Kondakta na Utingo wa Basi la Abood wakamatwa kwa kusafirisha bangi kwenye basi Mbeya

Kondakta na Utingo wa Basi la Abood wakamatwa kwa kusafirisha bangi kwenye basi Mbeya

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-12-06 at 13.35.50_3ca0a2dc.jpg

WhatsApp Image 2024-12-06 at 13.35.50_56ae21f2.jpg
Katika kipindi cha mwezi Novemba, 2024 jumla ya watuhumiwa wa makosa 97 wa makosa ya mauaji, kujeruhi, kupatikana na dawa za kulevya, kuingia nchini bila kibali na kupatikana na silaha bila kibali walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya kutokana na oparesheni na misako.

Novemba 21, 2024 huko katika kizuizi cha Polisi [Police Check Point) kilichopo mpakani Kijiji cha Igawa wilaya ya Mbarali, Jeshi la Polisi liliwakamata Shamim Maxwell [37] na Itika Bugale [36] wote wakazi wa Uyole Jijini Mbeya wakiwa na dawa za kulevya aina ya Bhangi Kilogramu 33.5

Watuhumiwa walikamatwa wakiwa wanasafirisha bhangi hiyo wakitokea Uyole kuelekea Dar es Salaam wakiwa abiria kwenye Gari yenye namba za usajili T.792 EDR Zhongtong Bus mali ya kampuni ya Achimwene.

Watuhumiwa walitumia mbinu ya kuficha dawa hizo za kulevya kwenye mabegi mawili ambayo ndani yake yalikuwa na nguo na walibainika baada ya kufanyika ukaguzi.

Wakati huo huo, Novemba 21, 2024 huko katika kizuizi cha Polisi kilichopo mpakani Kijiji cha Igawa Wilaya ya Mbarali, katika ukaguzi wa magari, Jeshi la Polisi lilifanikiwa kumkamata Kondakta wa Basi la Abood aitwaye Erick Patrick Mathew [46] na Tingo wa Basi hilo aitwaye Stanslaus Medson Nyagawa wakisafirisha dawa za kulevya aina ya Bhangi zenye uzito wa kilogramu 20.

Watuhumiwa walikuwa wakisafirisha dawa hizo kwenye Basi la Abood lenye namba za usajili T.823 DXJ Youtong wakitokea Mkoa wa Songwe kuelekea Dar es Salaam ambapo walificha dawa hizo kwenye mifuko miwili mikubwa ya sandarusi.


Sambamba na hayo, Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Askari wa TANAPA likiwa katika doria ndani ya hifadhi ya Taifa ya Ruaha, linamshikilia Adam Bandari Katani [58] mkazi wa Chunya kwa tuhuma za kupatikana na silaha aina ya Gobore bila kuwa na kibali cha kumiliki silaha hiyo.

Mtuhumiwa alikutwa na vipande 30 vya chuma ambavyo huvitumia kama risasi katika silaha hiyo, Unga wa baruti ukiwa kwenye kopo, Fataki 5 na vipande 7 vya nyama ya mnyama pori aina ya pimbi bila kuwa na kibali. Mtuhumiwa amekuwa akijihusisha na matukio ya uwindaji haramu ndani ya hifadhi ya taifa ya Ruaha.
WhatsApp Image 2024-12-06 at 13.39.51_f8268449.jpg

WhatsApp Image 2024-12-06 at 13.41.00_ac82e30e.jpg
 
Ndio wameuza kesi hapo wanasubiri mgao wao maana hapo zinaenda kutoka Hela hakuna kesi inayoenda mahakamani hapo zote zinaisha juu kwa juu
Hatari sana mkuu, Biashara kama hizo umakini Unahitajika sana, hasa Ratiba za usafiri( yani usijulikane kabisa kama unasafiri siku gani, ) 😊😊😊
 
Back
Top Bottom