Kubanwa mkojo kila wakati

Mwana ali

Member
Joined
Jan 19, 2013
Posts
14
Reaction score
6
Habari zenu wapenwa mi nna ujauzito wa miezi minne tatizo nilonalo ni kwamba naenda haja ndogo mara kwa mara hasa usiku na nikiuhisi tu mkojo nakua navimba chini ya kitovu na kuuma kidogo ila nikishakojoa tu nakua wa kawaida, je hili ni tatizo au kawaida kwa wajawazito?
 
Mimi ninavyojua ni kitu cha kawaida kwa wajawazito,ngoja na wengine waje.
 
Hili ni jambo la kawaida sana, ikumbukwe mfuko wa uzazi (uterus) upo nyuma ya kibofu cha mkojo (urethra), mama anapopata ujauzito kuna kuwa na mgandamizo kwenye kibofu cha mkojo kutokana na mfuko wa kizazi kukandamiza kibofu cha mkojo, ila ukishakojoa inaisha,. Jaribu kuzoea hii hali mpaka hapo utakapojifungua ndipo itakapoisha na hali hii haina madhara ila usikae na mkojo muda mrefu!!
 

Hiyo ni kawaida shemeji kwa wajawazito na inasababishwa na uzito wa mtoto kubana kibofu cha mkojo.Hongera sana naona hizi mvua umetumia vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…