Nikiwa naangalia taarifa ya habari, nimesikia waziri akisema wanataka kuanzisha madarasa janja akimaanisha "smart classes"
Nawaheshimu sana watu hawa wanaoitwa Prof. kwani wengi wao wamepita njia ngumu kufika walipofika.Hata hivyo hoja yangu sio kuanzishwa kwa "madarasa janja" hoja yangu ni tafsiri ya neno "smart" kwa lugha ya kiswahili kuwa ni "janja"
Je ni kweli hiyo ndiyo tafsiri?Ina maana Prof na wataalamu wote wizarani walishindwa kujua neno halisi linaloweza kuwa sawa na smart?
Tafsiri ya neno hilo ilianzishwa na Masoud Kipanya akijaribu kutafsiri neno "smart phone" akiita "simu janja".Kama tu mzaha vile kila aliyesikia akajua hiyo ndiyo tafsiri rasmi. Sasa watu wa kawaida ikawa ndiyo neno lao kuitambulisha smart phone. Shida inakuja pale wasomi nao, tena katika wizara nyeti,kuvutiwa na neno janja ( clever) kuwa lina maana ya smart bila kuchakata kidogo kupata neno halisi.
Nawapenda wakenya kwa kuwa kiswahili wanakijali na wao wanaita smart phone kama " simu tanashati"
Badala ya kuita madarasa janja ni bora wangeita darasa tanashati.Neno janja ni kama linaashiria utapeli,uswahili Swahili na mtu kutaka kulipua lipua kazi mradi awe wa kwanza kumaliza.
Mtu akikwambia acha ujanja ujanja ni kama anakwambia acha ubabaishaji.
Mimi sio nguli wala kamange wa lugha lakini nakereka kuona hatuchakati mambo na wakenya wanaoneka wako mbele yetu kwa mambo mengi.
Nawaheshimu sana watu hawa wanaoitwa Prof. kwani wengi wao wamepita njia ngumu kufika walipofika.Hata hivyo hoja yangu sio kuanzishwa kwa "madarasa janja" hoja yangu ni tafsiri ya neno "smart" kwa lugha ya kiswahili kuwa ni "janja"
Je ni kweli hiyo ndiyo tafsiri?Ina maana Prof na wataalamu wote wizarani walishindwa kujua neno halisi linaloweza kuwa sawa na smart?
Tafsiri ya neno hilo ilianzishwa na Masoud Kipanya akijaribu kutafsiri neno "smart phone" akiita "simu janja".Kama tu mzaha vile kila aliyesikia akajua hiyo ndiyo tafsiri rasmi. Sasa watu wa kawaida ikawa ndiyo neno lao kuitambulisha smart phone. Shida inakuja pale wasomi nao, tena katika wizara nyeti,kuvutiwa na neno janja ( clever) kuwa lina maana ya smart bila kuchakata kidogo kupata neno halisi.
Nawapenda wakenya kwa kuwa kiswahili wanakijali na wao wanaita smart phone kama " simu tanashati"
Badala ya kuita madarasa janja ni bora wangeita darasa tanashati.Neno janja ni kama linaashiria utapeli,uswahili Swahili na mtu kutaka kulipua lipua kazi mradi awe wa kwanza kumaliza.
Mtu akikwambia acha ujanja ujanja ni kama anakwambia acha ubabaishaji.
Mimi sio nguli wala kamange wa lugha lakini nakereka kuona hatuchakati mambo na wakenya wanaoneka wako mbele yetu kwa mambo mengi.