Kuanzisha biashara ndogo ya hifadhi ya nafaka je italipa? Nawaomba msaada wa ushauri wajasiriamali.

Kuanzisha biashara ndogo ya hifadhi ya nafaka je italipa? Nawaomba msaada wa ushauri wajasiriamali.

shoka mwitu

Member
Joined
Sep 30, 2013
Posts
7
Reaction score
0
Nina njozi ya kuanzisha hifadhi ya nafaka kama biashara ndogo hapa Arusha lakini sina ujuzi wa kutosha katika fani hii na sijui kama nitapata faida. Mtaji wangu ni milioni 5 tu! Nifanyaje wapendwa kwani ninapenda biashara hii tangu utoto wangu niliposoma Mwa.41:25-36 na kupata kisa hiki kizuri cha Yusufu na Farao huko Misri. Kutafakari kwangu kile alichofanya Yusufu nilipata wazo hili la kuhifadhi nafaka hivi karibuni. Mimi ni mfanyakazi mdogo katika taasisi moja ya utafiti na sina ujuzi wa kufanya biashara ila natamani sana kufanya biashara hii ili kuongeza kipato cha familia yangu huku nikihudumia jamii inayonizunguka kupitia biashara hii. Wajasiriamali tafadhalini naombeni msaada wenu muhimu!!!!!!!!
 
.....sijui kama nitapata faida.....
  • Biashara ya kuhifadhi na kuuza nafaka daima huwa haina hasara, ondoa shaka ndugu utafanikiwa.
 
  • Biashara ya kuhifadhi na kuuza nafaka daima huwa haina hasara, ondoa shaka ndugu utafanikiwa.

kweli kabisa, cha msingi ahakikishe eneo atakalohifadhi hizo nafaka ni kavu na haliruhusu unyevu ili nafaka zisioze.
Hii ni biashara nzuri sana na faida yake ni maradufu, pia hakikisha unakuwa updated na taarifa za soko mara kwa mara ili isile kwako..
 
kweli kabisa, cha msingi ahakikishe eneo atakalohifadhi hizo nafaka ni kavu na haliruhusu unyevu ili nafaka zisioze.
Hii ni biashara nzuri sana na faida yake ni maradufu, pia hakikisha unakuwa updated na taarifa za soko mara kwa mara ili isile kwako..

Ni kweli kabisaa mkuu, na upande wa mahindi hivi inalipa mkuu wangu??maana nilitaka niingie kwenye upande wa mahindi...

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom