Kuanzisha Business Bongo & Mozambique


Kwa Uzoefu wangu nilionao! kwa sasa Mji mzuri ni Maputo! ila kunauwezekano kabisa hata miji mingine kukawa kuna Biashara.
 
Kwa Uzoefu wangu mpka sasa ni Maputo, Ila hata miji mingine kutakuwa poa tu, sema sijatembea.
Mkuu upo Maputo cidade/Provincia? Na kampuni yako inaitwaje ili tuje kujionea?
 
Sante sana, saccoss zipo nyingi kule? Tukishaanzisha huku inabidi tukafungue sacco nyingine kule.
 
sidhani kama Saccos zipo.

Mhh Nahisi hakuna sacoos na kama zipo basi sio kama huku maana sijaona, Nitafanya Uchunguzi nikirudi! Now nipo Bongo nimekuja angalia biz yangu ya huku! Kwa kifupi kule vitu vingi bado wajameni, kama unakitu wataka fanya basi jaribu siku uje kama one week hivi unaangalia angalai then utaona tu kaupenyo tu. Kambi kokote wandugu! Pia Hela yao ipo juu zaidi yetu ujue. Buku ya kule ukipata sio sawa na buku la hapa.
 
Mkuu Nashukuru sana kwa thread yako na ninaimani kuwa wewe ni mpiganaji halisi;
Q: Je kuna biashara huko ambazo zinifocus kwa wazawa tuu? ninamaana kwa sisi waeni ni vigumu kuzianya? kwa mfano Building construction, ICT Consultancy na zinginezo?
Q: Je Serikali ina mtazamo gani kwa wafanyabiashara wa kigeni?

Asante.
 
Kweli kabisa jamaa hawajafunguka kabisa ujanja wao ni kutoa bidhaa South Africa, ambazo nyingi ni ghali sana kwa watu wa kipato cha chini hata kati. Ukileta bidhaa zenye ubora wa wastani kwa bei nafuu kidogo utapiga bao sana. Mimi nilifanya kazi hapo na jamaa wanaitwa Mali Yeru nilikuwa najifanyia vibiashara vyangu sana wakati wa W/end mambo yakawa poa sana.

Hata ukianzia Beira sio mbaya na kodi za nyumba utashangaa................bei ya nyumba ya ghorofa dizaini ya Mbezi Beach au Masaki kule unalipa hata Tsh laki tano. Nyumba ya laki tatu kwa mwezi duuu ni kama anayokaa jamaa anayefanya TRA- Customs bongo
 
Obrigado amigo. Já estou cá desde 2011 e consegir abrir um negócio e agora estou a fazer um bom tako. Valeu mano.
 
Niko interested sana na hii issue but naomba nikuulize maswali yafuatayo:-

1. Je ni utaratibu gani unatumika kwa kufanya biashara huko ?, je ni document za aina gani kwenye investment proposals?

2. Je unatakiwa kufungua account ya bank huko? na kama ndio kiasi gani unatakiwa ku deposit ili ku prove minimum capital has been paid?

3. , Na utaratibu wa kupata kibali cha biashara , ulipaji wa tax, usajili na jinsi ya kuingiza bidhaa huko charges zake zikoje?

Please nijibu hayo kwanza mengine tutaendelea.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…