Kubadili fani katika utumishi wa umma

Kubadili fani katika utumishi wa umma

Yukwapi

Member
Joined
Aug 27, 2024
Posts
90
Reaction score
170
Habari Wana JF naomba kuuliza .

Je? Kunauwezekano wakubadili fani baada ya kuajiriwa ( mfano nimeajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani katika fani ya electrical na badae nikaenda kuongeza elimu nikachukua fani nyingine ya electronics and telecommunications inauwezekano wakanibadilishia fani na ngazi ya mshahara???)
 
Habari Wana JF naomba kuuliza .

Je? Kunauwezekano wakubadili fani baada ya kuajiriwa ( mfano nimeajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani katika fani ya electrical na badae nikaenda kuongeza elimu nikachukua fani nyingine ya electronics and telecommunications inauwezekano wakanibadilishia fani na ngazi ya mshahara???)
Hiyo inawezekana Mkuu,ila kwa sheria za utumishi cheo chako kinaanza upya. Kwa maana umeingia kazini na cheo cha HR Officer II, na elimu ya Degree, na umekitumiaka kwa miaka ile minne then umepanda na kuwa HR Officer I.

Sasa kama umeenda kusoma fani nyingine, then unataka kubadilisha ile kazi yako kutoka HR kwenda ICT labda, kama umesoma tena Degree, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I na kuanza upya cheo cha muundo cha Degree ambacho ni ICT Officer II.

Na kama umeenda kusoma Diploma, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I, kwenda ICT Technician II.

Ushauri, kuama taalumu inaleta maana kama mwanzo labda umeingia na Diploma then umeenda kusoma Degree, hapo moja kwa moja cheo chako kitapanda.
Inaleta maana tena kama umeingia kazini , na ndani ya mwaka mmoja tu ukiama taalumu, basi hapo hakuna issue, cheo hata kikianza upya hakuna noma kwasabubu umekitumikia ndani ya muda mfupi.

Ila kama cheo umekitumia kwa muda mrefu, na tena umeenda kusoma level ya elimu ya chini/level ile ile kwa kweli hiyo ni hasara kubwa, otherwise kipendacho roho na una uhakika unapoenda utatoboa.

Cha mwisho kabisa, kama unaweza kuama kitengo, na cheo chako kitaendelea kuwa hiko hiko basi hakuna tatizo, manake cheo kitaendelea kama kawaida. Hii inaFavor watu ambao taasisi zao ni kubwa kidogo na zina vitengo vingi. Kwa mfano wewe ni ICT OFFICER wa IDARA ya ICT, ila kuna idara nyingine inaitwa FINANCE Department, ila wanakitengo cha IT System Audit, unaweza kuamia kitengo cha Finance then unaenda kufanya hiki kitengo cha ICT, maana yake utaendelea kuitwa ICT Officer, kwahyo utaama na cheo chao.
 
Habari Wana JF naomba kuuliza .

Je? Kunauwezekano wakubadili fani baada ya kuajiriwa ( mfano nimeajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani katika fani ya electrical na badae nikaenda kuongeza elimu nikachukua fani nyingine ya electronics and telecommunications inauwezekano wakanibadilishia fani na ngazi ya mshahara???)
Ndio ila utaanz upya kimshahara , (utakuw kam muajir mpya kimshahara) au uombe special salary

Incase muajir atakuhitaji dirctly utaendelea na mshahara wa sasa
 
Habari Wana JF naomba kuuliza .

Je? Kunauwezekano wakubadili fani baada ya kuajiriwa ( mfano nimeajiriwa katika wizara ya mambo ya ndani katika fani ya electrical na badae nikaenda kuongeza elimu nikachukua fani nyingine ya electronics and telecommunications inauwezekano wakanibadilishia fani na ngazi ya mshahara???)
Ndio. uwezekano upo.
 
Hiyo inawezekana Mkuu,ila kwa sheria za utumishi cheo chako kinaanza upya. Kwa maana umeingia kazini na cheo cha HR Officer II, na elimu ya Degree, na umekitumiaka kwa miaka ile minne then umepanda na kuwa HR Officer I.

Sasa kama umeenda kusoma fani nyingine, then unataka kubadilisha ile kazi yako kutoka HR kwenda ICT labda, kama umesoma tena Degree, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I na kuanza upya cheo cha muundo cha Degree ambacho ni ICT Officer II.

Na kama umeenda kusoma Diploma, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I, kwenda ICT Technician II.

Ushauri, kuama taalumu inaleta maana kama mwanzo labda umeingia na Diploma then umeenda kusoma Degree, hapo moja kwa moja cheo chako kitapanda.
Inaleta maana tena kama umeingia kazini , na ndani ya mwaka mmoja tu ukiama taalumu, basi hapo hakuna issue, cheo hata kikianza upya hakuna noma kwasabubu umekitumikia ndani ya muda mfupi.

Ila kama cheo umekitumia kwa muda mrefu, na tena umeenda kusoma level ya elimu ya chini/level ile ile kwa kweli hiyo ni hasara kubwa, otherwise kipendacho roho na una uhakika unapoenda utatoboa.

Cha mwisho kabisa, kama unaweza kuama kitengo, na cheo chako kitaendelea kuwa hiko hiko basi hakuna tatizo, manake cheo kitaendelea kama kawaida. Hii inaFavor watu ambao taasisi zao ni kubwa kidogo na zina vitengo vingi. Kwa mfano wewe ni ICT OFFICER wa IDARA ya ICT, ila kuna idara nyingine inaitwa FINANCE Department, ila wanakitengo cha IT System Audit, unaweza kuamia kitengo cha Finance then unaenda kufanya hiki kitengo cha ICT, maana yake utaendelea kuitwa ICT Officer, kwahyo utaama na cheo chao.
Kwamantiki hyo mimi nimesoma diploma ya electrical lakini hamna maslahi ila nataka nikasome degree ya electronics and telecommunication ambayo hapohapo wizarani wanakitengo Chao na mpunga nimrefu je? Ninani ambae atahusika kunishiftia fani pindi napomaliza kusoma au nimpaka nikafanye tena interview?
 
Kwamantiki hyo mimi nimesoma diploma ya electrical lakini hamna maslahi ila nataka nikasome degree ya electronics and telecommunication ambayo hapohapo wizarani wanakitengo Chao na mpunga nimrefu je? Ninani ambae atahusika kunishiftia fani pindi napomaliza kusoma au nimpaka nikafanye tena interview?
Kila mwaka kabda ya bajeti wanafanya recatorogization kila taasisi. Kwa kifupi ni kazi za HR hiyo
 
Kwamantiki hyo mimi nimesoma diploma ya electrical lakini hamna maslahi ila nataka nikasome degree ya electronics and telecommunication ambayo hapohapo wizarani wanakitengo Chao na mpunga nimrefu je? Ninani ambae atahusika kunishiftia fani pindi napomaliza kusoma au nimpaka nikafanye tena interview?
Ukienda kusoma si unatoa taarifa? Wanapokupa ruhusa watakueleza taratibu zote. Ukisoma bila kutoa taarifa wanaweza kukukatalia kwa sababu haukuwemo katika mpango wa wizara au taasisi yako.

Amandla....
 
Ukienda kusoma si unatoa taarifa? Wanapokupa ruhusa watakueleza taratibu zote. Ukisoma bila kutoa taarifa wanaweza kukukatalia kwa sababu haukuwemo katika mpango wa wizara au taasisi yako.

Amandla....
Dahhh kwahyo wanaweza wakanikatalia hata hiyo fani nisiisome
 
Hiyo inawezekana Mkuu,ila kwa sheria za utumishi cheo chako kinaanza upya. Kwa maana umeingia kazini na cheo cha HR Officer II, na elimu ya Degree, na umekitumiaka kwa miaka ile minne then umepanda na kuwa HR Officer I.

Sasa kama umeenda kusoma fani nyingine, then unataka kubadilisha ile kazi yako kutoka HR kwenda ICT labda, kama umesoma tena Degree, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I na kuanza upya cheo cha muundo cha Degree ambacho ni ICT Officer II.

Na kama umeenda kusoma Diploma, basi cheo chako kitashuka kutoka Officer I, kwenda ICT Technician II.

Ushauri, kuama taalumu inaleta maana kama mwanzo labda umeingia na Diploma then umeenda kusoma Degree, hapo moja kwa moja cheo chako kitapanda.
Inaleta maana tena kama umeingia kazini , na ndani ya mwaka mmoja tu ukiama taalumu, basi hapo hakuna issue, cheo hata kikianza upya hakuna noma kwasabubu umekitumikia ndani ya muda mfupi.

Ila kama cheo umekitumia kwa muda mrefu, na tena umeenda kusoma level ya elimu ya chini/level ile ile kwa kweli hiyo ni hasara kubwa, otherwise kipendacho roho na una uhakika unapoenda utatoboa.

Cha mwisho kabisa, kama unaweza kuama kitengo, na cheo chako kitaendelea kuwa hiko hiko basi hakuna tatizo, manake cheo kitaendelea kama kawaida. Hii inaFavor watu ambao taasisi zao ni kubwa kidogo na zina vitengo vingi. Kwa mfano wewe ni ICT OFFICER wa IDARA ya ICT, ila kuna idara nyingine inaitwa FINANCE Department, ila wanakitengo cha IT System Audit, unaweza kuamia kitengo cha Finance then unaenda kufanya hiki kitengo cha ICT, maana yake utaendelea kuitwa ICT Officer, kwahyo utaama na cheo chao.
Umemaliza kilakitu mkuu
 
Kwamantiki hyo mimi nimesoma diploma ya electrical lakini hamna maslahi ila nataka nikasome degree ya electronics and telecommunication ambayo hapohapo wizarani wanakitengo Chao na mpunga nimrefu je? Ninani ambae atahusika kunishiftia fani pindi napomaliza kusoma au nimpaka nikafanye tena interview?
Mkuu usichelewe kufanya haya maamuzi,.......miaka ya 2012,Kuna jamaa walikua na Diploma za ualimu,wakaenda kusoma Medicine,chini ya miaka hio kawaida sana kukuta mtu mwenye division 2-ameenda ualimu,walipomaliza degree,wengi walifanyiwa recategorization,wengine walifukuzwa kazi sababu ya figisu za walimu(poverty mentality),ila wizara ya afya ikawaajiri upya wengi wamekula vitengo wameshasahau mateso.
Fanya hayo maamuzi haraka sana bila kuchelewa
 
Dahhh kwahyo wanaweza wakanikatalia hata hiyo fani nisiisome
Kukukatalia ni mara chache sana kama utasoma part-time/online, kama kwenda full time hapo sasa HR ataamua anavyoona inafaa kwa kuzingatia mtu wakuziba pengo lako.
 
Back
Top Bottom