Kuahirishwa mara kwa mara kwa hukumu za kesi zinazogusa masikio ya wengi maana yake nini?

Inafuata hukumu ya kesi ndogo ya Mbowe nayo dalili zinaonesha wazi itaahirishwa.
 
Hawako huru Hawa!
 
Kwaiyo kama zinafatiliwa na wengi ndo mnataka mambo yaende mnavyotaka nyinyi sio?

Uwiano upoje kati ya izo kesi unazosema na zile ambazo hazifatiliwi na watu zipi zinaongoza kuahirishwa?

Je majaji wamevunja sheria?

Hii kwa lugha nzuri naweza kuiita mihemko
 
Yaani washitakiwe na akina Membe halafu lawama tupewe sisi !
Sabaya alishitakiwa na Membe?

Sabaya mlimwandama sana kwa kurusha video za uongo na kuandika barua nyingi za malalamiko ya wafanyabiashara wa hai kuporwa mali wakati mkijua sio kweli na aliyewasikiliza akaegemea kwenye 'emotional leadership' ambayo haitakiwi kuifanyia kazi kabla hujafikiri madhara baada ya uamuzi huo.

Kesi ya Sabaya alitakiwa aunganishwe waziri wa fedha na mipango pamoja na gavana wa benki kuu kwa kuwa walishawahi kumpongeza kwa kazi aliyotumwa kuifanikisha lakini leo eti anabandikwa kesi ya unyang'anyi na kutumia silaha pamoja na matumizi mabaya ya madaraka wakati waliopo madarakani sasa hivi walikuwepo na hawakujiuzulu kulinda heshima na maadili kwa kuona mabaya aliyokuwa anayafanya.

Mashitaka yote ya Mbowe, Sabaya, Musiba na wengineo matokeo yake yatawarudi waliozianzisha hizo kesi za visasi 'Karma is always a rolling ball, bouncing when it hits a rigid surface back to the exertion force'
 
Kama Sabaya hakupora hela za wafanyabiashara unadhani pongezi alizopata zilitokana na nini ? Halafu video zote za uvamizi na zingine zilizorekodiwa kwenye CCTV camera za mahoteli kadhaa Sabaya mwenyewe mbona hajawahi kuzikana , zaidi amedai alitumwa na Magufuli kufanya aliyoyafanya .

Wewe ni nani hadi upinge ?
 
Hujui kitu
 
Ni kama ambavyo DPP anatumia nafasi yake kuunda kesi bandia ili kutesa baadhi ya watu kwa manufaa ya kisiasa ndivyo hivyohivyo "baadhi ya mahakama zinatumika kuwa sehemu ya utesaji baadhi ya watuhumiwa ili kukidhi baadhi ya matakwa ya baadhi ya wenye mamlaka!"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…