Korea,Taiwan,Germany,Japan mmepata funzo kwa Ukraine

Korea,Taiwan,Germany,Japan mmepata funzo kwa Ukraine

LICHADI

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2015
Posts
4,491
Reaction score
12,560
Kwa sasa hawa watu watakuwa washapata funzo kwa ukraine kuwa marekani ni wa kumkimbia na ni muda wa kuanza kujipanga kibabe maana wakija kuvamiwa hakuna cha bure

Marekani alimzuia Japan,Ujerumani,Korea,Taiwan kumiliki nuke akiwaahidi kuwalinda hata Ukraine yenyewe ilikuwa na Nuke ikakubali ushauri wa Marekani kuyaangamiza hayo mabomu kwa ahadi kuwa italindwa na haitovamiwa na Urusi leo hii Ukraine imevamiwa walioahidi kumlinda na kumwambia asalimishe nuke zake wanamwambia agawe ardhi wavune madini hamna cha bure

Taiwan ni muda muafaka aanze kukaa vizuri na ndugu yake China ajue kabisa akiingia vitani na china ,Marekani atamgeuka hapo.hapo kuwa anunue silaha au atoe aina fulani ya dhamana ili alindwe inshort Marekani hana cha bure

Japan nae ni mbabe sema kafungwa mikono ila siku na yeye akija kuvamiwa atageukwa hivyo hivyo

South Korea nae ni muda muafaka akae na Ndugu zake wa North wapatane ikija kuzuka vita hapo Korea ,South ajue atapewa mikataba migumu na Marekani ili alindwe yaani nachokiona wamarekani wanamtengenezea mtu mtego aingie ili wavune pesa kupitia vita na maligafi ulizo nazo

Germany nayo baada ya vita kuu ya pili ya Dunia iliwekwa under control kuwa hakuna ruhusa ya kumiliki nuke ,yaani na yeye aliahidiwa kulindwa ila ni muda muafaka waanze kujipanga upya
 
Back
Top Bottom