Kubenea wa MWANAHALISI amenunuliwa na mafisadi?

Huyu mtoa mada katumwa na wanaotuhumiwa kutaka kujiunga na ccj.haiingii akilini issue ya parokwa kuandikwa kwenye mwanahalisi ni mpango wa rostam.nasema hivi wote wameandika issue ya parokwa lakini s.kubenea jumatano atahitimisha.
 
Huyu mtoa mada gamba jipya hili katumwa na mwendawazimu mwenzake NAPE,KUBENEA IS VERY BRIGHT.
 
Kwa hiyo asiandike habari nyingine zaidi ya Riwaya Za Rostam na Lowasa nini maaana ya Habari sasa Kisa 20Mil kaazi kweli kweli


Sidhani kama Kubenea yupo cheep kiasi hicho........
 

Hapa hujatueleza kitu labda umetumwa. Kama umetumwa kaanze upya
 
Siye KUBENEA nimfahamuye mimi,labda wewe una lako jambo

nyie ndio hamtakii mema Tanganyika yetu mnataka kila siku iwe kama jana na nyie wachache mfaidi maliasili kana kwamba mmepewa kibali na mungu

kamwe hatutawapa nafasi hiyo,anza kujiandaa kabla hatuja kuumbuwa
 
Hizi ni habari za uzushi. Habari za uhakika nilizopata kwa mtu wa karibu na Kubenea ni kwamba mtambo wa kuchapa kisha nunua kutoka kwa Mengi -- ule wa zamani uliokuwa unatumika kuchapishia magazeti yake ya IPP media hadi 2006 aliponunua mpya. Mtambo huo ni mzima ingawa ni wa kizamani kidogo. Sijui bei aliyonunulia lakini nasikia ilikuwa ni bei rahisi tu kwa sababu Mengi na Kubenea wana uelewano mzuri kutokana harakati zao za vita dhidi ya mafisadi.

Kisha toa instalment moja na nyingine atalipa polepole pale atakapoanza kuchapisha magazeti yake na pengine ya wateja wengine. Hivi sasa yuko mbioni kutafuta mahal;i pa kuufunga.

Linganisha huyu kijana Kubenea na Habari Corporation kamopuni ya Rostamu -- nasikiavyo sasa hivi wanahangaika kupiga chapa magazeti yao, walikimbia Jamana kutokana na deni kubwa wakaenda Mwananchi ambako ni bei ghali sana. Nasikia wameshindwa na wamerudi tena Jamana bila aibu. Wakati huo huo nasikia wafanya kazi hawajalipwa mishgahara ya Aprili, na sasa Mai inamalizika.
 

Ni kweli Kubenea kanunua mtambo wa IPP ule wa zamani. Nasikiavyo amemuuzia kwa Sh milioni 150 tu na kuambiwa kulipa sh milioni 20 za awali. Gazeti linalouza nakala zaidi ya 70,000 kila wiki ataweza kweli kubenea kukosa milioni 20 hadi alambe miguu ya RA, mtu ambaye amekuwa anampiga vita kwa ufisadi wake?

MODS ondoa thread hii mara moja ni ya kutunga tu.
 
si amini kama kweli kubenea(jembe)lifanye hivyo! It is a matter of tyme let us wait.
 
Objective ni kumzuia Kubenea kuandika story ya Porokwa maana wanamjua Kubenea anavyojua kuweka utamu kwenye hoja. wanahofu hao! hakuna cha kununuliwa na RA au EL, wao wenyewe wakikusikia watakucheka, maana wanamjua Kubenea. Unafiki wa akina Nape, Sita na Mwakyembe lazima uanikwe kama ulivyoanikwa uovu wa akina RA na EL kiasi kwamba sasa tunawajua vilivyo. sasa endelea kuwaanika wote usimwache hata mmoja ili mwisho tupate cream ya watu waadilifu wenye uchungu wa kweli na si waganga njaa.
 
Kubenea - kutiwa mfukoni na mwizi RA? Impossible! It's not true at all. Yaani huyu RA na EL wake waliotuma watu kutaka kumpofua macho na hata kumuuwa, Kubenea ambaye hadi sasa macho yake yameathirika na kubidi kwenda India mara kwa mara kwa matibabu ageuke kuwa kibaraka wa RA?

Hiyo kesi yake baadaye ilifutwa kwa nguvu za RA ambaye alimhonga Tibaigana kuvuruga ushahidi, huku shahidi mmoja muhimu alikimbizwa Kenya!

Hapana. Kubenea hawezi kamwe kufanya hivyo -- na siku ikiwa kweli atafanya hivyo mie naweza kujitundika! Ukweli ndo huo!
 
Hata mie nimesikia mtambo aliuziwa na Mengi, ule wake wa zamani kwa Sh milioni 200 na kalipa tayari milioni 20 cash! RA anaingia vipi hapo, huku yeye na Mengi hawawivi?

Mtoa mada mzushi wa kupindukia!
 
This is nonsesnse! Kubenea hawezi kujidhalilisha namna hiyo kwa mdosi. hakika mafisadi sasa wanatapatapa! Ukiamini hii pia ni lazima utaamini kwamba JK ni mwanachama wa CDM kisirisiri.
 
mwehu uyo m/halisi ni taasisi iuzayo nakala nyingi sana sembuse kurubuniwa kwa sh 20mil...au ni dola

WanaJF, maandishi hayaozi. Mtoa mada ametuambia kuwa jumatano kutaandikwa habari za Porokwa na jumatano si mbali na hii thread huenda itakuwepo na kama haitakuwepo karibu tutaihuisha ili kujua ili kumsuta mtoa mada ama kumuona shujaa kwa kutupa habari za ndani. Tusimhukumu kwa sasa ila tusubiri jumatano tuone kisha ahukumiwe kama aliyoyasema hayatatokea. Jamani mafisadi si watu wa kuandermine wanaweza kufanya lolote they can turn a hero to a zero!!
 
 

Sikubaliani nawe kabisa! Kutoa stori ya Porokwa si kitu cha kuprove kwamba Kubenea katiwa mfukoni -- kwani stori za namna hiyo ndo zake Kubenea daima dumu. Bila shaka mtoa mada kesha ambiwa kuwa kutakuwapo stori hiyo (usiku huu gazeti tayari limekwenda mtamboni) kwa hivyo kwa kuwa lazima gazeti litakuwa na stori hiyo ya Porokwa basi mtoa mada anajaribu kuiforce hoja yake kwa kuiunganisha na uwepo wa hiyo stori Jumatanao.

A very cheap way of raising an issue!.
 

Porokwa kapewa pesa kala mwenyewe wakati sisi ndio tuliomfanyia kampeni na kumlinda hapa mjini Arusha akiwa anaishi kwa mifuko yetu? Basi hafai maana yeye ndiye aliyetumwa kuanzisha ccj hapa Arusha akawaingiza watu fulani hasara ya ajabu kabisa, baada ya kuutosa ubunge akatutoroka kabisa, tutamkamata na siri zake tunazo maana sisi ndio tuliombeba.
 
majungu tu hana lolte huyu mtoa mada, yaani mwenzetu mpaka toleo lijalo ameshajuwa litaandika nini, kama si wehu huu tuuwitaje?

Inawezekana anajua ndg yangu, cku hizi hakuna siri Tanzania ndg yangu, unafki kila mahali! Hukumbuki suala la Mwakyembe? La Mengi je? Ufalme umegawanyika huu.
 
Kama ni kweli basi money can buy anything except peoples' power!!! Lakini nina wasiwasi mkubwa na mtoa mada hivi ni mtambo wa aina gani unaouzwa mil.20 labda tupe ufafanuzi kidogo!!

Photocopy Machine toleo la 2011
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…