Kuanzia Morogoro Road hadi Buguruni kuna foleni sana. Serikali fuateni ushauri huu

Kuanzia Morogoro Road hadi Buguruni kuna foleni sana. Serikali fuateni ushauri huu

Mgunda Jr

Member
Joined
Aug 11, 2013
Posts
9
Reaction score
18
Wakuu, hiki kipande cha Moro Road kwenda Mandela Road hadi Buguruni to Bandalili, ule utaratibu wa kuzuia malori asubuhi ungehamia pia jioni, labda kuanzia saa 9 au saa 10 hadi saa 1 au saa 2 jioni ndio yaruhusiwe.

Hii ingesaidia kidogo kupunguza malori hasa katika hizi peak hours, lakini pia kupunguza risk ya malori kuharibika na hali ya foleni kuwa mbaya zaidi.

Pia, ule mpango wa njia za mwendo kasi kulipia magari binafsi ambao Mh. Waziri Nashindwa alitaka kuanzisha wakati yupo Wizara ya Ujenzi sijui uliishia wapi. Naona pia ingesaidia kwa namna moja au nyingine, ni kuangalia tu organization yake ingekuaje.

Jiji la Dar lina accessibility kubwa ya kuwa na ring roads au peripheral roads ili kuweza kuyapeleka au kuyatawanya magari kwa urahisi kutoka katikati ya jiji.

Nashauri pia serikali iangalie mpango wa dharura kwa ajili ya hizi ring/peripheral roads, kwani zinasaidia sana hasa kwa ukuaji wa jiji na accessibility yake kwa kiwango kikubwa.


Nawalisha.
 
Kuna ulazima wa kufuta baadhi ya ruti kuelekea katikati ya mji

Kuna ulazima gan daladala zinazotoka Tabata Chang’ombe na maeneo jiran kuvuka kuja mjini kati?

Daladala ni nying sana njia panda ile
 
Back
Top Bottom