Korti yamwachia mtoto wa Keenja

Korti yamwachia mtoto wa Keenja

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
USIOMBE YAKUKUTE WE KAPUKU
SEGEDANC YAKO

Korti yamwachia mtoto wa Keenja

na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana ilimwachiria huru mtoto wa mbunge wa Jimbo la Ubungo, Charles Keenja, Eliasa Keenja, na wenzake watatu baada ya kuwaona hawana kesi ya kujibu.

Mbali na Keenja washtakiwa wengine waliofutiwa kesi ni Ahmed Mbilinga (Meneja wa NHC, Mkoa wa Tabora), Frola Nhamkolomwa na Damas Ngoiya ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 300.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa, alisema amefikia hatua ya kuwaachiria huru washtakiwa kwa sababu ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka umeshindwa kuishawishi mahakama kuwaona washtakiwa hao wana kesi ya kujibu.

Alisema ushahidi uliotolewa hauwezi kuwatia hatiani kwa kuwa hauonyeshi kama kweli washtakiwa hao walivunja nyumba ya mpangaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Li Jinglan, na kuiba vitu hivyo.

Awali, washtakiwa hao walidaiwa kuwa Mei 9, 2006, katika eneo la Kinondoni, Dar es Salaam, waliingia kwenye nyumba ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) anamoishi, Li Jinglan, na kuiba vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 300.
 
Ningependa kumpongeza Eliasa Keenja kwa kuachiwa huru na mahakama katika kesi hiyo,kwa ajili ilikosa ushahidi.
Nafurahi sana ninaposikia mtoto wa Mbunge Keenja akiachiwa huru,kwa sababu Mbunge Keenja ndiye aliyejenga barabara hizo nzuri za Dar es Salaam,[jambo ambalo lilitufanya wengi tusiamini macho yetu,yaani,uzuri wa barabara],lakini Keenja angegombea Ubunge Mbagala,asingeshinda,kwa sababu barabara zake hazikufika Mbagala.
 
Nafurahi sana ninaposikia mtoto wa Mbunge Keenja akiachiwa huru,kwa sababu Mbunge Keenja ndiye aliyejenga barabara hizo nzuri za Dar es Salaam,[jambo ambalo lilitufanya wengi tusiamini macho yetu,yaani,uzuri wa barabara],lakini Keenja angegombea Ubunge Mbagala,asingeshinda,kwa sababu barabara zake hazikufika Mbagala.


NI HATARI PALE UNAPOAMUA KUTEMBEA UCHI UNAKUTA NA MKWEO...USIOMBE HILO
 
Ningependa kumpongeza Eliasa Keenja kwa kuachiwa huru na mahakama katika kesi hiyo,kwa ajili ilikosa ushahidi.
Nafurahi sana ninaposikia mtoto wa Mbunge Keenja akiachiwa huru,kwa sababu Mbunge Keenja ndiye aliyejenga barabara hizo nzuri za Dar es Salaam,[jambo ambalo lilitufanya wengi tusiamini macho yetu,yaani,uzuri wa barabara],lakini Keenja angegombea Ubunge Mbagala,asingeshinda,kwa sababu barabara zake hazikufika Mbagala.

what kind of thinking is this?
 
what kind of thinking is this?

KIGOGO USSIMLAUMU KWANZA INATEGEMEA NA SHULE ALIPOSOMA@@#
 
what kind of thinking is this?

KIGOGO USSIMLAUMU KWANZA INATEGEMEA NA SHULE ALIPOSOMA@@#

asante sana umetuliza hasira zangu..yaani watu wengine wana thinking ya ajabu kabisa
 
Hakika pongezi hizi nzito si bila sababu .Tutacgunguza tujue
 
Ningependa kumpongeza Eliasa Keenja kwa kuachiwa huru na mahakama katika kesi hiyo,kwa ajili ilikosa ushahidi.
Nafurahi sana ninaposikia mtoto wa Mbunge Keenja akiachiwa huru,kwa sababu Mbunge Keenja ndiye aliyejenga barabara hizo nzuri za Dar es Salaam,[jambo ambalo lilitufanya wengi tusiamini macho yetu,yaani,uzuri wa barabara],lakini Keenja angegombea Ubunge Mbagala,asingeshinda,kwa sababu barabara zake hazikufika Mbagala.

Keenja ana barabara "zake"?
 
Ningependa kumpongeza Eliasa Keenja kwa kuachiwa huru na mahakama katika kesi hiyo,kwa ajili ilikosa ushahidi.
Nafurahi sana ninaposikia mtoto wa Mbunge Keenja akiachiwa huru,kwa sababu Mbunge Keenja ndiye aliyejenga barabara hizo nzuri za Dar es Salaam,[jambo ambalo lilitufanya wengi tusiamini macho yetu,yaani,uzuri wa barabara],lakini Keenja angegombea Ubunge Mbagala,asingeshinda,kwa sababu barabara zake hazikufika Mbagala.
Mkuu, sijui angewezaje kufanya kila kitu kwa miaka miwili na nusu tu. Alijitahidi kibinadamu.
 
USIOMBE YAKUKUTE WE KAPUKU
SEGEDANC YAKO

Korti yamwachia mtoto wa Keenja

na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, jana ilimwachiria huru mtoto wa mbunge wa Jimbo la Ubungo, Charles Keenja, Eliasa Keenja, na wenzake watatu baada ya kuwaona hawana kesi ya kujibu.

Mbali na Keenja washtakiwa wengine waliofutiwa kesi ni Ahmed Mbilinga (Meneja wa NHC, Mkoa wa Tabora), Frola Nhamkolomwa na Damas Ngoiya ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 300.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa, alisema amefikia hatua ya kuwaachiria huru washtakiwa kwa sababu ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka umeshindwa kuishawishi mahakama kuwaona washtakiwa hao wana kesi ya kujibu.

Alisema ushahidi uliotolewa hauwezi kuwatia hatiani kwa kuwa hauonyeshi kama kweli washtakiwa hao walivunja nyumba ya mpangaji wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Li Jinglan, na kuiba vitu hivyo.

Awali, washtakiwa hao walidaiwa kuwa Mei 9, 2006, katika eneo la Kinondoni, Dar es Salaam, waliingia kwenye nyumba ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) anamoishi, Li Jinglan, na kuiba vitu mbalimbali vyenye thamani ya sh milioni 300.
Hawa majizi kwa sasa wanakula mafao na kutakatisha pesa walizokwapua miaka hiyo...only in tanzania
 
Back
Top Bottom