Kubadilisha noti kutamsaidia sana Magufuli kwa sasa katika vita dhidi ya ufisadi

Nitamufikishia kama lilivyo
 
Uko serious or joke him?
 
Una badilisha note kwa sababu gani!? Unajua athari ya kubadilisha pesa zako kila wakati au unaandika tu upupu
Ni wakati muafaka wabadili maana kuna forgery. Angalia nchi zingine mfano UK noti zao wamebadili hivyo forgery inakuwa ngumu sana. JPM fanya mambo hawa wezi lazima ziwaozee huko walikoficha.
 
Ni wakati muafaka wabadili maana kuna forgery. Angalia nchi zingine mfano UK noti zao wamebadili hivyo forgery inakuwa ngumu sana. JPM fanya mambo hawa wezi lazima ziwaozee huko walikoficha.
Lini UK walibadilisha note au USA mkuu tupe mwaka ili tujifunze.
 
Lini UK walibadilisha note au USA mkuu tupe mwaka ili tujifunze.
''The polymer £20 notes, which went into circulation in February, replaced the old paper notes, leading many to question when the old currency will expire. The notes, which were released in February 2020, have been hailed as ‘the most secure banknote yet’ by the Bank of England, thanks to their plastic material.''





 
Mtoa mada umefanikiwa!

Likifanyika hilo waliokushambulia wata kuheshim sana.

Tena ningependa iwe ghafla.

Mara paaap! Noti mpya hiyo!!, itolewe window period ya aliekua na noti nyumbani kuja kutoa maelezo genuine.

Binafsi naamini fedha za ugaidi na mambo mengine yenye hila kwa nchi yetu yanaweza kuwa cheked namna hiyo.
 
Ni layman tu ndo anaweza kuzani kuwa pesa imeadimika sababu Eti kutakuwa na watu wamezifungia majumbani au maofisini mwao [emoji3][emoji3][emoji3]
 

fanya utafiti kwanza ndugu yangu, pesa aichapishwi bure,,,kuna gharama zake nazo ni kubwa tu. Nakumbuka makampuni haya yafuatayohuko nyuma yalikuwa yaki print pesa zetu,
Giesecke & Devrient -german,
Crane Currency AB - Sweeden
Thomas De La Rue -UK
Gharama ya kuchapisha inaendana na thamani ya pesa ichapishwayo/

mfano kwa The USA
DenominationPrinting Costs
$1 and $27.7 cents per note
$515.5 cents per note
$1015.9 cents per note
$2016.1 cents per note
 
Mwandishi unajisikiaje sasa? mjinga, mpumbavu vyote umeitwa wewe kwa sababu ya haka kathread tu
 
Hivi kwa akili yako, mtu ana weka noti ya Tanzania ndani? Hao labda waswaga ng'ombe. Watu wanao jua thamani ya hela huzibadilisha kuwa pesa mzee.. Yaani dolari.. Ndio wana weka ndani. Lbda mwambie aongee na Biden abadilishe dola[emoji133]
Abadilishe Dollar tena
 

Tu - assume, unachodhani ni kweli na halisi...

Kama ndivyo, maana yake ni moja tu...

Kuna shida au mapungufu makubwa kwenye SERA za kiuchuni za serikali ya CCM chini ya Rais John Pombe Magufuli...

Ni Sera ambazo ni very unpredictable, they create uncertainty & economic insecurity to investors. Hata hili unalopendekeza/shauri lifanyike ni ktk kutekeleza sera mbovu za kiuchumi kwa kudhani ni suluhisho...

SULUHISHO LAKE NINI?

Arekebishe SERA zake za kiuchumi. Serikali ije na sera zinazotoa economic security assurance kwa internal & external investors...

Serikali ije na sera itakayowafanya watu wenye fedha badala ya kuzihifadhi mahali kwa mfumo wa USD au Rupee au Pound Sterling nk waziachilie ziwe katika mfumo wa invested assets...

Hii ina manufaa makubwa sana kwa sbb na tatizo la ajira linaweza kutatuliwa kwa kiasi kikubwa na hili...
 
Mara nyingi sana watu wenye tabia kama hizi huwa hawana kitu,huwa wanafikiri ili wao wafarijike basi alienacho awe kama yeye,huu ni wivu wakijinga.

Ndio maana vijijini kurogana ni kwingi kuhakikisha hakuna kwenda mbele.
Hata wewe kama si mwanga basi mchawi na kama huna vyote hivyo basi uko mbioni kuvitafuta ili kukurahisishia kuroga wale unaowaona wanakuzidi kimaendeleo.

Nakushauri badilika ukimuona mwenzako kakuzidi wewe pambana kutafuta uwe zaidi yake kinyume chake utabaiki hivyohivyo na ufakara wako.
 
Ni nani tajiri mjinga ataficha fedha zake kabla ya kuzibadilisha kuwa riyal au dollar?
 
Yaani mkuu umekosa kitu cha kuandika/kusifia humu ili ulipwe umeona uandike ujinga huu???
 
Sijaelewa vizuri apa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…