Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Lenye lengo la kupokea maoni kuhusu maboresho mbalimbali ya tozo na ada kuelekea uandaaji wa bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2023/24
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema maendeleo yoyote Nchini lazima yawe na uhusiano wa moja kwa moja na kodi
Amesema “Kwa Nchi zenye hali mbaya, zile za mwisho kwenye umasikini ambazo hazina vyanzo vya kodi vyenyewe ndio wanaweza kutegemea vyanzo vingine kama misaada, lakini Nchi ambazo zimeshaendelea kama ya kwetu hata ukikopeshwa malipo yake yatatokana na kodi.
“Ili uonekane unakopesheka, unapimwa kama unaweza kukusanya kodi, kipimo kikubwa ni kuona makusanyo yako kama yanaweza kurejesha deni.”
Aidha, amewataka watendaji wa Serikali kubadilisha mtazamo wa ukusanyaji wa kodi kwa kuwaheshimu watu wanaowekeza kiuzalishaji ili walipe kodi.
Ameyasema hayo leo Januari 11, 2023 jijini Dar es Salaam katika kongamano la kodi kitaifa.
Mwigulu: Vijana milioni 1 wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema soko la ajira linatakiwa kuboreshwa katika sekta binafsi kwa kuwa kuna vijana wengi wanaoingia kwenye la ajira kutoka shuleni na vyuoni ambapo Serikali haina uwezo wa kuajiri wote.
Amesema “Kuna wanaohitimu darasa la 7 na hawaendelei sekondari, wapo wanaohitimu kidato cha nne, cha 6 na hawaendeleo, pia wapo wahitimu wa vyuo vya kati na vyuo vikuu, jumla kwa mwaka ni milioni 1 na wanaingia kwenye soko kutafuta ajira.”
Ameeleza kwa idadi ya taasisi za Serikali, Wizara, Halmashauri idadi hiyo haitoshi na wanahitaji sekta binafsi iliyo imara kuweza kuhakikisha watu wote hao wanakuwa kazini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema maendeleo yoyote Nchini lazima yawe na uhusiano wa moja kwa moja na kodi
Amesema “Kwa Nchi zenye hali mbaya, zile za mwisho kwenye umasikini ambazo hazina vyanzo vya kodi vyenyewe ndio wanaweza kutegemea vyanzo vingine kama misaada, lakini Nchi ambazo zimeshaendelea kama ya kwetu hata ukikopeshwa malipo yake yatatokana na kodi.
“Ili uonekane unakopesheka, unapimwa kama unaweza kukusanya kodi, kipimo kikubwa ni kuona makusanyo yako kama yanaweza kurejesha deni.”
Aidha, amewataka watendaji wa Serikali kubadilisha mtazamo wa ukusanyaji wa kodi kwa kuwaheshimu watu wanaowekeza kiuzalishaji ili walipe kodi.
Ameyasema hayo leo Januari 11, 2023 jijini Dar es Salaam katika kongamano la kodi kitaifa.
Mwigulu: Vijana milioni 1 wanaingia kwenye soko la ajira kila mwaka
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba amesema soko la ajira linatakiwa kuboreshwa katika sekta binafsi kwa kuwa kuna vijana wengi wanaoingia kwenye la ajira kutoka shuleni na vyuoni ambapo Serikali haina uwezo wa kuajiri wote.
Amesema “Kuna wanaohitimu darasa la 7 na hawaendelei sekondari, wapo wanaohitimu kidato cha nne, cha 6 na hawaendeleo, pia wapo wahitimu wa vyuo vya kati na vyuo vikuu, jumla kwa mwaka ni milioni 1 na wanaingia kwenye soko kutafuta ajira.”
Ameeleza kwa idadi ya taasisi za Serikali, Wizara, Halmashauri idadi hiyo haitoshi na wanahitaji sekta binafsi iliyo imara kuweza kuhakikisha watu wote hao wanakuwa kazini.