Korea kama hauna degree haupewi mke, Ifike mahala kama hauna degree usigombee ubunge

Msingi wa CCM ni ujinga. Ujinga ukiondoka, hawawezi kutawala.
 
Nikikuuliza degree ni mdudu gani? Wenye hizo degrees ndiyo wanataka kuifanya Tanzania iwe ya wakimbizi.

Wanawazia pesa zilizo mfukoni kwa mtu mwingine. Kula degree yako.
 
Hiwe hawe Γ—Γ—Γ—Γ—Γ— iwe na awe sasa kama mtoa mada mwenyewe unaandika hivyo Korea ungepewa mke kweli
 
Kuna msomi anajua kugeuza mchanga/ udongo kuwa mashine?

Nchi hii wanaolisha chakula kwa kulima karibia wote ni elimu la saba au chini ya hapo na wachache form iv.

Wanakula rushwa na kuiingiza nchi katika mikataba mibovu ni darasa la saba?

Uzalendo ndio muarubaini wa kweli utakaowezesha kuchangia nchi isonge mbele sio mtu kuwa amekaa darasani muda mrefu tu.

Ubaguzi wa aina yeyote hautakiwi kinachotakiwa ni uchaguzi huru na wa haki tu ili kila anayedhani anaweza awe msomi, hajasoma, kijana, mzee, mwanamke au mwanamme aweze kugombea na iwe juu ya wapiga kura kuamua.
 
Hiwe hawe Γ—Γ—Γ—Γ—Γ— iwe na awe sasa kama mtoa mada mwenyewe unaandika hivyo Korea ungepewa mke kweli
😁😁😁😁 Uzuri hawaangalii degree za kiswahili.Kiswahili nilijifunza nilipokuwa narudi Tz likizo.
 
Katiba ndivyo inavyotaka. Lakini 2020 haikua hivyo, chama cha kijani tangu kwenye kura za maoni, kiliamua nani awe mbunge, maamuzi hayakua ya wananchi. Tena to be precisely, Mwenyekiti wao ndiye alikua final.
Yaa hapo ndo penye shida, ila ile haki ya kuchagua na kuchaguliwa hata huyu wa darasa la saba anayo......ila mchakato mzima unatakiwa kuwa huru na haki, siyo kama uchafuzi tulioshuhudia 2020. Kadri jamii nzima inavyoendelea kupata elimu na maarifa ya juu zaidi itafikia kipindi wananchi wengi watazingatia elimu kama sifa muhimu kuweza kukupa kura uwe mbunge wao. Ni mchakato tu unaoweza kuwaengua hawa wa darasa la saba nafikiri wanayo haki ya kuomba kuchaguliwa hata nafasi ya urais.
 
Bill Gates hana degree lakini ni tajiri na anaongoza kampuni kubwa duniani.
Watu mmekariri mkipata degree ndio mmemaliza kila kitu wakati wengine wanatumia degree zao kuleta tija .
Kwa hoja yako nina wasiwasi na degree yako kama haijaangukia degree za chupi au zinazofanana na hizo.
 
Kwa hiyo hapo ndio umechangia mawazo yako teyari na wewe?inaonyesha jinsi gani ulivyo mjinga.
 
Korea wana haki ya kufanya hivyo.
Lakini pia hili la wabunge kuwa na degree naliunga mkono ila wasiwasi wangu ni kwamba wabunge wengi watakuwa vijana na vijana wamezingua sana hapo kati. Imeonyesha vijana wapo too ambitious,, wana urahisi wa kuwa wajinga na kukiuka wanacho kiamini.
 
Korea wao mtu kama hana degree hawezi kupata mke sisi huku darasa la saba m bunge wakati wasomi wapo wengi .
Umechanganya maembe na machungwa: Haki ya kuoa na haki ya kufanya siasa katika nafasi ya ubunge haitokani na aina ya genitalia aliyo nayo na jinsi anavyoitumia.

Itikadi ya genitalism inasemakuwa mtu anakuwa na haki kwa sababu ya aina ya genitalia aliyo nayo na jinsi anavyoitumia. Ni itikadi ya hovyo.

Badala yake haki zinaanzia kwenye uwezo kufikiri, kuhukumu na kutekeleza maamuzi sahihi --merit.

Mengine ni nyongeza.
 
Pia tunaomba JF waongeze kigezo cha kujua kuandika na kusoma kwa kila atakaetoa uzi.
 
nina wasiwasi hata mtoa mada kama ana degree maana vitu alivyoandika havifanani na degree anatufanya watu wote uelewa wetu ni mdogo.
 
Yaani Mke mpaka upewe na sio makubaliano baina ya hao wawili (kweli unaweza kuona watu wameendelea ila kumbe wameendelea kurudi nyuma na sio kwenda mbele)

Mbunge ni mwakilishi wa watu wake sasa kama hao watu wanaona anawawakilisha vyema na ndivyo iwe.... (Ni Choice ya Wapiga Kura wenyewe)
 
Kama wabunge wenye PhD tu ni uozo wa kutupa huko bungeni, ni bora wa darasa la saba wawe wengi tena sanaaaa.
 
Degree is useless, character is everything.... character makes a person, kama unafikiri ni rahis hivyo nenda na wewe kagombee.. shida ni hawa alfa ulela wa CCM wasiojua chochote na waliteuliwa ba mwendazake kwa mkono wa chuma...

Bora ungekuwa mkono wa nyama.
 
Labda mtaala urekebishwe kwanza sio kwa elimu yetu hii ambayo maprofesa wenyewe hamna kitu. Wasomi wanajipendekeza kwa kiongozi wajuu na kuzisaliti taaluma zao utadhani walispecialize kwenye masomo ya kulamba viatu na sendo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…