Kubebana kunavyoathiri dhana na dhima ya taasisi zetu

Dogoalice

New Member
Joined
Mar 16, 2013
Posts
2
Reaction score
1
Jana niliaidi kueleza japo kwa ufupi tu kile kinachoendelea kwenye taasisi ya umma tena ya elimu ya juu ambapo asasi za kijamii, taasisi binafsi, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGOs), mashirika wakala ya serikali na hata watu binafsi (mmojammoja) walioowengi wangependa kujifunza kutoka hapo maswala mbalimbali ya kiutawala (utawala bora) na elimu (elimu bora). Mambo hayo makuu mawili yamekuwa ni kinyume na mategemeo ya wengi.
Kuna watu wamekuwa wakifanya maamuzi bila kufuata taratibu na sheria hatimaye kuleta athari mbaya (negative impact) kwa taasisi au kwa watu binafsi. Wewe kama kiongozi katika ngazi ya kwanza na unataka kufanya maamuzi ya ngazi ya pili tena bila hata kumshirikisha huyo wa ngazi ya pili, unataka kumaanisha nini? ua unataka kuonesha wakubwa kwamba huyu wa ngazi ya pili hawezi kazi? Mbona unataka cheo kwa nguvu? Hujui kama huyu yupo hapo kihalali? ukubwa (umri) na kielimu kakuzidi, sasa wewe na elimu yako ya kuungaunga unataka leo uwe cheo cha pili. Kwanini usikae utulie usome ili uwe na vigezo kama wenzako? Hakika wewe ni mjinga ila ninaamini ukikaa na watu wakikutoa ujinga utaelewa haya ninayoyasema.Watu hawalali wanavurugwa na ujinga wako!! Hii si sawa hata kidogo. Nasema hivi kwasababu binadamu ni wavumilivu sana ila ipo siku uvumilivu ukiwashinda watakubadilikia kwa yale uliyowatendea.
Nilikuwa najaribu kuwahoji wale unaowatumia kama ndio washauri wako kumbe nao ni bomu kuliko wewe mwenyewe. kama wewe ni mjinga usitumie wajinga kama washauri wako maana watakushuri vibaya. Kwani haujifunzi tu mpaka hapo ulipofika? Watu wanakereka sana kwa hayo unayofanya. Badilika kabla na ufanye kazi kwa taratibu na sheria inavyokuongoza. najua elimu yako ndogo lakini tumia busara na hekima kufanya maamuzi. Huenda ukawa umekuja hapa kwa kubebwa basi kaza buti usome na ufaulu ili hata mwingine asjue kama unabebwa tu.
Muda tu umenibana hapa nitafunguka zaidi baadaye.
Asanten
 
Dogoalice achq hii maneno, Kwani hapo ofisini kwenu hamna platform ya kuiongelea hii maneno.


Kwa sababu haujataja hata taasisi au mtu unayemlenga kwa hiyo ni kazi huyo mtu kujilekebisha, au kuwa mtazamaji kwanza kabla ya kuleta thread ili ujifunze namna gani watu wanaandaa mada humu kwenye jamvi,

Na punguza jazba mkuu.
Join Date : 16th March 2013
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…