Ku-socialize kazini ni muhimu kwa afya

Ku-socialize kazini ni muhimu kwa afya

Ukwelimtupu

Member
Joined
Nov 21, 2011
Posts
36
Reaction score
13
Je wajua ku socialize kazini ni muhimu sana kwa afya yako wewe mfanyakazi? Ku-socialize kazini na wafanyakazi wenzako kunakuondolea stress kwa kuufanya ubongo wako kuchangamka.

Hivyo wale wenye tabia ya kukaa kimya kazini na kuagiza lunch na kulia mezani au ofisini kwako inabidi WABADILIKE.

Nawatakieni Ijumaa Karim!
 
Unasocialize kazini wakati gani? Hiki ndicho kinaharibu utendaji na ufanisi wa ofisi za uma. Kutokujua kwamba muda wa kazi ni wa kufanya kazi ili kazi zikamilike kwa muda muafaka. Kupiga midomo muda wa kazi ni tatizo kubwa sana linalorudisha nyuma maendeleo na mafanikio ya taasisi husika.

Kusocialize ni muhimu lakini si muda wa kazi:-

Socialize wakati wa mapumziko ambapo hata kanuni zinatambua kwamba unahitaji break kwa afya ya mwili na akili.

Socialize baada ya muda wa kazi na ndiyo sababu kazi zina masaa maalumu,

Socialize nje ya kazi wakati wowote au mnapokuwa kwenye majumuiko na wafanyakazi wenziyo lakini si wakati wa kufanya kazi.

Tujizoeshe kutumia muda ipasavyo, na hautauona ugumu wa kazi, itapunguza majungu na uzembe makazini, itaboresha uwajibikaji na kuongeza uzalishaji na hivyo maslahi zaidi kwa namna moja ama nyingine.

Ahsante.


Je wajua ku socialize kazini ni muhimu sana kwa afya yako wewe mfanyakazi?
Ku socialize kazani na wafanyakazi wenzako kunakuondolea stress kwa kuufanya ubongo wako kuchangamka
Hivyo wale wenye tabia ya kukaa kimya kazini na kuagiza lunch na kulia mezani au ofisini kwako inabidi WABADILIKE.

NAWATAKIENI IJUMAA KARIM
 
Tabby nimefurahishwa na maboresho uliyoyatoa. Ni kweli kwamba ku socialize kazini kuna muda wake. Mfano wakati wa tea break au lunch time. Pia haifai watu ku socialize muda wa kazi. Kusudi langu la kuweka ujumbe huu ni kuwaasa watu kujenga mahusiano mazuri na wafanyakazi wenzao ili waweze kuepuka stress kazini. Ukweli ni kwamba ku socialize kazini kunategemea mind-set ya mtu mwenyewe, kuna wale hupenda kupiga soga muda wote na kuna wale ambao hu socialize muda mwafaka..mfano kabla ya saa mbili asubuhi au muda wa lunch...Chochote chenye manufaa chaweza kuwa na madhara kulingana na matumizi kwa mfano kuna wale wanaotumia WhatsApp kurushiana picha, video clips na message za kingono ngono na mambo ya kipuuzi muda wote( Brain cell killers). Pia kuna wale wanaotumia WhatsApp katika kujuzana habari za kujenga na mambo yenye manufaa. Kwa kifupi ku socialize chanya kuna manufaa kwa mfanyakazi.
 
Back
Top Bottom