FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Habari!
Marekani imeiondolea Korea Kusini vizuizi ama ukipenda waweza kuita vikwazo vya muda mrefu (miaka 42) juu ya uwezo wake wa kutengeneza makombora. Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in alitangaza uamuzi huo Ijumaa kufuatia mkutano wake na Rais wa Marekani Joe Biden hivi karibuni jijini Washington.
Vizuizi vya Marekani hapo awali viliweka ukomo kwa Korea Kusini kuendeleza au kuwa na makombora yenye masafa zaidi ya kilometa 800 sawa na maili takribani 497.
Mnamo mwaka 1979, Korea Kusini iliingia katika makubaliano ya kuweka kikomo cha makombora cha kilometa 180 sawa na maili 112 kama sharti maalumu ili iweze kupatiwa teknolojia ya utengenezaji makombora kutoka Marekani.
Kutokana na kuongezeka kwa vitisho vya kiusalama kutoka Korea Kaskazini, miongozo ya makubaliano hayo imerekebishwa mara nne mpaka sasa. Marekebisho ya 1997 yaliiruhusu Korea Kusini kutengeneza kombora la balistiki lililokuwa na uwezo wa kubeba silaha (warhead) ya kilo 500, lenye uwezo wa kusafiri kwa umbali wa hadi kilometa 300.
Marekebisho mengine yalifanywa mnamo mwaka 2012 ambayo yaliongeza uwezo wa makombora ya balistiki hadi kilometa 800 (sawa na maili 497) na uzito wa silaha wa kilo 500.
Kufuatia jaribio la sita la nyuklia la Pyongyang (Korea Kaskazini) mnamo mwaka 2017, Korea Kusini na Marekani zilikubaliana kuondoa kikomo cha uzito wa silaha, na marekebisho mengine yalifanywa mnamo 2020 ili kuruhusu utengenezaji wa roketi za anga za mbali (solid-propellant space rockets).
Vikwazo ama vizuizi vyote sasa vimeondolewa rasmi baada ya miaka 42. Hii ina maana kuwa, Korea Kusini sasa inaweza kutengeneza makombora ya balistiki yasiyo na kikomo cha uzito wa silaha na yenye uwezo wa kuzifikia shabaha za mbali zaidi ya Rasi ya Korea.
Matarajio ya wengi (nikiwemo mimi) ni kuamshwa kwa mashindano makubwa ya silaha hususani makombora ya balistiki katika Rasi ya Korea. Uwezo wa kiuchumi na kiteknolojia wa nchi ya Korea Kusini hivi sasa unatosha kwa kiasi kikubwa kuiwezesha nchi hiyo kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya makombora.
Pia, hii inatazamwa na baadhi ya wachambuzi kama njia mojawapo ama hatua ya Marekani kama sehemu ya mkakati wa kukabiliana na mataifa kama China katika eneo hilo kupitia mshirika wake, Korea Kusini.
Waweza kuisoma taarifa hii [kwa ukamilifu wake] kupitia vyanzo vifuatavyo:
1. Defense News | US lifts missile restrictions on South Korea, ending range and warhead limits
2. The Korea Times | Seoul's 'missile sovereignty' comes as double-edged sword
3. The Defense Post | US, South Korea scrap bilateral missile guidelines
Marekani imeiondolea Korea Kusini vizuizi ama ukipenda waweza kuita vikwazo vya muda mrefu (miaka 42) juu ya uwezo wake wa kutengeneza makombora. Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in alitangaza uamuzi huo Ijumaa kufuatia mkutano wake na Rais wa Marekani Joe Biden hivi karibuni jijini Washington.
Vizuizi vya Marekani hapo awali viliweka ukomo kwa Korea Kusini kuendeleza au kuwa na makombora yenye masafa zaidi ya kilometa 800 sawa na maili takribani 497.
Mnamo mwaka 1979, Korea Kusini iliingia katika makubaliano ya kuweka kikomo cha makombora cha kilometa 180 sawa na maili 112 kama sharti maalumu ili iweze kupatiwa teknolojia ya utengenezaji makombora kutoka Marekani.
Kutokana na kuongezeka kwa vitisho vya kiusalama kutoka Korea Kaskazini, miongozo ya makubaliano hayo imerekebishwa mara nne mpaka sasa. Marekebisho ya 1997 yaliiruhusu Korea Kusini kutengeneza kombora la balistiki lililokuwa na uwezo wa kubeba silaha (warhead) ya kilo 500, lenye uwezo wa kusafiri kwa umbali wa hadi kilometa 300.
Marekebisho mengine yalifanywa mnamo mwaka 2012 ambayo yaliongeza uwezo wa makombora ya balistiki hadi kilometa 800 (sawa na maili 497) na uzito wa silaha wa kilo 500.
Kufuatia jaribio la sita la nyuklia la Pyongyang (Korea Kaskazini) mnamo mwaka 2017, Korea Kusini na Marekani zilikubaliana kuondoa kikomo cha uzito wa silaha, na marekebisho mengine yalifanywa mnamo 2020 ili kuruhusu utengenezaji wa roketi za anga za mbali (solid-propellant space rockets).
Vikwazo ama vizuizi vyote sasa vimeondolewa rasmi baada ya miaka 42. Hii ina maana kuwa, Korea Kusini sasa inaweza kutengeneza makombora ya balistiki yasiyo na kikomo cha uzito wa silaha na yenye uwezo wa kuzifikia shabaha za mbali zaidi ya Rasi ya Korea.
Matarajio ya wengi (nikiwemo mimi) ni kuamshwa kwa mashindano makubwa ya silaha hususani makombora ya balistiki katika Rasi ya Korea. Uwezo wa kiuchumi na kiteknolojia wa nchi ya Korea Kusini hivi sasa unatosha kwa kiasi kikubwa kuiwezesha nchi hiyo kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya makombora.
Pia, hii inatazamwa na baadhi ya wachambuzi kama njia mojawapo ama hatua ya Marekani kama sehemu ya mkakati wa kukabiliana na mataifa kama China katika eneo hilo kupitia mshirika wake, Korea Kusini.
Waweza kuisoma taarifa hii [kwa ukamilifu wake] kupitia vyanzo vifuatavyo:
1. Defense News | US lifts missile restrictions on South Korea, ending range and warhead limits
2. The Korea Times | Seoul's 'missile sovereignty' comes as double-edged sword
3. The Defense Post | US, South Korea scrap bilateral missile guidelines