Kombe la Lowassa linavyofana Monduli!

Kombe la Lowassa linavyofana Monduli!

Joined
Mar 6, 2010
Posts
74
Reaction score
2
VIJANA wa jamii ya kifugaji kote nchini, wanapaswa kuungwa mkono katika suala la kuendelezwa kisoka, kwani kwa kufanya hivyo kutawafanya wajitume zaidi na kuacha fikira potofu kuwa wametengwa katika michezo.

Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Iddi Kipingu wakati wa ufunguzi wa mashindano ya kuwania Kombe la Lowassa mjini Monduli juzi.

Kipingu alisema kitendo cha Mbunge wa Monduli Edward Lowassa kuanzisha Kombe hilo ni kutaka kuona vijana wa jamii ya Kimasai wanaachana na hisia kuwa wao hawawezi kucheza soka na badala yake wanapaswa kuchunga mifugo tu.

Alimsifu mbunge huyo kwa uamuzi wake wa kuanzisha timu ya wanawake, kwani ni wilaya ya pili hapa nchini kufanya hivyo ukiachilia mbali Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti huyo alisema vijana wa Monduli katika soka wanaweza kufanya vizuri kwani wana maumbile mazuri kimichezo kama ya watu wa Afrika Magharibi.

''Tunapaswa kumuunga mkono Lowassa kwa kufanya jambo hili, ili Taifa liwe na vijana wenye uwezo wa kisoka na vijana wa kifugaji waweze kujua kuwa taifa bado linawajali,''alisema Kipingu.

Naye Lowassa alisema lengo la kuanzisha Kombe hilo miaka kumi iliyopita ni kutaka kuona vijana wanashiriki vyema michezo na kuacha tabia ya kujiingiza katika mambo yasiyokuwa na maana.

Lowassa alisema mwaka huu zawadi na gharama za mashindano zitatangazwa hapo baadaye.

Mwaka jana mashindano hayo yaligharimu zaidi ya Sh milioni 66, vijana wawili walioonesha uwezo mkubwa katika soka waliteuliwa kwenda kuona Kombe la Dunia litakalofanyika Afrika Kusini kuanzia Juni mwaka huu.

Mbali ya vijana hao, ambao ni Achi Ngomelo na Kayai Alfred, pia Katibu wa Chama cha Soka Wilaya ya Monduli, Ndauka Njelekele naye atakuwa miongoni mwa wanamichezo watakaoenda kushuhudia fainali hizo za Kombe la Dunia .

Katika mashindano ya mwaka huu, timu 25 zitashiriki kuwania Kombe la Lowassa na timu zote zimepewa seti moja ya jezi na mipira miwili.

Katika mchezo wa ufunguzi juzi, timu ya soka ya wanawake ya Kinondoni kama wageni waalikwa iliifunga timu ya wanawake ya Monduli mabao 2-1 katika mchezo wa aina yake uliochezwa Uwanja wa Bomani Monduli.
 
Asante Major Mkandala kutuhabarisha habari hii.Jana nilishuhudia kupitia Channel Ten (inamilikiwa na RA na Tanil) jinsi ufunguzi ilivyofana.Pia nampongeza mshauri wa EL katika suala zima za kujisafisha kwani nyingi njia alizoakitumia, zilikuwa kujaribu kunawa kwa kutumia maji taka, ila hii ya kupitia michezo, tena kupeleka vijana kushuhudia kombe la dunia, kwa kweli this time atawin, atasafishika, na atangara na kumeremeta ready for kombe la Dunia 2014 na kumalizia kombe kuu la nchi la 2015!.
 
Nadhani kwa njia hii, sasa atatakata tu, mpende msipended!!!! Lets give it time!!
 
Amefulia tu hata afanyeje-----------snake is a snake, hawezi badilika akawa Dynasour or Acmes, better go to his hell
 
Kaniki hata ukiisafisha kwa sabuni ya aina gani haiwezi kuwa nyeupe bali itabaki nyeusi tu. Huyu hawezi kujisafisha kwa kuanzisha michezo bali akatubie dhambi zake kwa mola wake kwa ufisadi wake.
 
wachezaji bora wa mashindano wanapelekwa kuangalia mechi za kombe la dunia, baada ya hapo..wakafie mbele??
Mikakati gani imeandaliwa baada ya hapo? najua yeye lengo lake litakuwa limetimia!
 
Kaniki hata ukiisafisha kwa sabuni ya aina gani haiwezi kuwa nyeupe bali itabaki nyeusi tu. Huyu hawezi kujisafisha kwa kuanzisha michezo bali akatubie dhambi zake kwa mola wake kwa ufisadi wake.

pumbavu
 
Edward lowassa atabaki kuwa lowassa

mpaka atakapoingia ikulu 2015 ndipo mtajua yeye ni nani

kidumu chama cha mapinduzi;;mambo ya kuchafuana ya kizamani

hata achafuliwe vipi atabaki lowassa mtamjua vizuri uwanja wa taifa 01nov 2015
 
Edward lowassa atabaki kuwa lowassa

mpaka atakapoingia ikulu 2015 ndipo mtajua yeye ni nani

kidumu chama cha mapinduzi;;mambo ya kuchafuana ya kizamani

hata achafuliwe vipi atabaki lowassa mtamjua vizuri uwanja wa taifa 01nov 2015


Mkuu umeahidiwa ka uwaziri hiyo 2015?mana duh naona umekua mkali ghafla.
 
ukitaka kupoteza maisha nenda monduli hata umkashifu lowassa kwenye kiduka ukisimama kunywa soda, this guy anapendwa uko monduli cjapata ona, watch out next election atashinda kwa kishindo kuliko wabunge wote tz! wananchi wake kawaletea maendeleo mengi sana hata ukiwa unajenga ukafikisha nyumba kwenye rinta wakimfata anawapa mabati na mbao za kupaulia uo ni mfano mdogo tu, suala izo ela zimetoka wapi is another matter altogether lakini wananchi wake hawawezi jali maadam wanapata matunda, si kama uyu muhindi mohamed dewji kule singida, kinadharia ameleta maendeleo mengi tu jimboni matrekta, shule, visima tena kwa pesa zake binafsi lakini mwisho wa siku chanzo cha izo ela ni wapi? je wananchi wanaweza kumbadilikia mbunge aliyeleta maendeleo jimboni kwa pesa chafu, na ambazo ufisadi au wizi huo hajaufanyia jimboni apo?
 
ukitaka kupoteza maisha nenda monduli hata umkashifu lowassa kwenye kiduka ukisimama kunywa soda, this guy anapendwa uko monduli cjapata ona, watch out next election atashinda kwa kishindo kuliko wabunge wote tz! wananchi wake kawaletea maendeleo mengi sana hata ukiwa unajenga ukafikisha nyumba kwenye rinta wakimfata anawapa mabati na mbao za kupaulia uo ni mfano mdogo tu, suala izo ela zimetoka wapi is another matter altogether lakini wananchi wake hawawezi jali maadam wanapata matunda, si kama uyu muhindi mohamed dewji kule singida, kinadharia ameleta maendeleo mengi tu jimboni matrekta, shule, visima tena kwa pesa zake binafsi lakini mwisho wa siku chanzo cha izo ela ni wapi? je wananchi wanaweza kumbadilikia mbunge aliyeleta maendeleo jimboni kwa pesa chafu, na ambazo ufisadi au wizi huo hajaufanyia jimboni apo?

Mkuu u got a big point hapa. Watu wengi pengine hawajaliona hili kwamba Mbunge anaweza kuwa kaleta maendeleo makubwa sana kutokana na sources zake za fund. The fact kwamba hizo funds source ni chafu au funds ni chafu mara nyingi sio concern ya wananchi...kama ulivyosema mtu kaezekewa paa la nyumba yake how come atamuona huyo Mbunge mbaya hata umchome sindano ya kumwona hivyo! Hawezi kabisa...

Kwa hiyo swala ni kudeal na mifumo yetu kuhakikisha watu kama hao (wenye fedha chafu) hawazipati au kuwadhibiti as soon as wanajulikana. So hamna haja ya kuwalaumu wananchi wanaoneemeka na fedha ambazo sie ndo tunaziona chafu.
 
thats the only option he is having. Afanyaje sasa!
 
Back
Top Bottom