Kuadimika kwa makuti ya kuezekea hasa

Kuadimika kwa makuti ya kuezekea hasa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
1595042256048.jpeg

Makuti ni majani ya minazi yanayopatikana katika mikoa ya kando ya bahari hasa katika nchi za kitropiki. Makuti husukwa viungo na viungo hufungwa kwenye miti au mbao za nyumba ili kuzuia jus na mvua na kujistri.

Makuti hushurubu
joto la jua na kuifanya nyumba kuwa na nyuzi joto ya wastani hata kama nje ni jua kali la kiangazi. Kwa miaka mingi watu wa kipato chachini hata katika mimi mikubwa ya Pwani walitumia makuti katika ujenzi wa nyumba zao.

Ukitaka kuepuka gharama za Air Condition hasa kipindupindu cha kiangazi unaweza kujenga kibanda nyuma ya nyumba na kuezeka paa la makuti. Unaweza kuweka bustani nje au bwawa la kuogelea, ndani ukaweka viti, meza hata TV na fridge ya vinywaji. Sehemu hii ikawa ya kupumzika mchana.

Tatizo kubwa ni uhaba wa viungo na makuti uanojitokea siku hizi. Ni kuwa watu wengi wameacha kilimo cha minazi?
 
Makuti ni majani au magamba ya mgomba ambayo tunatumia kule Tukuyu, bukoba na Moshi kuuzekea nyumba
 
mikoa ya kandidaat ya bahari


Hiyo ni mikoa ya pwani,

Ala kulli hali, kuna makuti ya mnazi, makuti ya mgomba, makuti ya mchikichi (kiangalala cha mgazi) nk,

Makuti ya mnazi na mgomba hutumika kuezekea, makuti ya mnazi na mchikichi pia hutumika kutengenezea fagio cha chelewa nk.

Kifupi makuti ya mnazi hayajaadimika isipokuwa watu siku hizi wanaenda na nyakati, angalia watu wengi siku hizi hawatumii fagio za chelewa kama zamani pia watu wanaezekea mabati na vifaa vingine hivyo hakuna mtu tena anayeona biashara ya makuti kama inalipa sasa yanini apoteze muda bila faida, hii ndiyo apparent reason unaweza kusema makuti ya mnazi yameadimika.
 
Hiyo ni mikoa ya pwani,

Ala kulli hali, kuna makuti ya mnazi, makuti ya mgomba, makuti ya mchikichi (kiangalala cha mgazi) nk,

Makuti ya mnazi na mgomba hutumika kuezekea, makuti ya mnazi na mchikichi pia hutumika kutengenezea fagio cha chelewa nk.

Kifupi makuti ya mnazi hayajaadimika isipokuwa watu siku hizi wanaenda na nyakati, angalia watu wengi siku hizi hawatumii fagio za chelewa kama zamani pia watu wanaezekea mabati na vifaa vingine hivyo hakuna mtu tena anayeona biashara ya makuti kama inalipa sasa yanini apoteze muda bila faida, hii ndiyo apparent reason unaweza kusema makuti ya mnazi yameadimika.
Makuti ya minazi bado yana soko sana kwa wamiliki wa mahoteli hasa kando ya bahari. Pamoja na hao tupo tunao yatumia katika vibanda vya kupumzikia.
 
Bado ninajenga kibanda cha kupumzikia kaka.
Hongera dada! Umaliziaji mwema wa kibanda chenye kupunguza gharama na athari za Ac. Lakini hata ukiyahitaji kwa ajili ya kuweka sehemu maalumu kule kwenye ile hotel usisite kunijuza ili nikuletee
 
Hiyo ni mikoa ya pwani,

Ala kulli hali, kuna makuti ya mnazi, makuti ya mgomba, makuti ya mchikichi (kiangalala cha mgazi) nk,

Makuti ya mnazi na mgomba hutumika kuezekea, makuti ya mnazi na mchikichi pia hutumika kutengenezea fagio cha chelewa nk.

Kifupi makuti ya mnazi hayajaadimika isipokuwa watu siku hizi wanaenda na nyakati, angalia watu wengi siku hizi hawatumii fagio za chelewa kama zamani pia watu wanaezekea mabati na vifaa vingine hivyo hakuna mtu tena anayeona biashara ya makuti kama inalipa sasa yanini apoteze muda bila faida, hii ndiyo apparent reason unaweza kusema makuti ya mnazi yameadimika.
makuti ya mnazi yameadimika wengi hupasua minazi kufanya mbao za kupaulia minaz mingi hasa kwa tanga ni sehem za madanga - pangani na watu wanaenda na wakati hakuna kuezekea makuti ni mabat
 
Back
Top Bottom