kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,634
- 7,015
Wazo la kuahirishwa kwa mechi bila shaka limetolewa na msomi wa chuo kikuu aloyeaminiwa kupewa kazi kwa usomi wake.Huyu hakuangalia maslahi ya washabiki amabao tangu saa moja asubuhi wameingia uwanjani.
Kama vile haitoshi,makosa yameshafanyika,kulikuwa bado na nafasi ya kupunguza maumivu,msomi mwingine kutoka club ya mpira,akaamua kuchagua matumizi ya kanuni badala ya busara.Bila kufikiri anayeumia si TFF,wala serikali,bali mashabiki ,na wengine wametoka mbali sana,akaamua kuonesha usomi wake kwa kusimamia kanuni.
Natamani hiyo kanuni isomwe kwa lugha ya kisheria.
Kuahirisha mechi ni sawa na kusogeza muda wa mechi mbele?
Kama kuahirisha mechi ni sawa na kusogeza mechi mbele, basi ninazidi kuamini wasomi wetu waliohusika kutengeneza hizi kanuni,wana haki ya kupokea hoja zote za mbunge wa Geita mh.Musukuma.
Tumeambiwa kuwa yalikuwa maelekezo ya wizara.Hao watu wa wizara wanasubiri nini kutoa taarifa.Au ndio mpaka jumatatu waingie ofisini?
Hizi elimu za kitanzania mbona huwa zipo kumkandamiza tu mtu mnyonge?
Kama vile haitoshi,makosa yameshafanyika,kulikuwa bado na nafasi ya kupunguza maumivu,msomi mwingine kutoka club ya mpira,akaamua kuchagua matumizi ya kanuni badala ya busara.Bila kufikiri anayeumia si TFF,wala serikali,bali mashabiki ,na wengine wametoka mbali sana,akaamua kuonesha usomi wake kwa kusimamia kanuni.
Natamani hiyo kanuni isomwe kwa lugha ya kisheria.
Kuahirisha mechi ni sawa na kusogeza muda wa mechi mbele?
Kama kuahirisha mechi ni sawa na kusogeza mechi mbele, basi ninazidi kuamini wasomi wetu waliohusika kutengeneza hizi kanuni,wana haki ya kupokea hoja zote za mbunge wa Geita mh.Musukuma.
Tumeambiwa kuwa yalikuwa maelekezo ya wizara.Hao watu wa wizara wanasubiri nini kutoa taarifa.Au ndio mpaka jumatatu waingie ofisini?
Hizi elimu za kitanzania mbona huwa zipo kumkandamiza tu mtu mnyonge?