monde arabe, Gilba, Biblia, ........Inaitwa Maggie, ilikuwa ni moja ya hit song iliyofanywa na Koffi Papaa Mopao akishirikiana na kundi lake la Quartier Latin na ndo ilibeba jina la album iliyotoka 1994.
Koffi ni moja ya wasanii ninao wahusudu sana ktk anga za music duniani. Tangu nipo vidudu (nursery) mpaka leo hii nipo kazini huyu mzee bado anatoa pini tu na zote ni moto!!!
Sent using Jamii Forums mobile app